Return to Video

Jinsi gani Afrika itaendelea kukua

  • 0:00 - 0:04
    Simulizi za Afrika inayokua
    zinapata changamoto
  • 0:04 - 0:09
    Karibia miaka 10 iliyopita
    Niliongea kuhusu Afrika,
  • 0:09 - 0:12
    Afrika yenye matumaini na fursa,
  • 0:12 - 0:13
    Afrika ya wajasiriamali,
  • 0:14 - 0:17
    Afrika tofauti kabisa na Afrika
    ambayo umezoaea kusikia
  • 0:17 - 0:20
    ya vifo, umaskini na magonjwa.
  • 0:20 - 0:22
    Na kile nilichokiongelea,
  • 0:22 - 0:27
    ikawa sehemu ya kile kinachojulikana sasa
    kama hadithi ya Afrika inayokua.
  • 0:27 - 0:31
    Nataka niwaambie hadithi mbili
    kuhusu hii Afrika inayokua.
  • 0:31 - 0:32
    Ya kwanza inaihusisha Rwanda,
  • 0:33 - 0:36
    nchi ambayo imepitia majaribu mengi
    na dhiki.
  • 0:36 - 0:40
    Na Rwanda ikaamua kuwa kitovu
    cha teknolojia, au kitovu cha teknolojia
  • 0:40 - 0:42
    kwenye bara la Afrika.
  • 0:42 - 0:45
    Ni nchi yenye milima na ardhi ya eneo
    lenye vilima,
  • 0:45 - 0:46
    kidogo kama hapa,
  • 0:46 - 0:49
    hivyo ni vigumu sana
    kupeleka huduma kwa watu.
  • 0:49 - 0:51
    Hivyo Rwanda imesema nini?
  • 0:51 - 0:55
    Ili kuweza kuokoa maisha,
    itajaribu kutumia ndege zisizo na rubani
  • 0:55 - 0:58
    kupeleka madawa ya kuokoa maisha,
    chanjo na damu
  • 0:58 - 1:00
    kwa watu katika sehemu zisizo fikika
  • 1:00 - 1:02
    wakishirikiana na
    kampuni inayoitwa Zipline,
  • 1:03 - 1:07
    pamoja na UPS, na pia Gavi
    shirika la kimataifa la chanjo.
  • 1:07 - 1:09
    Katika kufanya hivi, itaokoa maisha.
  • 1:09 - 1:15
    Hii ni sehemu ya ubunifu
    tunayotaka kuona katika Afrika inayokua.
  • 1:15 - 1:17
    Hadithi ya pili inahusiana na jambo
  • 1:17 - 1:20
    ambalo ninauhakika wengi wenu
    mmeona au mtakumbuka.
  • 1:20 - 1:24
    Mara nyingi, nchi za Afrika
    zimeteseka na ukame na mafuriko,
  • 1:24 - 1:28
    na inaongezeka zaidi kwasababu
    ya athari za mabadiliko ya tabia nchi.
  • 1:28 - 1:34
    Wakati haya yanapotokea, kawaida
    husubiri nchi za kimataifa kuchanga fedha.
  • 1:34 - 1:37
    Unaona picha za watoto
    wakiwa na nzi kwenye nyuso zao
  • 1:37 - 1:40
    mizoga ya wanyama waliokufa na kadhalika.
  • 1:40 - 1:43
    Sasa nchi hizi,
    nchi 32, zilikutana pamoja
  • 1:43 - 1:45
    chini ya mwamvuli wa Umoja wa Afrika
  • 1:45 - 1:50
    na kuamua kuunda shirika
    linaloitwa Africa Risk Capacity.
  • 1:50 - 1:51
    Linafanya nini?
