Jinsi gani Afrika itaendelea kukua
-
0:00 - 0:04Simulizi za Afrika inayokua
zinapata changamoto -
0:04 - 0:09Karibia miaka 10 iliyopita
Niliongea kuhusu Afrika, -
0:09 - 0:12Afrika yenye matumaini na fursa,
-
0:12 - 0:13Afrika ya wajasiriamali,
-
0:14 - 0:17Afrika tofauti kabisa na Afrika
ambayo umezoaea kusikia -
0:17 - 0:20ya vifo, umaskini na magonjwa.
-
0:20 - 0:22Na kile nilichokiongelea,
-
0:22 - 0:27ikawa sehemu ya kile kinachojulikana sasa
kama hadithi ya Afrika inayokua. -
0:27 - 0:31Nataka niwaambie hadithi mbili
kuhusu hii Afrika inayokua. -
0:31 - 0:32Ya kwanza inaihusisha Rwanda,
-
0:33 - 0:36nchi ambayo imepitia majaribu mengi
na dhiki. -
0:36 - 0:40Na Rwanda ikaamua kuwa kitovu
cha teknolojia, au kitovu cha teknolojia -
0:40 - 0:42kwenye bara la Afrika.
-
0:42 - 0:45Ni nchi yenye milima na ardhi ya eneo
lenye vilima, -
0:45 - 0:46kidogo kama hapa,
-
0:46 - 0:49hivyo ni vigumu sana
kupeleka huduma kwa watu. -
0:49 - 0:51Hivyo Rwanda imesema nini?
-
0:51 - 0:55Ili kuweza kuokoa maisha,
itajaribu kutumia ndege zisizo na rubani -
0:55 - 0:58kupeleka madawa ya kuokoa maisha,
chanjo na damu -
0:58 - 1:00kwa watu katika sehemu zisizo fikika
-
1:00 - 1:02wakishirikiana na
kampuni inayoitwa Zipline, -
1:03 - 1:07pamoja na UPS, na pia Gavi
shirika la kimataifa la chanjo. -
1:07 - 1:09Katika kufanya hivi, itaokoa maisha.
-
1:09 - 1:15Hii ni sehemu ya ubunifu
tunayotaka kuona katika Afrika inayokua. -
1:15 - 1:17Hadithi ya pili inahusiana na jambo
-
1:17 - 1:20ambalo ninauhakika wengi wenu
mmeona au mtakumbuka. -
1:20 - 1:24Mara nyingi, nchi za Afrika
zimeteseka na ukame na mafuriko, -
1:24 - 1:28na inaongezeka zaidi kwasababu
ya athari za mabadiliko ya tabia nchi. -
1:28 - 1:34Wakati haya yanapotokea, kawaida
husubiri nchi za kimataifa kuchanga fedha. -
1:34 - 1:37Unaona picha za watoto
wakiwa na nzi kwenye nyuso zao -
1:37 - 1:40mizoga ya wanyama waliokufa na kadhalika.
-
1:40 - 1:43Sasa nchi hizi,
nchi 32, zilikutana pamoja -
1:43 - 1:45chini ya mwamvuli wa Umoja wa Afrika
-
1:45 - 1:50na kuamua kuunda shirika
linaloitwa Africa Risk Capacity. -
1:50 - 1:51Linafanya nini?
-
1:51 - 1:54Ni wakala wa bima wa hali ya hewa
-
1:54 - 1:58na nchi hizi zinachofanya
ni kulipa bima kila mwaka, -
1:58 - 2:01karibia dola milioni 3 kwa mwaka
kutoka kwenye rasilimali zao, -
2:01 - 2:06ili kwamba endapo wanakumbwa
na hali ya ukame mgumu au mafuriko, -
2:06 - 2:08fedha hizi zitalipwa kuwasaidia
-
2:08 - 2:11ambazo wanaweza kuzitumia
kuwatunza wananchi wao -
2:11 - 2:14badala ya kusubiri msaada kuja.
