Return to Video

Uzuri wa ambavyo hatutovijua

  • 0:01 - 0:05
    Asubuhi moja ya mwezi Oktoba yenye joto,
  • 0:05 - 0:07
    nilishuka kutoka kwenye treni ya usiku
  • 0:07 - 0:09
    Mandalay,
  • 0:09 - 0:12
    mji mkuu wa kifalme wa zamani wa Burma,
  • 0:12 - 0:13
    sasa Myanmar.
  • 0:14 - 0:18
    Kwenye mtaa, nikakutana na kundi la
    wanaume ambao ni wakorofi
  • 0:18 - 0:22
    wakiwa wamesimama pembeni ya baiskeli zao.
  • 0:22 - 0:23
    Mmoja kati yao akanifuata
  • 0:23 - 0:25
    na kujitolea kunionesha maeneo.
  • 0:27 - 0:29
    Bei aliyoitaja ilikuwa ni ya kushangaza.
  • 0:30 - 0:34
    Ilikuwa ni kidogo kuliko ambayo ningetumia
    kununua chokoleti nyumbani.
  • 0:34 - 0:37
    Nikapanda kwenye baiskeli yake,
  • 0:37 - 0:43
    na akaanza kutuendesha polepole
    kwenye makasri na mahekalu.
  • 0:44 - 0:49
    Wakati anaendesha, akaniambia jinsi
    alivyokuja mjini kutoka kijijini kwake.
  • 0:49 - 0:52
    Alikuwa na digrii ya hisabati.
  • 0:52 - 0:54
    Ndoto yake ilikuwa awe mwalimu.
  • 0:54 - 0:59
    Hakika maisha ni magumu kwenye
    udikteta wa kijeshi,
  • 0:59 - 1:03
    kwa sasa, hii ilikuwa ni namna
    pekee ya kujipatia kipato.
  • 1:05 - 1:09
    Mara nyingi usiku, aliniambia,
    alilala kwenye guta yake
  • 1:09 - 1:13
    ili kusudi apate wateja wa kwanza
    wa treni ya usiku.
  • 1:16 - 1:19
    Punde si punde, tukagundua kwamba
    kwa namna fulani
  • 1:19 - 1:21
    tuna mengi ya kufanana --
  • 1:21 - 1:23
    wote tulikuwa kwenye miaka ya 20,
  • 1:23 - 1:26
    sote tulikuwa tunavutiwa na
    tamaduni za kigeni --
  • 1:27 - 1:29
    mpaka akanikaribisha nyumbani.
  • 1:30 - 1:34
    Tukatoka kwenye mtaa wenye watu wengi,
  • 1:34 - 1:38
    na tukaanza kupita kwenye njia zenye
    mabonde na kona nyingi
  • 1:38 - 1:40
    Kulikuwa na nyumba zilizo bomoka
    kila sehemu.
  • 1:40 - 1:43
    Kwakweli sikujua nilipokuwepo,
  • 1:44 - 1:48
    na nikagundua kua chochote
    kinaweza kunitokea sasa.
  • 1:48 - 1:50
    Ninaweza ibiwa au leweshwa
  • 1:50 - 1:52
    au kibaya zaidi.
  • 1:52 - 1:53
    Hamna ambaye angejua.
  • 1:54 - 1:58
    Mwishowe, akasimama na akanipeleka
    kwenye kibanda,
  • 1:58 - 2:01
    ambacho kilikuwa na chumba kimoja
    tu kidogo.
  • 2:02 - 2:04
    Kisha akainama chini,
  • 2:04 - 2:06
    kwenye kitanda chake.
  • 2:08 - 2:10
    Kitu ndani yangu kikaganda.
  • 2:12 - 2:15
    Nikawa nasubiri nione atavuta nini.
  • 2:15 - 2:18
    Mwishowe akatoa boksi.
  • 2:19 - 2:24
    Ndani yake kulikuwa na barua zote
    alizowahi kupokea
  • 2:24 - 2:26
    kutoka kwa wageni wa nchi za nje,
  • 2:27 - 2:29
    na baadhi zao alikuwa amebandika
  • 2:29 - 2:33
    picha ndogo zisizo na rangi zilizochoka
  • 2:33 - 2:35
    za marafiki zake wapya wa kigeni.