  • 1:51 - 1:54
    Ni wakala wa bima wa hali ya hewa
  • 1:54 - 1:58
    na nchi hizi zinachofanya
    ni kulipa bima kila mwaka,
  • 1:58 - 2:01
    karibia dola milioni 3 kwa mwaka
    kutoka kwenye rasilimali zao,
  • 2:01 - 2:06
    ili kwamba endapo wanakumbwa
    na hali ya ukame mgumu au mafuriko,
  • 2:06 - 2:08
    fedha hizi zitalipwa kuwasaidia
  • 2:08 - 2:11
    ambazo wanaweza kuzitumia
    kuwatunza wananchi wao
  • 2:11 - 2:14
    badala ya kusubiri msaada kuja.
  • 2:14 - 2:18
    Shirika la African Risk Capacity
    mwaka jana lilipa dola milioni 26
  • 2:18 - 2:21
    kwa Mauritania, Senegal na Niger.
  • 2:21 - 2:26
    Hii iliwawezesha kuwatunza
    watu milioni 1.3 walioathirika na ukame.
  • 2:26 - 2:29
    Waliweza kurudisha tena maisha yao,
  • 2:29 - 2:31
    kununua majani ya n'gombe
    kulisha watoto mashuleni
  • 2:31 - 2:37
    kuwafanya wananchi wabaki nyumbani
    badala ya kuhama nje ya eneo.
  • 2:37 - 2:39
    Hivyo hizi ni aina za hadithi
  • 2:39 - 2:43
    za Afrika iliyotayari
    kuchukua majikumu yake yenyewe,
  • 2:43 - 2:46
    na kutafuta suluhisho
    kwa matatizo yake yenyewe.
  • 2:46 - 2:48
    Ila simulizi hizo zinapata changamoto sasa
  • 2:48 - 2:53
    kwasababu bara letu halijafanya vema
    kwa miaka miwili iliyopita.
  • 2:53 - 2:56
    Ilikuwa inakua kwa kiwango
    cha asilimia 5 kwa mwaka
  • 2:56 - 2:58
    kwa muongo mmoja na nusu uliopita
  • 2:58 - 3:01
    lakini utabiri wa mwaka huu
    ulikuwa asilimia tatu. Kwanini?
  • 3:01 - 3:05
    kwa mazingira ya ulimwengu yanavyobadilika
    bei za bidhaa zimeshuka.
  • 3:05 - 3:08
    Uchumi wa nchi nyingi
    bado unaendeshwa na bidhaa,
  • 3:08 - 3:11
    na hivyo utendaji wake
    umeteleza
  • 3:11 - 3:15
    Na sasa suala la kujitoa kwa Uingereza
    haifanyi iwe rahisi
  • 3:15 - 3:19
    Sikujua kama Uingereza ingejitoa
  • 3:19 - 3:23
    na hilo lingekuwa moja ya vitu ambavyo
    vingeleta kutokuwa na uhakika ulimwenguni
  • 3:23 - 3:25
    kama tulivyo.
  • 3:25 - 3:27
    Hivyo sasa tuna hii hali
  • 3:27 - 3:30
    na ninafikiri ni wakati wakuangalia
  • 3:30 - 3:35
    na kusema ni vitu gani ambavyo
    nchi za Afrika zilifanya sahihi?
  • 3:35 - 3:36
    Kipi walikosea?
  • 3:37 - 3:39
    Tutajengaje kwenye haya yote
    na kujifunza
  • 3:39 - 3:42
    ili kwamba tuendeleze Afrika inayokua?
  • 3:43 - 3:46
    Hivyo ngoja niongelee kuhusu mambo sita
    ninayofikiri tulifanya sahihi.
