Return to Video

Je dini yangu inasema nini hasa kuhusu wanawake?

  • 0:01 - 0:04
    Njiani kufika hapa,
  • 0:04 - 0:08
    nilikuwa na mazungumzo mazuri na
    mtu aliyekuwa anakaa pembeni yangu kwenye
  • 0:08 - 0:11
    ndege. Alinambia
  • 0:11 - 0:14
    "Hamna kazi tena USA,
  • 0:14 - 0:16
    yaani sasa wamebuni kazi mpya:
  • 0:16 - 0:21
    mwanasaikolojia wa paka,
    mzungumzaji wa mbwa,msasi wa kimbunga."
  • 0:21 - 0:24
    Punde, aliniuliza,
  • 0:24 - 0:27
    "Kwani wewe unafanya kazi gani?"
  • 0:27 - 0:30
    Nikamjibu, "Mjenzi wa usalama?"
  • 0:30 - 0:33
    (Vicheko)
  • 0:34 - 0:39
    Kila siku, nafanya bidii
    kuwazidishia wanawake sauti
  • 0:39 - 0:43
    na kuoneysha maisha yao na michango yao
  • 0:43 - 0:46
    katika hatua za kutafuta usalama
    na kutatua migogoro,
  • 0:48 - 0:53
    na kwa sababu ya kazi zangu,
    natambua kwamba njia ya pekee
  • 0:53 - 0:55
    kwa kuhakikisha ushirikiano kamili
  • 0:55 - 0:59
    wa wanawake duniani
    ni kuchukua tena dini mikononi mwetu.
  • 0:59 - 1:03
    Sasa, jambo hilo ni muhimu sana kwangu.
  • 1:03 - 1:07
    Kama muislamu na mwanamke kijana,
    ninaijali dini yangu sana.
  • 1:08 - 1:12
    Inanipa nguvu na msimamo katika
    kazi zangu kila siku.
  • 1:12 - 1:15
    Ndiyo sababu inayoniwezesha
    kusimama hapa leo mbele yenu.
  • 1:16 - 1:20
    Lakini siwezi kutojali hasara kubwa
    zilizofanyika kwa kutumia jina la dini,
  • 1:21 - 1:25
    si dini yangu tu, lakini
    dini zote kubwa za dunia.
  • 1:25 - 1:30
    Kuyatumia vibaya na
    kuyageuza maandiko ya kidini
  • 1:31 - 1:34
    kumebadilisha desturi zetu
    za kijamii na kitamaduni,
  • 1:34 - 1:37
    sheria zetu, kila siku zetu,
  • 1:37 - 1:40
    hadi kumefikia tusipoweza
    kupagundua.
  • 1:40 - 1:45
    Wazazi wangu walihama Libya,
    Afrika ya Kaskazini kwenda Kanada
  • 1:45 - 1:47
    mwanzoni mwa miaka 1980,
  • 1:47 - 1:51
    na mimi niko katikati ya watoto 11.
  • 1:51 - 1:53
    Ehee, 11.
  • 1:54 - 1:55
    Lakini katika kukulia kwangu,
  • 1:55 - 2:00
    niliwaona wazazi wangu, wote wacha Mungu
    na waumini wa Akhera, wakisali na
  • 2:00 - 2:02
    kumshukuru kwa baraka zao,
  • 2:02 - 2:06
    kama mimi, lakini zinginezo pia.
    (Vicheko)
  • 2:07 - 2:10
    Walikuwa na huruma, wenye kuchekesha,
    na wenye subira,
  • 2:10 - 2:15
    subira kubwa, aina inayofunzwa
    kwa kuwalea watoto 11.
  • 2:16 - 2:18
    Pia walifanya haki.
  • 2:18 - 2:22
    Sikuwahi kupaswa kuijua dini kwa
    mtazamo wa kitamaduni tu.
  • 2:23 - 2:25
    Nilitendewa sawasawa na kaka zangu,
    na sisi sote
  • 2:25 - 2:27
    tulikuwa tunatarijiwa
    kufanya sawasawa.
  • 2:27 - 2:32
    Sikuwahi kuambiwa kwamba Mungu
    huhukumu tofauti kwa jinsia.