-
2:14 - 2:18Shirika la African Risk Capacity
mwaka jana lilipa dola milioni 26 -
2:18 - 2:21kwa Mauritania, Senegal na Niger.
-
2:21 - 2:26Hii iliwawezesha kuwatunza
watu milioni 1.3 walioathirika na ukame. -
2:26 - 2:29Waliweza kurudisha tena maisha yao,
-
2:29 - 2:31kununua majani ya n'gombe
kulisha watoto mashuleni -
2:31 - 2:37kuwafanya wananchi wabaki nyumbani
badala ya kuhama nje ya eneo. -
2:37 - 2:39Hivyo hizi ni aina za hadithi
-
2:39 - 2:43za Afrika iliyotayari
kuchukua majikumu yake yenyewe, -
2:43 - 2:46na kutafuta suluhisho
kwa matatizo yake yenyewe. -
2:46 - 2:48Ila simulizi hizo zinapata changamoto sasa
-
2:48 - 2:53kwasababu bara letu halijafanya vema
kwa miaka miwili iliyopita. -
2:53 - 2:56Ilikuwa inakua kwa kiwango
cha asilimia 5 kwa mwaka -
2:56 - 2:58kwa muongo mmoja na nusu uliopita
-
2:58 - 3:01lakini utabiri wa mwaka huu
ulikuwa asilimia tatu. Kwanini? -
3:01 - 3:05kwa mazingira ya ulimwengu yanavyobadilika
bei za bidhaa zimeshuka. -
3:05 - 3:08Uchumi wa nchi nyingi
bado unaendeshwa na bidhaa, -
3:08 - 3:11na hivyo utendaji wake
umeteleza -
3:11 - 3:15Na sasa suala la kujitoa kwa Uingereza
haifanyi iwe rahisi -
3:15 - 3:19Sikujua kama Uingereza ingejitoa
-
3:19 - 3:23na hilo lingekuwa moja ya vitu ambavyo
vingeleta kutokuwa na uhakika ulimwenguni -
3:23 - 3:25kama tulivyo.
-
3:25 - 3:27Hivyo sasa tuna hii hali
-
3:27 - 3:30na ninafikiri ni wakati wakuangalia
-
3:30 - 3:35na kusema ni vitu gani ambavyo
nchi za Afrika zilifanya sahihi? -
3:35 - 3:36Kipi walikosea?
-
3:37 - 3:39Tutajengaje kwenye haya yote
na kujifunza -
3:39 - 3:42ili kwamba tuendeleze Afrika inayokua?
-
3:43 - 3:46Hivyo ngoja niongelee kuhusu mambo sita
ninayofikiri tulifanya sahihi. -
3:47 - 3:50La kwanza ni kusimamia
uchumi wa nchi zetu vizuri -
3:50 - 3:54Miaka ya 80 na 90 ni miongo iliyopotea,
wakati Afrika haikuwa ikifanya vizuri, -
3:54 - 3:58na baadhi yenu mtakumbuka ukurasa
wa mbele wa gazeti la "Economist" -
3:58 - 4:00lililosema, "Bara lililopotea"
-
4:00 - 4:04Ila miaka ya 2000 watunga sera walijifunza
-
4:04 - 4:08kwamba wanahitaji kusimamia
mazingira ya uchumi vizuri zaidi, -
4:08 - 4:10kuhakikisha uthabiti,
-
4:10 - 4:13kushusha mfumuko wa bei kufika
tarakimu moja, -
4:13 - 4:18kushusha nakisi ya bajeti, chini ya
asilimia tatu ya Pato la Taifa, -
4:18 - 4:22wape wawekezaji, wote wa ndani na wageni,
-
4:22 - 4:26aina ya uthabiti ili wawe na imani ya
kuwekeza kwenye chumi hizi. -
4:26 - 4:27Hivyo hiyo ilikuwa namba moja.
-
4:27 - 4:29Mbili, deni.