  • 3:47 - 3:50
    La kwanza ni kusimamia
    uchumi wa nchi zetu vizuri
  • 3:50 - 3:54
    Miaka ya 80 na 90 ni miongo iliyopotea,
    wakati Afrika haikuwa ikifanya vizuri,
  • 3:54 - 3:58
    na baadhi yenu mtakumbuka ukurasa
    wa mbele wa gazeti la "Economist"
  • 3:58 - 4:00
    lililosema, "Bara lililopotea"
  • 4:00 - 4:04
    Ila miaka ya 2000 watunga sera walijifunza
  • 4:04 - 4:08
    kwamba wanahitaji kusimamia
    mazingira ya uchumi vizuri zaidi,
  • 4:08 - 4:10
    kuhakikisha uthabiti,
  • 4:10 - 4:13
    kushusha mfumuko wa bei kufika
    tarakimu moja,
  • 4:13 - 4:18
    kushusha nakisi ya bajeti, chini ya
    asilimia tatu ya Pato la Taifa,
  • 4:18 - 4:22
    wape wawekezaji, wote wa ndani na wageni,
  • 4:22 - 4:26
    aina ya uthabiti ili wawe na imani ya
    kuwekeza kwenye chumi hizi.
  • 4:26 - 4:27
    Hivyo hiyo ilikuwa namba moja.
  • 4:27 - 4:29
    Mbili, deni.
  • 4:29 - 4:35
    Mwaka 1994, urari wa deni la Pato la taifa
    wa nchi za Kiafrila ulikuwa asilimia 130,
  • 4:35 - 4:37
    na hawakuwa na nafasi ya fedha nakisi
  • 4:37 - 4:40
    Hawakuweza kutumia rasilimali zao
    kuwekeza kwenye maendeleo yao
  • 4:40 - 4:41
    kwakuwa walikuwa wanalipa deni
  • 4:41 - 4:46
    kwaweza kuwa na baadhi yenu humu ndani
    mliofanyakazi kusaidia nchi za Afrika
  • 4:46 - 4:47
    kupata unafuu wa madeni.
  • 4:47 - 4:52
    Hivyo wadai binafsi, wa pande mbalimbali
    na pande mbili waliunganika
  • 4:52 - 4:56
    na kuamua kuanzisha mpango wa
    Nchi Fukara zenye Mzigo wa madeni
  • 4:56 - 4:57
    na kutoa unafuu wa madeni.
  • 4:57 - 4:59
    Hivyo unafuu huu wa madeni mwaka 2005
  • 4:59 - 5:03
    ulifanya urari wa deni kwa Pato la taifa
    kushuka hadi takriban asilimia 30,
  • 5:03 - 5:07
    na kulikuwa na rasilimali za kutosha
    kujaribu na kuwekeza upya.
  • 5:07 - 5:09
    Kitu cha tatu kilikuwa
    makampuni yaliyopata hasara
  • 5:09 - 5:11
    Serikali zilishiriki katika biashara
  • 5:11 - 5:14
    ambazo hawakupaswa kuzifanya.
  • 5:14 - 5:17
    Na walikuwa wanaendesha biashara,
    walikuwa wanapata hasara.
  • 5:17 - 5:20
    Hivyo baadhi ya makampuni haya
    yaliundwa upya,
  • 5:20 - 5:22
    kuwa kibiashara,kubinafsishwa au kufungwa,
  • 5:22 - 5:25
    na kupunguza mzigo mkubwa
    kwa serikali.
  • 5:26 - 5:28
    Kitu cha nne kilikuwa
    kitu cha kuvutia sana
  • 5:29 - 5:31
    Mapinduzi ya makampuni ya simu yakaja,
  • 5:32 - 5:34
    na nchi za Kiafrika zikarukia.
  • 5:34 - 5:37
    Mwaka 2000, laini za simu zilikuwa
    milioni 11
  • 5:37 - 5:42
    Leo, tuna takriban laini milioni 687
    za simu za mkononi barani.
  • 5:42 - 5:44
    Na hi imetuwezesha
  • 5:44 - 5:47
    kwenda na kusonga mbele
    na teknolojia ya simu za mkononi
  • 5:47 - 5:49
    ambapo Afrika hakika inaongoza.