  • 2:36 - 2:40
    Hivyo tulivyoagana usiku ule,
  • 2:40 - 2:43
    nikagundua kua amenionyesha pia
  • 2:43 - 2:45
    siri ya kwenye kusafiri,
  • 2:45 - 2:47
    ambayo ni kufanya kitu bila uwoga,
  • 2:47 - 2:50
    kusafiri ndani vile vile na nje,
  • 2:50 - 2:52
    kwenda sehemu ambazo usingeenda
    vinginevyo,
  • 2:53 - 2:55
    kufanya usiyoyafahamu,
  • 2:56 - 2:57
    usichokielewa,
  • 2:57 - 2:59
    hata uwoga.
  • 3:00 - 3:03
    Nyumbani, ni hatari kirahisi
  • 3:03 - 3:05
    kujiona tupo juu ya mambo.
  • 3:06 - 3:10
    Nje kwenye dunia, unakumbushwa
    kila saa kwamba haupo
  • 3:10 - 3:13
    na hauwezi kufikia kwenye
    mwisho wa mambo pia.
  • 3:14 - 3:17
    Kila sehemu, "Watu wanatamani kutulia,"
  • 3:17 - 3:19
    Ralph Waldo Emerson alitukumbusha,
  • 3:19 - 3:22
    "lakini mara nyingi tunapokuwa
    hatujatulia
  • 3:22 - 3:24
    ndipo kuna tumaini kwetu."
  • 3:25 - 3:27
    Kwenye hili kongamano,
    tumebahatika sana
  • 3:27 - 3:31
    kusikia mawazo mapya ya
    kustaajabisha na vumbuzi
  • 3:31 - 3:33
    na kweli, kuhusu njia zote
  • 3:33 - 3:36
    ambazo maarife yanasukumwa
    mbele sana.
  • 3:37 - 3:40
    Lakini kuna hatua, maarifa yanaondoka.
  • 3:41 - 3:42
    Na huo ndio muda
  • 3:42 - 3:45
    ambao maisha yako yanaamua kweli:
  • 3:46 - 3:48
    unapata upendo;
  • 3:48 - 3:50
    unapoteza rafiki;
  • 3:51 - 3:52
    taa zinazimika.
  • 3:53 - 3:58
    Na ni hapo, ambapo ukiwa umepotea,
    au huelewi au umepoteza matumaini,
  • 3:58 - 4:00
    ndipo unapogundua wewe ni nani.
  • 4:02 - 4:06
    Siamini kama ujinga ni starehe.
  • 4:06 - 4:09
    Sayansi imefanya maisha yetu
  • 4:09 - 4:12
    yang'ae zaidi, marefu zaidi na yenye
    afya zaidi.
  • 4:13 - 4:18
    Na ninawashukuru sana walimu
    walionifundisha kanuni za fizikia,
  • 4:18 - 4:21
    na kunielekeza kwamba
    tatu mara tatu ni tisa.
  • 4:22 - 4:25
    Naweza kuhesabu hiyo kwa vidole vyangu.
  • 4:25 - 4:27
    muda wowote wa usiku au mchana.
  • 4:29 - 4:30
    Lakini mwanahisabati akiniambia
  • 4:30 - 4:34
    hio ukitoa mara tatu
    ukitoa tatu ni tisa,
  • 4:34 - 4:39
    hiyo ni aina ya mantiki inayoonekana
    kama uaminifu.
  • 4:41 - 4:44
    Tofauti ya maarifa, kwa maneno mengine,
    sio lazima iwe ujinga.
  • 4:45 - 4:46
    Inaweza ikawa mshangao.
  • 4:46 - 4:48
    Au maajabu.
  • 4:48 - 4:49
    Uwezekano.
  • 4:50 - 4:54
    Na kwenye maisha yangu, nimegundua
    ni vile nisivyovijua
  • 4:54 - 4:56
    ndivyo ambavyo vimeninyanyua
    na kunisukuma mbele zaidi
  • 4:56 - 4:59
    kushinda vile ninavyovijua.
  • 5:00 - 5:02
    Ni pia vile nisivyovijua
  • 5:02 - 5:05
    vilivyonileta karibu na kila mtu
    anaenizunguka.