-
4:29 - 4:35Mwaka 1994, urari wa deni la Pato la taifa
wa nchi za Kiafrila ulikuwa asilimia 130, -
4:35 - 4:37na hawakuwa na nafasi ya fedha nakisi
-
4:37 - 4:40Hawakuweza kutumia rasilimali zao
kuwekeza kwenye maendeleo yao -
4:40 - 4:41kwakuwa walikuwa wanalipa deni
-
4:41 - 4:46kwaweza kuwa na baadhi yenu humu ndani
mliofanyakazi kusaidia nchi za Afrika -
4:46 - 4:47kupata unafuu wa madeni.
-
4:47 - 4:52Hivyo wadai binafsi, wa pande mbalimbali
na pande mbili waliunganika -
4:52 - 4:56na kuamua kuanzisha mpango wa
Nchi Fukara zenye Mzigo wa madeni -
4:56 - 4:57na kutoa unafuu wa madeni.
-
4:57 - 4:59Hivyo unafuu huu wa madeni mwaka 2005
-
4:59 - 5:03ulifanya urari wa deni kwa Pato la taifa
kushuka hadi takriban asilimia 30, -
5:03 - 5:07na kulikuwa na rasilimali za kutosha
kujaribu na kuwekeza upya. -
5:07 - 5:09Kitu cha tatu kilikuwa
makampuni yaliyopata hasara -
5:09 - 5:11Serikali zilishiriki katika biashara
-
5:11 - 5:14ambazo hawakupaswa kuzifanya.
-
5:14 - 5:17Na walikuwa wanaendesha biashara,
walikuwa wanapata hasara. -
5:17 - 5:20Hivyo baadhi ya makampuni haya
yaliundwa upya, -
5:20 - 5:22kuwa kibiashara,kubinafsishwa au kufungwa,
-
5:22 - 5:25na kupunguza mzigo mkubwa
kwa serikali. -
5:26 - 5:28Kitu cha nne kilikuwa
kitu cha kuvutia sana -
5:29 - 5:31Mapinduzi ya makampuni ya simu yakaja,
-
5:32 - 5:34na nchi za Kiafrika zikarukia.
-
5:34 - 5:37Mwaka 2000, laini za simu zilikuwa
milioni 11 -
5:37 - 5:42Leo, tuna takriban laini milioni 687
za simu za mkononi barani. -
5:42 - 5:44Na hi imetuwezesha
-
5:44 - 5:47kwenda na kusonga mbele
na teknolojia ya simu za mkononi -
5:47 - 5:49ambapo Afrika hakika inaongoza.
-
5:49 - 5:52Nchini Kenya, maendeleo ya kutuma
fedha kwa simu -
5:52 - 5:55M-Pesa, ambayo nyote
mmesikia habari zake-- -
5:55 - 5:58ilichukua muda kwa dunia
kuona kwamba Afrika ipo mbele -
5:58 - 6:00katika hii teknolojia.
-
6:00 - 6:03na hii kutuma pesa kwa simu za mkononi
pia inatoa jukwaa -
6:03 - 6:05kwa upatikanaji wa nishati mbadala
-
6:05 - 6:09Unajua, watu wanaoweza sasa kulipia sola
-
6:09 - 6:13kwa njia wanayotumia kulipia
kwa kadi kwenye simu zao. -
6:13 - 6:18Hivyo haya yalikuwa maendeleo mazuri sana
kitu ambacho kilikwenda sahihi. -
6:18 - 6:23Tuliwekeza zaidi kwenye elimu
na afya, isivyo vyakutosha, -
6:23 - 6:24lakini kulikuwa na maboresho.
-
6:24 - 6:30Watoto milioni 25 walipata chanjo
katika muogo mmoja nanusu uliopita. -
6:31 - 6:34Kitu kingine ilikuwa
kwamba migogoro ilipungua. -
6:34 - 6:36Kulikuwa na migogoro mingi
barani. -
6:36 - 6:37Wengi wenu mnafahamu hilo.