  • 5:49 - 5:52
    Nchini Kenya, maendeleo ya kutuma
    fedha kwa simu
  • 5:52 - 5:55
    M-Pesa, ambayo nyote
    mmesikia habari zake--
  • 5:55 - 5:58
    ilichukua muda kwa dunia
    kuona kwamba Afrika ipo mbele
  • 5:58 - 6:00
    katika hii teknolojia.
  • 6:00 - 6:03
    na hii kutuma pesa kwa simu za mkononi
    pia inatoa jukwaa
  • 6:03 - 6:05
    kwa upatikanaji wa nishati mbadala
  • 6:05 - 6:09
    Unajua, watu wanaoweza sasa kulipia sola
  • 6:09 - 6:13
    kwa njia wanayotumia kulipia
    kwa kadi kwenye simu zao.
  • 6:13 - 6:18
    Hivyo haya yalikuwa maendeleo mazuri sana
    kitu ambacho kilikwenda sahihi.
  • 6:18 - 6:23
    Tuliwekeza zaidi kwenye elimu
    na afya, isivyo vyakutosha,
  • 6:23 - 6:24
    lakini kulikuwa na maboresho.
  • 6:24 - 6:30
    Watoto milioni 25 walipata chanjo
    katika muogo mmoja nanusu uliopita.
  • 6:31 - 6:34
    Kitu kingine ilikuwa
    kwamba migogoro ilipungua.
  • 6:34 - 6:36
    Kulikuwa na migogoro mingi
    barani.
  • 6:36 - 6:37
    Wengi wenu mnafahamu hilo.
  • 6:37 - 6:42
    Lakini ilipungua, na viongozi wetu
    waliweza hata kufifiza mapinduzi.
  • 6:42 - 6:46
    Aina mpya ya migogoro imeibuka,
    na nitaielezea hiyo baadaye.
  • 6:46 - 6:50
    Hivyo kutokana na yote haya, pia
    kuna baadhi ya utofautishaji barani
  • 6:50 - 6:51
    ambao nataka muufahamu,
  • 6:52 - 6:54
    kwasababu pamoja na kuwa
  • 6:54 - 6:58
    kuna baadhi ya nchi--
    Cote d'Ivoire, Kenya, Ethiopia
  • 6:58 - 7:01
    Tanzania na Senegal
    zinafanya vizuri kwa sasa
  • 7:03 - 7:05
    Lakini tulikosea wapi?
  • 7:05 - 7:07
    Ngoja nitaje mambo nane.
  • 7:07 - 7:09
    Unapaswa kuwa umekosea zaidi
    kuliko kupatia.
  • 7:09 - 7:10
    (Kicheko)
  • 7:10 - 7:13
    Hivyo kuna mambo nane tulikosea.
  • 7:13 - 7:16
    La kwanza ilikuwa pamoja na kukua
    hatukutengeneza ajira za kutosha.
  • 7:17 - 7:19
    Hatukutengeneza ajira kwa vijana wetu.
  • 7:19 - 7:22
    Ukosefu wa ajira kwa vijana barani
    ni karibia asilimia 15,
  • 7:22 - 7:25
    na upungufu wa ajira ni tatizo kubwa.
  • 7:25 - 7:31
    Jambo la pili tulichofanya ni kuwa kiwango
    cha ukuaji hakikuwa kizuri vyakutosha
  • 7:31 - 7:34
    Hata ajira zilizoundwa
    zilikuwa ni ajira zenye tija ndogo sana,
  • 7:35 - 7:38
    hivyo tulihamisha watu
    kutoka kilimo duni kisicho na tija
  • 7:38 - 7:42
    kwenda biashara zisizo na tija
    na kufanyia kazi sekta isiyo rasmi
  • 7:42 - 7:44
    katika maeneo ya mijini.
  • 7:44 - 7:48
    Jambo la tatu ni kwamba
    kukosekana kwa usawa kuliongezeka.
  • 7:49 - 7:54
    Hivyo tuliunda mabilionea zaidi.