  • 5:07 - 5:09
    Kwa Novemba nane mfululizo, hivi karibuni,
  • 5:09 - 5:13
    nimesafiri kila mwaka kupitia
    Japan na Dalai Lama.
  • 5:14 - 5:17
    Na kitu ambacho alikuwa anasema kila siku
  • 5:17 - 5:21
    ambacho kilionekana kuwapa watu
    suluhisho na tumaini
  • 5:21 - 5:23
    ilikuwa ni "sijui."
  • 5:24 - 5:26
    "Nini kitatokea Tibet?"
  • 5:27 - 5:30
    "Lini tutapata amani duniani?"
  • 5:31 - 5:33
    "Ipi ni njia sahihi ya kulea watoto?"
  • 5:34 - 5:37
    "Kiukweli," anasema huyu mtu mwenye
    busara,
  • 5:37 - 5:38
    "Sijui."
  • 5:40 - 5:44
    Mshindi wa tuzo ya Nobeli,
    mwanauchumi Daniel Kahneman
  • 5:44 - 5:48
    ametumia zaidi ya miaka 60 sasa
    akichunguza tabia za binadamu,
  • 5:48 - 5:50
    na muafaka wake ni
  • 5:50 - 5:55
    kua huwa tunajiamini sana na kile
    tunachodhani tunakijua
  • 5:55 - 5:57
    kuliko tunavyotakiwa kuwa.
  • 5:57 - 5:59
    Tunakuwa, kama anavyosema,
  • 5:59 - 6:04
    na "uwezo usio na kikomo wa
    kupuuzia ujinga wetu."
  • 6:05 - 6:10
    Tunajua -- nanukuu -- timu yetu
    itaenda kushinda wikiendi hii,
  • 6:10 - 6:12
    na tunakumbuka tu hayo maarifa
  • 6:12 - 6:15
    mara chache tukiwa sahihi.
  • 6:16 - 6:18
    Mara nyingi, tunakuwa gizani.
  • 6:19 - 6:23
    Na hapo ndipo hisia za kweli zipo.
  • 6:25 - 6:28
    Unajua mpenzi wako
    atakachokua anafanya kesho?
  • 6:29 - 6:30
    Je unataka kujua?
  • 6:32 - 6:34
    Wazazi wetu sote
    kama watu wanavyowaita,
  • 6:34 - 6:36
    Adam na Hawa,
  • 6:36 - 6:40
    wasigeweza kufa, alimradi waliendelea kula
    kutoka kwenye mti wa uzima.
  • 6:41 - 6:43
    Ila punde walivyoanza kula
  • 6:43 - 6:45
    kutoka kwenye mti wa maarifa,
    ya mema na mabaya,
  • 6:45 - 6:47
    wakaanguka kutoka kwenye weupe wao.
  • 6:48 - 6:51
    Wakajawa na aibu na uwoga,
  • 6:51 - 6:52
    wakajitambua.
  • 6:53 - 6:55
    Na wakajifunza,
    kwa kuchelewa, pengine,
  • 6:55 - 6:58
    kwamba kwa kweli kuna vitu
    tunahitaji kuvijua,
  • 6:58 - 7:02
    lakini kuna vingi, vingi zaidi
    ambavyo ni bora visichunguzwe.
  • 7:04 - 7:06
    Sasa, nilivyokuwa mtoto,
  • 7:06 - 7:09
    nilijua vyote, bila shaka.
  • 7:09 - 7:14
    Nilitumia miaka 20 darasani
    nikikusanya mawazo,
  • 7:14 - 7:16
    na nilikuwa kweli
    kwenye biashara ya habari,
  • 7:16 - 7:18
    nikiandika makala ya gazeti la Time.
  • 7:19 - 7:24
    Nikasafiri kwenda Japan kwa mara ya kwanza
    kwa muda wa wiki mbili na nusu,
  • 7:24 - 7:28
    na nikarudi na insha ya karatasi 40
  • 7:28 - 7:31
    ikielezea kila kitu kuhusu
    nyumba za ibada za Japan,
  • 7:31 - 7:34
    mitindo yake, michezo yake ya besiboli,
  • 7:34 - 7:36
    nafsi yake.