  • 2:33 - 2:40
    Wazazi wangu walimwona Mungu kuwa
    Mwingi wa Rehema, Fadhila na rizki
  • 2:40 - 2:42
    na mimi nilichukulia
    msimamo wao.
  • 2:43 - 2:46
    Kwa uhakika, malezi yangu yalikuwa
    na faida zake.
  • 2:47 - 2:51
    kuwa katikati ya watoto 11
    ni kama Diplomasia 101. (Vicheko)
  • 2:52 - 2:55
    Mpaka leo, watu huniuliza wapi
    nilipokwenda skule,
  • 2:55 - 2:58
    kama, “Ulienda Skule ya
    Kennedy ya Serikali?"
  • 2:58 - 2:59
    na mimi huwatazama na
    kuwambia, “Hapana,
  • 2:59 - 3:03
    Nimeenda Skule ya Murabit ya
    Mambo ya Kimataifa.”
  • 3:03 - 3:08
    Ni maalum sana. Ungeongea na
    Mamangu kwa kujipatia nafasi
  • 3:08 - 3:11
    Lakini kwa bahati yenu, yupo leo.
  • 3:12 - 3:16
    Lakini kuwa miongoni wa watoto 11,
    na kuwa na ndugu 10,
  • 3:16 - 3:20
    kunafundisha mengi kama
    mifumo ya mamlaka na muungano.
  • 3:20 - 3:23
    Kama kuzingatia lengo;
    useme haraka au
  • 3:23 - 3:26
    usiseme sana, kwa sababu
    utadakiwa mazungumzo kila mara.
  • 3:26 - 3:28
    Kunafundisha umuhimu wa kuwa
    mjumbe mzuri.
  • 3:29 - 3:33
    Uyaulize maswali kwa mpango kwa
    kupata jibu unalolitaka, na
  • 3:33 - 3:36
    ujue kusema 'la' kwa mpango pia
    kwa kufuliza usalama.
  • 3:37 - 3:41
    Lakini funzo muhimu sana
    nililolipata kutoka utoto wangu
  • 3:41 - 3:44
    lilikuwa umuhimu wa kuwa na nafasi kwenye
    meza.
  • 3:45 - 3:48
    Taa yake ndogo mamangu ilipovunjika,
    alivyoipenda sana, ilinilazimu niwepo
  • 3:48 - 3:53
    wakati alipochunguza ilikuwaje,
    ili nijitetee,
  • 3:54 - 3:57
    kwa sababu kama hupo,
    lawama inakuangukia kwako,
  • 3:57 - 4:00
    na kabla hujagundua, utakuwa umeadhibiwa.
  • 4:00 - 4:03
    Kwa uhahika, sijapewa
    adhabu mimi mwenyewe.
  • 4:04 - 4:09
    Nilipokuwa na miaka 15 mwakani 2005,
    nikatimiza skule ya sekondari nikahamia
  • 4:09 - 4:11
    Kanada-- Saskatoon --
  • 4:12 - 4:16
    Ila Zawiya, Libya,
    mji wa nyumbani wa wazazi wangu,
  • 4:16 - 4:18
    mji wa kidesturi sana.
  • 4:18 - 4:23
    Fikiri, muda huo niliwahi kufika
    Libya kwa ajili ya matembezi tu,
  • 4:23 - 4:28
    na kama msichana wa miaka 7,
    ilipendeza sana.
  • 4:28 - 4:32
    Ilikuwa aiskrimu na pwani na jamaa
    wenye furaha.
  • 4:34 - 4:38
    niligundua haiko vilevile kama
    msichana wa miaka 15.
  • 4:38 - 4:44
    Nikakutana upesi na mambo ya dini ya
    kiutamaduni.
  • 4:45 - 4:49
    Maneno ya "haramu" --
    lenye maana ya kukatazwa kidini --
  • 4:49 - 4:52
    na "aibu" -- lenye maana ya kutofaa
    kimaadili --
  • 4:52 - 4:55
    yalibadilishanwa bila mpango.
  • 4:55 - 4:59
    kama yalikuwa na maana moja na
    adhabu moja vilevile.