  • 7:54 - 7:56
    mabilionea 50 wenye thamani ya dola
    bilioni 96
  • 7:56 - 8:01
    wanamiliki utajiri zaidi kuliko watu
    milioni 75 wa chini barani.
  • 8:02 - 8:03
    Umaskini,
  • 8:04 - 8:08
    uwiano wa watu katika umaskini--
    hilo ni jambo la nne--ulipungua
  • 8:08 - 8:12
    lakini namba halisi hazikupungua
    kwasababu ya ongezeko la idadi ya watu.
  • 8:12 - 8:15
    Na ongezeko la idadi ya watu ni jambo
  • 8:15 - 8:18
    ambalo hatujafanyia
    mazungumzo ya kutosha barani.
  • 8:18 - 8:21
    Na ninafikiri tutahitaji
    kulielewa na kulifanyia kazi
  • 8:21 - 8:24
    haswa jinsi ya kuelimisha wasichana.
  • 8:25 - 8:29
    Hiyo ndio njia haswa kufanyia kazi
    hasusan kwenye suala hili.
  • 8:30 - 8:37
    Jambo la tano ni kwamba hatukuwekeza
    vya kutosha kwenye miundombinu.
  • 8:37 - 8:39
    Tulikuwa na uwekezaji kutoka kwa Wachina.
  • 8:39 - 8:42
    Ambao ulisaidia baadhi ya nchi,
    lakini haitoshi.
  • 8:42 - 8:45
    Utumiaji wa umeme
    barani Afrika
  • 8:45 - 8:49
    Kusini mwa jangwa la Sahara Afrika
    ni sawasawa na Hispania.
  • 8:49 - 8:52
    Utumiaji kwa ujumla
    ni sawasawa na ule wa Hispania
  • 8:53 - 8:55
    Hivyo watu wengi wanaishi gizani,
  • 8:55 - 8:59
    na kama Rais wa Benki ya Maendeleo
    Afrika alivyosema hivi karibuni,
  • 8:59 - 9:01
    Afrika haiwezi kuendelea gizani.
  • 9:02 - 9:04
    Kitu kingine ambacho hatujafanya
  • 9:04 - 9:10
    ni kwamba chumi zetu
    zimeshikilia muundo uliofanana
  • 9:10 - 9:11
    ambao tumekuwa nao kwa miongo.
  • 9:11 - 9:13
    Hivyo pamoja na kwamba tumekua
  • 9:13 - 9:16
    muundo wa chumi zetu
    haujabadilika kwa kiasi kikubwa.
  • 9:16 - 9:18
    Bado tunauza bidhaa nchi za nje
  • 9:18 - 9:22
    na kuuza bidhaa nchi za nje ni nini?
    kuuza ajira nchi za nje.
  • 9:22 - 9:26
    Ongezeko la thamani ya uzalishaji wetu
    ni asilimia 11 tu
  • 9:26 - 9:30
    Hatuundi ajira za kutosha kwenye
    uzalishaji kwa vijana wetu,
  • 9:30 - 9:33
    na biashara kati yetu ni kidogo.
  • 9:33 - 9:36
    Takriban asilimi 12 tu ya biashara
    kati yetu sisi wenyewe
  • 9:36 - 9:39
    Hivyo hilo ni tatizo lingine zito sana.
  • 9:39 - 9:41
    Kisha utawala bora.
  • 9:41 - 9:44
    Utawala bora ni suala zito.
  • 9:44 - 9:46
    Tuna taasisi dhaifu,
  • 9:46 - 9:51
    na wakati mwingine taasisi hewa,
    ninafikiri hii inaleta mwanya wa rushwa.
  • 9:51 - 9:56
    Rushwa ni suala ambalo bado
    hatujalimudu kiasi cha kutosha,
  • 9:56 - 9:59
    na tunatakuwa kupambana kufa na kupona,
  • 9:59 - 10:02
    hiyo na ongezeko la uwazi katika
    jinsi tunavyosimamia chumi zetu
  • 10:02 - 10:05
    na jinsi tunavyosimamia fedha zetu.