-
6:37 - 6:42Lakini ilipungua, na viongozi wetu
waliweza hata kufifiza mapinduzi. -
6:42 - 6:46Aina mpya ya migogoro imeibuka,
na nitaielezea hiyo baadaye. -
6:46 - 6:50Hivyo kutokana na yote haya, pia
kuna baadhi ya utofautishaji barani -
6:50 - 6:51ambao nataka muufahamu,
-
6:52 - 6:54kwasababu pamoja na kuwa
-
6:54 - 6:58kuna baadhi ya nchi--
Cote d'Ivoire, Kenya, Ethiopia -
6:58 - 7:01Tanzania na Senegal
zinafanya vizuri kwa sasa -
7:03 - 7:05Lakini tulikosea wapi?
-
7:05 - 7:07Ngoja nitaje mambo nane.
-
7:07 - 7:09Unapaswa kuwa umekosea zaidi
kuliko kupatia. -
7:09 - 7:10(Kicheko)
-
7:10 - 7:13Hivyo kuna mambo nane tulikosea.
-
7:13 - 7:16La kwanza ilikuwa pamoja na kukua
hatukutengeneza ajira za kutosha. -
7:17 - 7:19Hatukutengeneza ajira kwa vijana wetu.
-
7:19 - 7:22Ukosefu wa ajira kwa vijana barani
ni karibia asilimia 15, -
7:22 - 7:25na upungufu wa ajira ni tatizo kubwa.
-
7:25 - 7:31Jambo la pili tulichofanya ni kuwa kiwango
cha ukuaji hakikuwa kizuri vyakutosha -
7:31 - 7:34Hata ajira zilizoundwa
zilikuwa ni ajira zenye tija ndogo sana, -
7:35 - 7:38hivyo tulihamisha watu
kutoka kilimo duni kisicho na tija -
7:38 - 7:42kwenda biashara zisizo na tija
na kufanyia kazi sekta isiyo rasmi -
7:42 - 7:44katika maeneo ya mijini.
-
7:44 - 7:48Jambo la tatu ni kwamba
kukosekana kwa usawa kuliongezeka. -
7:49 - 7:54Hivyo tuliunda mabilionea zaidi.
-
7:54 - 7:56mabilionea 50 wenye thamani ya dola
bilioni 96 -
7:56 - 8:01wanamiliki utajiri zaidi kuliko watu
milioni 75 wa chini barani. -
8:02 - 8:03Umaskini,
-
8:04 - 8:08uwiano wa watu katika umaskini--
hilo ni jambo la nne--ulipungua -
8:08 - 8:12lakini namba halisi hazikupungua
kwasababu ya ongezeko la idadi ya watu. -
8:12 - 8:15Na ongezeko la idadi ya watu ni jambo
-
8:15 - 8:18ambalo hatujafanyia
mazungumzo ya kutosha barani. -
8:18 - 8:21Na ninafikiri tutahitaji
kulielewa na kulifanyia kazi -
8:21 - 8:24haswa jinsi ya kuelimisha wasichana.
-
8:25 - 8:29Hiyo ndio njia haswa kufanyia kazi
hasusan kwenye suala hili. -
8:30 - 8:37Jambo la tano ni kwamba hatukuwekeza
vya kutosha kwenye miundombinu. -
8:37 - 8:39Tulikuwa na uwekezaji kutoka kwa Wachina.
-
8:39 - 8:42Ambao ulisaidia baadhi ya nchi,
lakini haitoshi. -
8:42 - 8:45Utumiaji wa umeme
barani Afrika -
8:45 - 8:49Kusini mwa jangwa la Sahara Afrika
ni sawasawa na Hispania. -
8:49 - 8:52Utumiaji kwa ujumla
ni sawasawa na ule wa Hispania -
8:53 - 8:55Hivyo watu wengi wanaishi gizani,
-
8:55 - 8:59na kama Rais wa Benki ya Maendeleo
Afrika alivyosema hivi karibuni, -
8:59 - 9:01Afrika haiwezi kuendelea gizani.
-
9:02 - 9:04Kitu kingine ambacho hatujafanya
-
9:04 - 9:10ni kwamba chumi zetu
zimeshikilia muundo uliofanana -
9:10 - 9:11ambao tumekuwa nao kwa miongo.