  • 7:37 - 7:40
    Lakini chini ya hayo yote,
  • 7:40 - 7:43
    kitu ambacho sikuweza elewa
  • 7:43 - 7:47
    kiliniongoza kwa sababu
    nisizoweza kuwaelezea bado,
  • 7:48 - 7:51
    mpaka nikaamua kwenda kuishi Japan.
  • 7:52 - 7:55
    Na sasa ambapo nimekuwa kule kwa miaka 28,
  • 7:55 - 7:58
    siwezi kuwaelezea mengi kabisa
  • 7:58 - 7:59
    kuhusu nyumbani kwangu.
  • 8:00 - 8:02
    Ambayo ni nzuri,
  • 8:02 - 8:04
    sababu inamaanisha kila siku
    ninagundua kitu kipya.
  • 8:04 - 8:06
    na kwenye hiyo harakati,
  • 8:06 - 8:10
    kuangalia pembeni na kuona
    mamia na maelfu ya vitu
  • 8:10 - 8:11
    nisingeweza kujua.
  • 8:13 - 8:15
    Maarifa ni zawadi kubwa sana.
  • 8:16 - 8:21
    Lakini maarifa ya uwongo
    yanaweza kua hatari kuliko ujinga.
  • 8:22 - 8:25
    Kuwaza kwamba unamjua mpenzi wako
  • 8:25 - 8:26
    au adui yako
  • 8:27 - 8:28
    inaweza kua ya hila zaidi
  • 8:28 - 8:31
    kuliko kukubali kwamba hautowajua.
  • 8:32 - 8:36
    Kila asubuhi Japan, ua likiwaka kwenye
    nyumba yetu ndogo,
  • 8:36 - 8:41
    inanichukua maumivu mengi
    kutokuangalia utabiri wa hali ya hewa,
  • 8:41 - 8:42
    sababu nikiangalia,
  • 8:42 - 8:46
    akili yangu itajawa na mawazo,
    na itasumbuka
  • 8:46 - 8:48
    hata kama siku ikiwa angavu.
  • 8:50 - 8:54
    Nimekuwa mwandishi kwa miaka 34 sasa.
  • 8:55 - 8:58
    Na kitu kimoja ambacho nimejifunza
  • 8:58 - 9:01
    ni kua mabadiliko huja pale
    nisipoyapangilia,
  • 9:01 - 9:03
    pale ambapo sijui nini kinafuata,
  • 9:03 - 9:08
    pale ambapo siwezi kuwaza kua ni mkubwa
    kuliko kila kitu kinachonizunguka.
  • 9:09 - 9:11
    Na hio ni kweli pia kwenye upendo
  • 9:12 - 9:14
    au kwenye wakati wa majanga.
  • 9:15 - 9:18
    Ghafla, tumerudi kwenye ile guta tena
  • 9:18 - 9:22
    na tunaruka mitaa mikubwa yenye taa;
  • 9:22 - 9:26
    na tunakumbushwa, kweli,
    kwenye kanuni ya kwanza ya safari
  • 9:26 - 9:28
    na hivyo, ya maisha:
  • 9:29 - 9:34
    una nguvu tu kama uwezo
    wako wa kujisalimisha.
  • 9:36 - 9:38
    Mwishowe, pengine,
  • 9:38 - 9:39
    kuwa binadamu
  • 9:39 - 9:41
    ni muhimu zaidi
  • 9:41 - 9:44
    kuliko kuwa kwenye kujua kikamilifu.
  • 9:45 - 9:46
    Asanteni.
  • 9:46 - 9:53
    (Makofi)
Title:
Uzuri wa ambavyo hatutovijua
Speaker:
Pico Iyer
Description:

Takribani miaka 30 iliyopita,Pico Iyer alisafiri kwenda Japan, akaipenda nchi na akahamia huko. Mfwatiliaji wa karibu wa roho ya binadamu, Iyer anasema kwamba sasa anaona anajua machache kuhusiana na Japan -- au, hakika, kuhusu chochote kile -- kama ambavyo alidhani anajua miongo mitatu iliyopita. Kwenye hii tafakari ya kishairi kuhusu hekima, Iyer anaelezea kuhusu uelewa unavyokuja na umri: kadri tunavyodhani tunajua, ndivyo tunagundua tunajua kidogo.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
10:05

Swahili subtitles

Revisions