  • 10:05 - 10:10
    Tunahitaji pia kujihadhari na migogoro
    mipya,
  • 10:10 - 10:11
    aina mpya ya migogoro,
  • 10:12 - 10:15
    kama tuliyonayo na Boko Haram
    katika nchi yangu, Nigeria,
  • 10:15 - 10:17
    Na Al-Shabaab nchini Kenya.
  • 10:17 - 10:20
    Tunahitaji kushirikiana na
    washiriki wa kimataifa,
  • 10:20 - 10:23
    nchi zilizoendelea,
    kupambana juu ya hili pamoja.
  • 10:23 - 10:25
    Ama sivyo, tunaunda ukweli mpya
  • 10:25 - 10:28
    ambao sio aina tunayotaka
    kwa Afrika inayokua.
  • 10:28 - 10:32
    Na mwisho, ni suala la elimu.
  • 10:32 - 10:35
    Mifumo yetu ya elimu
    katika nchi nyingi imevunjika.
  • 10:35 - 10:40
    Hatuundi aina ya stadi
    zinazohitajika kwa siku za usoni
  • 10:40 - 10:42
    Hivyo tunatakiwa tutafute njia
    ya kutoa elimu kwa ubora.
  • 10:43 - 10:46
    Hivyo hayo ni mambo ambayo
    hatufanyi kwa usahihi.
  • 10:46 - 10:49
    Sasa, tunaenda wapi kutokea hapo?
  • 10:49 - 10:54
    Ninaamini njia ya kusongambele
    ni kujifunza kusimamia mafanikio.
  • 10:54 - 10:58
    Mara nyingi, watu wanapofanikiwa
    au nchi zinapofanikiwa
  • 10:58 - 11:00
    husahau kullichowafanya wafanikiwe.
  • 11:01 - 11:03
    Kujifunza kile unachoweza kufanikiwa,
  • 11:03 - 11:06
    kukisimamia na kukitunza
    ni jambo muhimu kwetu.
  • 11:06 - 11:08
    Hivyo vitu vyote nilivyosema
    tulifanya sahihi,
  • 11:08 - 11:12
    tunatakiwa kujifunza kuvifanya kwa usahihi
    tena, na kuviendeleza.
  • 11:12 - 11:15
    Kusimamia uchumi wakati
    unaunda ustawi ni muhimu,
  • 11:15 - 11:19
    kupata bei sahihi
    na sera thabiti.
  • 11:19 - 11:21
    Mara nyingi hatuna uthabiti
  • 11:21 - 11:24
    Mfumo wa utawala mmoja ukitoka
    unaingia mwingine
  • 11:24 - 11:27
    na wanatupa mbali hata sera zilizokuwa
    zinafanyakazi vizuri awali
  • 11:27 - 11:28
    Hii inafanya nini?
  • 11:28 - 11:31
    Inaleta sintofahamu kwa watu,
    kaya
  • 11:31 - 11:32
    sintofahamu kwa biashara
  • 11:32 - 11:35
    Hawajui jinsi na wakati wa kuwekeza.
  • 11:35 - 11:39
    Deni: tunatakiwa tusimamie' mafanikio
    tuliyopata katika kupunguza deni letu,
  • 11:39 - 11:42
    lakini sasa nchi zimerudia
    katika kukopa tena,
  • 11:42 - 11:45
    na tumeona urari wa deni kwa Pato la taifa
    unaanza kupanda tena,
  • 11:45 - 11:47
    na katika baadhi ya nchi,
  • 11:47 - 11:49
    deni linakuwa ni tatizo,
    hivyo tunatakiwa tuliepuke.
  • 11:49 - 11:51
    Hivyo usimamizi wa mafanikio
  • 11:51 - 11:53
    Kinachofuata
    ni kuwa makini sana
  • 11:53 - 11:55
    na yale mambo ambayo
    hatukufanya vizuri.