  • 5:00 - 5:04
    Nikajikuta sana katika mazungumzo na
    wenzangu wa skule
  • 5:04 - 5:08
    na wa kazi, profesa, rafiki zangu na hata
    jamaa zangu,
  • 5:08 - 5:12
    nikaanza kujiuliza kuhusu desturi zangu
    na malengo yangu.
  • 5:12 - 5:16
    Na hata na msingi mzuri niliopokea
    kutoka wazazi wangu,
  • 5:16 - 5:20
    Nilijikuta nikajiuliza kuhusu nafasi
    ya mwanamke katika dini yangu.
  • 5:22 - 5:24
    Kule kwenye Skule ya Murabit ya Mambo
    ya Kimataifa,
  • 5:24 - 5:27
    tunapenda sana kufanya mjadala,
  • 5:27 - 5:33
    na sheria ya kwanza ni fanya utafiti wako,
    na hivyo ndivyo nilivyofanya mimi,
  • 5:33 - 5:36
    Ikanishangaza sana vipi ilikuwa rahisi
  • 5:36 - 5:40
    kuwagundua wanawake katika Uislamu
    waliokuwa viongozi,
  • 5:40 - 5:44
    wavumbuzi, wenye nguvu --
  • 5:44 - 5:47
    za kisiasa, za kiuchumi hata za kijeshi.
  • 5:47 - 5:51
    Khadija aliziendesha fedha za
    harakati za Kiislamu
  • 5:51 - 5:53
    katika siku zake za mwanzo.
  • 5:53 - 5:55
    Tusingekuwepo hapa leo bila michango yake.
  • 5:56 - 5:58
    Kwa nini tusifundishwe kisa chake?
  • 5:58 - 6:01
    Kwa nini tusifundishwe
    visa vya hao wanawake?
  • 6:01 - 6:04
    Kwa nini wanawake wapewe vyeo
    vilivyotoka
  • 6:04 - 6:07
    zama zilizotangulia mafunzo ya dini yetu?
  • 6:07 - 6:09
    Na kwa nini, kama sisi sote tuko sawasawa
    machoni mwa Mungu,
  • 6:09 - 6:12
    hatuko sawasawa machoni mwa binadamu?
  • 6:13 - 6:17
    Hayo yalinipeleka kufikiria mafunzo
    yangu ya utotoni.
  • 6:18 - 6:22
    Anayeamua, na kuwa na mamlaka
    juu ya ujumbe,
  • 6:22 - 6:25
    anayo nafasi kwenye meza,
  • 6:25 - 6:29
    na kwa bahati mbaya, katika dini zote
    za kidunia,
  • 6:29 - 6:31
    hao si wanawake.
  • 6:32 - 6:35
    Taasisi za kidini
    zinatawaliwa na wanaume
  • 6:35 - 6:37
    na kuendeshwa na viongozi vya kiume,
  • 6:37 - 6:41
    na wanabuni sera zinazowafaa wanaume tu,
  • 6:41 - 6:45
    na ila tunaweza kubadilisha mfumo huo
    kabisa, kwa kweli hatuwezi
  • 6:45 - 6:48
    kutarajia wanawake kushiriki
    kwa ukamilifu
  • 6:48 - 6:50
    katika uchumi au siasa.
  • 6:52 - 6:54
    Msingi wetu umevunjika.
  • 6:56 - 7:00
    Mamangu husema, "huwezi kujenga nyumba
    nzima juu ya msingi mbovu".
  • 7:03 - 7:09
    Mwakani 2011, Mapinduzi ya Libya yaliripuka
    na aila yangu walikuwepo mistari ya mbele.
  • 7:10 - 7:13
    Kuna jambo moja la kushangaza
    linalojitokeza katika vita,
  • 7:13 - 7:15
    kama mageuzo ya kiutamaduni,
    kwa muda mfupi tu.
  • 7:16 - 7:19
    Kwa mara ya kwanza nilijisikia
    ilikubaliwa, au hata
  • 7:19 - 7:22
    ilisisitizwa kwa mimi kujihusisha
    na mambo.
  • 7:22 - 7:24
    Ilihitajika.
  • 7:25 - 7:27
    Mimi na wanawake wengine walipewa nafasi
    kwenye meza.