-
9:11 - 9:13Hivyo pamoja na kwamba tumekua
-
9:13 - 9:16muundo wa chumi zetu
haujabadilika kwa kiasi kikubwa. -
9:16 - 9:18Bado tunauza bidhaa nchi za nje
-
9:18 - 9:22na kuuza bidhaa nchi za nje ni nini?
kuuza ajira nchi za nje. -
9:22 - 9:26Ongezeko la thamani ya uzalishaji wetu
ni asilimia 11 tu -
9:26 - 9:30Hatuundi ajira za kutosha kwenye
uzalishaji kwa vijana wetu, -
9:30 - 9:33na biashara kati yetu ni kidogo.
-
9:33 - 9:36Takriban asilimi 12 tu ya biashara
kati yetu sisi wenyewe -
9:36 - 9:39Hivyo hilo ni tatizo lingine zito sana.
-
9:39 - 9:41Kisha utawala bora.
-
9:41 - 9:44Utawala bora ni suala zito.
-
9:44 - 9:46Tuna taasisi dhaifu,
-
9:46 - 9:51na wakati mwingine taasisi hewa,
ninafikiri hii inaleta mwanya wa rushwa. -
9:51 - 9:56Rushwa ni suala ambalo bado
hatujalimudu kiasi cha kutosha, -
9:56 - 9:59na tunatakuwa kupambana kufa na kupona,
-
9:59 - 10:02hiyo na ongezeko la uwazi katika
jinsi tunavyosimamia chumi zetu -
10:02 - 10:05na jinsi tunavyosimamia fedha zetu.
-
10:05 - 10:10Tunahitaji pia kujihadhari na migogoro
mipya, -
10:10 - 10:11aina mpya ya migogoro,
-
10:12 - 10:15kama tuliyonayo na Boko Haram
katika nchi yangu, Nigeria, -
10:15 - 10:17Na Al-Shabaab nchini Kenya.
-
10:17 - 10:20Tunahitaji kushirikiana na
washiriki wa kimataifa, -
10:20 - 10:23nchi zilizoendelea,
kupambana juu ya hili pamoja. -
10:23 - 10:25Ama sivyo, tunaunda ukweli mpya
-
10:25 - 10:28ambao sio aina tunayotaka
kwa Afrika inayokua. -
10:28 - 10:32Na mwisho, ni suala la elimu.
-
10:32 - 10:35Mifumo yetu ya elimu
katika nchi nyingi imevunjika. -
10:35 - 10:40Hatuundi aina ya stadi
zinazohitajika kwa siku za usoni -
10:40 - 10:42Hivyo tunatakiwa tutafute njia
ya kutoa elimu kwa ubora. -
10:43 - 10:46Hivyo hayo ni mambo ambayo
hatufanyi kwa usahihi. -
10:46 - 10:49Sasa, tunaenda wapi kutokea hapo?
-
10:49 - 10:54Ninaamini njia ya kusongambele
ni kujifunza kusimamia mafanikio. -
10:54 - 10:58Mara nyingi, watu wanapofanikiwa
au nchi zinapofanikiwa -
10:58 - 11:00husahau kullichowafanya wafanikiwe.
-
11:01 - 11:03Kujifunza kile unachoweza kufanikiwa,
-
11:03 - 11:06kukisimamia na kukitunza
ni jambo muhimu kwetu. -
11:06 - 11:08Hivyo vitu vyote nilivyosema
tulifanya sahihi, -
11:08 - 11:12tunatakiwa kujifunza kuvifanya kwa usahihi
tena, na kuviendeleza. -
11:12 - 11:15Kusimamia uchumi wakati
unaunda ustawi ni muhimu, -
11:15 - 11:19kupata bei sahihi
na sera thabiti. -
11:19 - 11:21Mara nyingi hatuna uthabiti
-
11:21 - 11:24Mfumo wa utawala mmoja ukitoka
unaingia mwingine -
11:24 - 11:27na wanatupa mbali hata sera zilizokuwa
zinafanyakazi vizuri awali -
11:27 - 11:28Hii inafanya nini?