  • 11:55 - 11:57
    Kitu cha kwanza kabisa ni miundombinu
  • 11:57 - 12:01
    Ndio, nchi nyingi sasa zinatambua
    zinahitaji kuwekeza kwenye hili,
  • 12:01 - 12:03
    na zinajaribu kufanya
    kadiri ziwezavyo kufanya hivyo.
  • 12:03 - 12:05
    Lazima.
  • 12:05 - 12:06
    Kitu muhimu sana ni umeme.
  • 12:06 - 12:09
    Huwezi kuendelea katika giza.
  • 12:09 - 12:11
    Na kisha utawala bora na rushwa:
  • 12:11 - 12:12
    tunatakiwa tupambane.
  • 12:12 - 12:15
    Tunatakiwa kuendesha nchi zetu kwa uwazi.
  • 12:15 - 12:19
    Pamoja na yote hayo, lazima
    tuwashirikishe vijana.
  • 12:19 - 12:21
    Tuna ubunifu katika vijana wetu
  • 12:21 - 12:22
    Ninauona kila siku.
  • 12:22 - 12:26
    Ndio kinachoniamsha asubuhi
    na kujisikia tayari kwenda.
  • 12:26 - 12:28
    Tunatakiwa tusibanie ubunifu
    katika vijana wetu,
  • 12:28 - 12:31
    tusiwazibie njia,
    tuwaunge mkono kuunda na ugunduzi
  • 12:31 - 12:33
    na kuongoza njia.
  • 12:33 - 12:35
    Na ninajua kwamba watatuongoza
    katika mwelekeo sahihi.
  • 12:35 - 12:37
    Na wanawake wetu, na wasichana wetu:
  • 12:37 - 12:41
    tunatakiwa tutambue kwamba
    wanawake na wasichana ni zawadi.
  • 12:41 - 12:42
    Wana nguvu,
  • 12:42 - 12:44
    na tunatakiwa tusiwabanie hiyo nguvu
  • 12:44 - 12:47
    ili waweze kutoa mchango
    wao barani.
  • 12:47 - 12:51
    Nina amini kwa nguvu
    kwamba tukifanya hayo yote,
  • 12:51 - 12:54
    tutakuta kwamba simulizi za Afrika
    inayokua
  • 12:54 - 12:56
    sio ubabaishaji.
  • 12:56 - 12:57
    ni harakati.
  • 12:58 - 13:02
    Ni harakati, na tukiendelea,
    tusipowabania vijana wetu,
  • 13:02 - 13:03
    tusipowabania wanawake wetu,
  • 13:03 - 13:05
    wakati mwingine tunaweza kurudi nyuma,
  • 13:05 - 13:07
    tunaweza pia kukaa pembezoni,
  • 13:07 - 13:08
    lakini harakati ziko wazi.
  • 13:09 - 13:11
    Afrika itaendelea kukua.
  • 13:11 - 13:14
    Na ninawaambia wafanyabiashara
    mliopo kwenye hadhira hii,
  • 13:14 - 13:18
    uwekezaji Afrika sio kwa ajili ya leo,
    sio kwa ajili ya kesho,
  • 13:18 - 13:21
    sio kitu cha muda mfupi,
    ni kitu cha muda mrefu.
  • 13:21 - 13:23
    Lakini ikiwa hamtawekeza Afrika,
  • 13:24 - 13:25
    basi mtakuwa mnakosa
  • 13:25 - 13:29
    mojawapo ya fursa zinazoibuka
    duniani.
  • 13:29 - 13:30
    Asante.
  • 13:30 - 13:33
    (Makofi)
  • 13:39 - 13:42
    Kelly Stoetzel: Umegusia rushwa
    katika mazungumzo yako
  • 13:42 - 13:45
    na unafahamika vizuri
    kuwa mpambanaji thabiti wa rushwa.