  • 7:27 - 7:31
    Hatukuwa wasaidizi wa wanaume tu.
  • 7:31 - 7:32
    Tulichangia katika uamuzi.
  • 7:32 - 7:36
    Tulichangia katika kutoa taarifa.
    Tulikuwa muhimu sana.
  • 7:36 - 7:40
    Na mimi nilitaka, nilihitaji mageuzo hayo
    kutoondoka.
  • 7:43 - 7:45
    Lakini niligundua si rahisi
    kuwa nilivyotaka.
  • 7:45 - 7:49
    Ilichukua wiki chache tu kabla hao
    wanawake niliowafanya nao kazi
  • 7:49 - 7:52
    walikuwa wanarejea katika kazi zao za
    zamani,
  • 7:52 - 7:56
    na wengi walipewa maneno ya
    kusisitizwa
  • 7:56 - 7:59
    kutoka kwa viongozi wa kidini na
    vya kisiasa, wengi wao
  • 7:59 - 8:02
    walijaribu kuthibitisha hoja
    zao kwa maandishi ya kidini.
  • 8:02 - 8:06
    Ndivyo walivyojipatia mikono ya
    watu katika hoja zao.
  • 8:07 - 8:12
    Mwanzoni, nilizingatia kuwapa
    wanawake nguvu katika siasa na uchumi.
  • 8:12 - 8:15
    Nikafikiri ingeliongoza
    mabadiliko ya kiutamaduni na kijamii.
  • 8:16 - 8:20
    Niligundua, ilifanikiwa kidogo tu, lakini
    sio sana.
  • 8:20 - 8:24
    Nikaamua kuitumia njia yao wale
    viongozi wa kidini
  • 8:24 - 8:28
    nikaanza kuthibitisha hoja zangu kwa
    maandishi ya kiislamu pia.
  • 8:29 - 8:33
    Katika miaka 2012 na 2013, shirika langu
    liliongoza kampeni ya pekee iliyokuwa
  • 8:33 - 8:36
    kubwa na pana kuliko zote Libya.
  • 8:37 - 8:40
    Tulipenyeza nyumbani, skuleni na
    vyuoni, hata misikitni.
  • 8:41 - 8:44
    Tulizungumza na watu 50,000
    uso kwa uso, na mamia ya maelfu zaidi
  • 8:45 - 8:47
    kwa njia za
    matangazo ya kubandika,
  • 8:47 - 8:49
    matangazo kwenye tv na kwenye radio.
  • 8:51 - 8:53
    Labda mnajiuliza, shirika la
    haki za wanawake
  • 8:53 - 8:57
    waliweza kufanya hivyo vipi katika jamii
    ilyopingana na sisi
  • 8:57 - 8:58
    kabisa mwanzoni.
  • 8:59 - 9:02
    Niliyatumia maandishi ya kiislamu.
  • 9:02 - 9:06
    Nilitumia aya za Korani na misemo ya
    Mtume Mohammed,
  • 9:07 - 9:11
    Hadithi zake, misemo yake ambayo ni,
    kwa mfano,
  • 9:12 - 9:15
    "Mtu bora ndiye anayefanya
    wema kwa familia yake."
  • 9:15 - 9:18
    "Usimruhusu mtu kumdhulumu mwingine."
  • 9:19 - 9:24
    Kwa mara ya kwanza, hotuba za Ijumaa
    kutoka kwa imamu wa kienyeji
  • 9:24 - 9:26
    zilitangaza haki za wanawake.
  • 9:26 - 9:30
    zilizungumzia masuala yasiyo kawaida, kama
    vurugu ya nyumbani.
  • 9:31 - 9:33
    Sera zilibadilishwa.
  • 9:34 - 9:39
    Katika jamii fulani, ilitubidi
    kusema lile Azimio
  • 9:39 - 9:42
    la Kimataifa la Haki ya Wanadamu
    mlilopingana nayo
  • 9:42 - 9:45
    kwa sababu haikuandikwi na watalaamu
    wa kidini,
  • 9:45 - 9:49
    eti, misingi yote ile imo kitabu chetu.
  • 9:50 - 9:53
    Yaani, Shirika la Umoja wa Mataifa
    lilituiga tu.