-
11:28 - 11:31Inaleta sintofahamu kwa watu,
kaya -
11:31 - 11:32sintofahamu kwa biashara
-
11:32 - 11:35Hawajui jinsi na wakati wa kuwekeza.
-
11:35 - 11:39Deni: tunatakiwa tusimamie' mafanikio
tuliyopata katika kupunguza deni letu, -
11:39 - 11:42lakini sasa nchi zimerudia
katika kukopa tena, -
11:42 - 11:45na tumeona urari wa deni kwa Pato la taifa
unaanza kupanda tena, -
11:45 - 11:47na katika baadhi ya nchi,
-
11:47 - 11:49deni linakuwa ni tatizo,
hivyo tunatakiwa tuliepuke. -
11:49 - 11:51Hivyo usimamizi wa mafanikio
-
11:51 - 11:53Kinachofuata
ni kuwa makini sana -
11:53 - 11:55na yale mambo ambayo
hatukufanya vizuri. -
11:55 - 11:57Kitu cha kwanza kabisa ni miundombinu
-
11:57 - 12:01Ndio, nchi nyingi sasa zinatambua
zinahitaji kuwekeza kwenye hili, -
12:01 - 12:03na zinajaribu kufanya
kadiri ziwezavyo kufanya hivyo. -
12:03 - 12:05Lazima.
-
12:05 - 12:06Kitu muhimu sana ni umeme.
-
12:06 - 12:09Huwezi kuendelea katika giza.
-
12:09 - 12:11Na kisha utawala bora na rushwa:
-
12:11 - 12:12tunatakiwa tupambane.
-
12:12 - 12:15Tunatakiwa kuendesha nchi zetu kwa uwazi.
-
12:15 - 12:19Pamoja na yote hayo, lazima
tuwashirikishe vijana. -
12:19 - 12:21Tuna ubunifu katika vijana wetu
-
12:21 - 12:22Ninauona kila siku.
-
12:22 - 12:26Ndio kinachoniamsha asubuhi
na kujisikia tayari kwenda. -
12:26 - 12:28Tunatakiwa tusibanie ubunifu
katika vijana wetu, -
12:28 - 12:31tusiwazibie njia,
tuwaunge mkono kuunda na ugunduzi -
12:31 - 12:33na kuongoza njia.
-
12:33 - 12:35Na ninajua kwamba watatuongoza
katika mwelekeo sahihi. -
12:35 - 12:37Na wanawake wetu, na wasichana wetu:
-
12:37 - 12:41tunatakiwa tutambue kwamba
wanawake na wasichana ni zawadi. -
12:41 - 12:42Wana nguvu,
-
12:42 - 12:44na tunatakiwa tusiwabanie hiyo nguvu
-
12:44 - 12:47ili waweze kutoa mchango
wao barani. -
12:47 - 12:51Nina amini kwa nguvu
kwamba tukifanya hayo yote, -
12:51 - 12:54tutakuta kwamba simulizi za Afrika
inayokua -
12:54 - 12:56sio ubabaishaji.
-
12:56 - 12:57ni harakati.
-
12:58 - 13:02Ni harakati, na tukiendelea,
tusipowabania vijana wetu, -
13:02 - 13:03tusipowabania wanawake wetu,
-
13:03 - 13:05wakati mwingine tunaweza kurudi nyuma,
-
13:05 - 13:07tunaweza pia kukaa pembezoni,
-
13:07 - 13:08lakini harakati ziko wazi.
-
13:09 - 13:11Afrika itaendelea kukua.
-
13:11 - 13:14Na ninawaambia wafanyabiashara
mliopo kwenye hadhira hii, -
13:14 - 13:18uwekezaji Afrika sio kwa ajili ya leo,
sio kwa ajili ya kesho, -
13:18 - 13:21sio kitu cha muda mfupi,
ni kitu cha muda mrefu. -
13:21 - 13:23Lakini ikiwa hamtawekeza Afrika,
-
13:24 - 13:25basi mtakuwa mnakosa
-
13:25 - 13:29mojawapo ya fursa zinazoibuka
duniani. -
13:29 - 13:30Asante.