  • 13:45 - 13:48
    Lakini hiyo ilikuwa na matokeo yake.
  • 13:48 - 13:51
    Watu walijibu mashambulizi,
    na mama yako alitekwa nyara.
  • 13:51 - 13:53
    Umewezaje kulimudu hili?
  • 13:53 - 13:55
    Ngozi Okonjo-Iweala:
    Imekuwa ngumu sana.
  • 13:55 - 14:00
    Asante kwa kugusia
    suala la kutekwa nyara mama yangu
  • 14:00 - 14:02
    Ni mada ngumu sana.
  • 14:02 - 14:06
    Lakini inachomaanisha
    ni kwamba unapopambana na rushwa,
  • 14:06 - 14:10
    unapogusa mifuko ya watu
    wanaoiba pesa,
  • 14:10 - 14:12
    hawanyamazi kimya tu.
  • 14:12 - 14:15
    Watajibu mashambulizi, na suala kubwa
    ni wanapojaribu kutumia vitisho
  • 14:15 - 14:19
    unakata tamaa, au unaendeleza mapambano?
  • 14:19 - 14:22
    Unatafuta njia ya kubakia
    na kujibu mashambulizi?
  • 14:22 - 14:26
    Na jibu nililokuwa nalo
    nikiwa na timu zilizofanya nazo kazi
  • 14:26 - 14:28
    ni kuendeleza mapambano
  • 14:28 - 14:30
    Tunatakiwa kuunda hizo taasisi.
  • 14:30 - 14:33
    Tunatakiwa kutafuta njia ya kuwazuia
    hawa watu
  • 14:33 - 14:36
    waache kuchukua urithi
    wa baadaye.
  • 14:36 - 14:38
    Na hicho ndicho tulichofanya.
  • 14:38 - 14:42
    Na hata nje ya serikali,
    tuliendelea kuweka msisitizo.
  • 14:42 - 14:46
    Katika nchi zetu, hakuna,
    hakuna atakaye pambana na rushwa
  • 14:46 - 14:47
    isipokuwa sisi wenyewe.
  • 14:47 - 14:50
    kwa hiyo,
    hilo linakuja na matokeo,
  • 14:50 - 14:52
    na tunatakiwa kufanya kadiri tuwezavyo.
  • 14:52 - 14:55
    Lakini nakushukuru na kuwashukuru TED
    kutupa sauti
  • 14:55 - 14:58
    kuwaambia hao watu, hamtashinda,
  • 14:58 - 15:01
    na hatutatishika
  • 15:01 - 15:02
    Asante.
  • 15:02 - 15:03
    (Makofi)
  • 15:03 - 15:07
    Kelly Stoetzel: Asante sana
    kwa mazungumzo yako mazuri na kazi muhimu.
  • 15:07 - 15:10
    (Makofi)
Title:
Jinsi gani Afrika itaendelea kukua
Speaker:
Ngozi Okonjo-Iweala
Description:

Ukuaji wa Kiafrika ni harakati, sio ubabaishaji, anasema mchumi na aliyekuwa Waziri wa Fedha wa Nigeria Ngozi Okonjo-Iweala. Katika mazungumzo haya ya kusisimua yaliyo wazi,Okonjo Iweala anaelezea hatua endelevu barani na kuainia changamoto nane ambazo mataifa ya Kiafrika bado yanahitaji kuzungumzia ili kuweza kuwa na maisha bora baadaye.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
15:23
Joachim Mangilima approved Swahili subtitles for How Africa can keep rising
Joachim Mangilima edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising
Joachim Mangilima accepted Swahili subtitles for How Africa can keep rising
Leah Ligate edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising
Leah Ligate edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising
Leah Ligate edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising
Leah Ligate edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising
Leah Ligate edited Swahili subtitles for How Africa can keep rising
Show all

Swahili subtitles

Revisions