  • 9:56 - 9:59
    Kwa kuubadilisha ujumbe wenyewe,
    tuliweza kuitoa
  • 9:59 - 10:03
    sura mpya iliyotangaza haki za wanawake
    Libya.
  • 10:03 - 10:06
    Ni jambo ambalo sasa limeigwa duniani,
  • 10:09 - 10:12
    na sisemi ni rahisi--- niamini,
    si rahisi kabisa.
  • 10:13 - 10:17
    'Liberals' watasema unaitumia dini
    na kukuita 'conservative' mbaya.
  • 10:17 - 10:20
    na 'conservatives' watakupa
    matusi mengi.
  • 10:20 - 10:24
    Mimi mwenyewe nimeyapata mengi, kama
    "Wazazi wako hawaaibiki na wewe?" --
  • 10:24 - 10:26
    sio kweli;
    wao wananipenda kuliko wote --
  • 10:26 - 10:29
    au "Hutoishi kuona siku
    yako ya kuzaliwa tena" --
  • 10:29 - 10:31
    tena sio kweli, nimeshaiona.
  • 10:33 - 10:37
    Na bado, ninaamini kabisa
  • 10:37 - 10:40
    kwamba haki za wanawake
    na dini zinaweza kuendana.
  • 10:42 - 10:46
    Lakini lazima tupewe nafasi kwenye meza.
  • 10:46 - 10:49
    Tusiache kupigania
    nafasi yetu, kwa sababu
  • 10:49 - 10:55
    kwa kukaa kimya, tunaruhusu mateso na
    dhuluma za wanawake duniani kuendelea.
  • 10:56 - 10:59
    Kwa kudai tutapigania haki za wanawake
  • 10:59 - 11:02
    na kupigania ugaidi kwa kutumia
    mabomu na vita,
  • 11:03 - 11:07
    tunaharibu jamii za kienyeji zinazohitaji
    kuyashughulikia masuala hayo
  • 11:08 - 11:11
    ili yawezekane kuendelea.
  • 11:12 - 11:16
    Sio rahisi, kushindana na taarifa za dini
    za kupotosha.
  • 11:17 - 11:22
    Utapata vyako vya matusi na dhihaka na
    vitisho.
  • 11:22 - 11:24
    Lakini ni lazima ifanyike.
  • 11:24 - 11:29
    Hatuna budi ila kuuchukua tena
    ujumbe wa haki za binadamu,
  • 11:29 - 11:33
    maadili ya dini yetu, si kwa ajili yetu,
  • 11:33 - 11:35
    na si kwa ajili ya
    wanawake wenu tu,
  • 11:35 - 11:36
    si kwa ajili ya
    wanawake humu leo,
  • 11:36 - 11:39
    hata si kwa ajili ya
    wanawake kule nje,
  • 11:40 - 11:43
    bali kwa ajili ya jamii ambazo
    zingebadilika kuwa nzuri
  • 11:43 - 11:46
    kwa mashirikiano ya wanawake.
  • 11:46 - 11:49
    Na jinsi ya pekee sisi tunavyoweza
    kufanya hivyo,
  • 11:49 - 11:50
    njia yetu moja tu,
  • 11:50 - 11:53
    ni kupata nafasi na kukaa daima,
    kwenye meza.
  • 11:54 - 11:55
    Asante.
  • 11:55 - 11:58
    (Makofi)
Title:
Je dini yangu inasema nini hasa kuhusu wanawake?
Speaker:
Alaa Murabit
Description:

Familia ya Alaa Murabit ilihamia Canada kutoka Libya alipokuwa na miaka 15. Kabala alijiona yuko sawa na kaka zake, lakini katika mazingira haya mapya alihisi vizuizi kuhusu yale mafanikio anayoweza kuyapata. Kama mwanamke wa Kiislam , alijiuliza kama haya kweli ni mafundisho ya dini? Kwa namna ya kuchangamsha anatushirikisha ugunduzi wa mifano ya viongozi wanawake katika historia ya imani yake - Na jinsi alivyoanzisha kampeni ya kupigania haki za wanawake kwa kutumia mistari ya Korani.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
12:13

Swahili subtitles

Revisions