-
13:30 - 13:33(Makofi)
-
13:39 - 13:42Kelly Stoetzel: Umegusia rushwa
katika mazungumzo yako -
13:42 - 13:45na unafahamika vizuri
kuwa mpambanaji thabiti wa rushwa. -
13:45 - 13:48Lakini hiyo ilikuwa na matokeo yake.
-
13:48 - 13:51Watu walijibu mashambulizi,
na mama yako alitekwa nyara. -
13:51 - 13:53Umewezaje kulimudu hili?
-
13:53 - 13:55Ngozi Okonjo-Iweala:
Imekuwa ngumu sana. -
13:55 - 14:00Asante kwa kugusia
suala la kutekwa nyara mama yangu -
14:00 - 14:02Ni mada ngumu sana.
-
14:02 - 14:06Lakini inachomaanisha
ni kwamba unapopambana na rushwa, -
14:06 - 14:10unapogusa mifuko ya watu
wanaoiba pesa, -
14:10 - 14:12hawanyamazi kimya tu.
-
14:12 - 14:15Watajibu mashambulizi, na suala kubwa
ni wanapojaribu kutumia vitisho -
14:15 - 14:19unakata tamaa, au unaendeleza mapambano?
-
14:19 - 14:22Unatafuta njia ya kubakia
na kujibu mashambulizi? -
14:22 - 14:26Na jibu nililokuwa nalo
nikiwa na timu zilizofanya nazo kazi -
14:26 - 14:28ni kuendeleza mapambano
-
14:28 - 14:30Tunatakiwa kuunda hizo taasisi.
-
14:30 - 14:33Tunatakiwa kutafuta njia ya kuwazuia
hawa watu -
14:33 - 14:36waache kuchukua urithi
wa baadaye. -
14:36 - 14:38Na hicho ndicho tulichofanya.
-
14:38 - 14:42Na hata nje ya serikali,
tuliendelea kuweka msisitizo. -
14:42 - 14:46Katika nchi zetu, hakuna,
hakuna atakaye pambana na rushwa -
14:46 - 14:47isipokuwa sisi wenyewe.
-
14:47 - 14:50kwa hiyo,
hilo linakuja na matokeo, -
14:50 - 14:52na tunatakiwa kufanya kadiri tuwezavyo.
-
14:52 - 14:55Lakini nakushukuru na kuwashukuru TED
kutupa sauti -
14:55 - 14:58kuwaambia hao watu, hamtashinda,
-
14:58 - 15:01na hatutatishika
-
15:01 - 15:02Asante.
-
15:02 - 15:03(Makofi)
-
15:03 - 15:07Kelly Stoetzel: Asante sana
kwa mazungumzo yako mazuri na kazi muhimu. -
15:07 - 15:10(Makofi)
- Title:
- Jinsi gani Afrika itaendelea kukua
- Speaker:
- Ngozi Okonjo-Iweala
- Description:
-
Ukuaji wa Kiafrika ni harakati, sio ubabaishaji, anasema mchumi na aliyekuwa Waziri wa Fedha wa Nigeria Ngozi Okonjo-Iweala. Katika mazungumzo haya ya kusisimua yaliyo wazi,Okonjo Iweala anaelezea hatua endelevu barani na kuainia changamoto nane ambazo mataifa ya Kiafrika bado yanahitaji kuzungumzia ili kuweza kuwa na maisha bora baadaye.
- Video Language:
- English
- Team:
- closed TED
- Project:
- TEDTalks
- Duration:
- 15:23
Joachim Mangilima approved Swahili subtitles for How Africa can keep rising | ||
Joachim Mangilima edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising | ||
Joachim Mangilima accepted Swahili subtitles for How Africa can keep rising | ||
Leah Ligate edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising | ||
Leah Ligate edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising | ||
Leah Ligate edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising | ||
Leah Ligate edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising | ||
Leah Ligate edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising |