Jinsi nilivyojifunza kusoma --na biashara ya hisa -- gerezani
-
0:01 - 0:03Nilikuwa na umri wa miaka 14
-
0:03 - 0:05nikiwa kwenye jumba la michezo,
-
0:05 - 0:06nikiiba kwenye mashine ya mchezo,
-
0:07 - 0:09na nilipokuwa nikitoka nje ya jengo
-
0:09 - 0:11mlinzi alikamata mkono wangu,
hivyo nikakimbia. -
0:12 - 0:15Nilikimbilia mtaani,
na nikaruka juu ya uzio. -
0:15 - 0:16Na nilipofika juu,
-
0:16 - 0:19uzito wa sarafu 3,000 kwenye mkoba wangu
-
0:19 - 0:20ulinielemea na kunivuta chini.
-
0:21 - 0:24Niliponyanyuka, mlinzi
alikuwa amesima juu yangu, -
0:24 - 0:27na akasema, "Siku nyingine nyinyi vibaka,
ibeni vitu mnavyoweza kubeba." -
0:27 - 0:29(Kicheko)
-
0:29 - 0:32Nilipelekwa kwenye mahabusu ya watoto
-
0:32 - 0:34na nilipoachiliwa
chini ya dhamana ya mama yangu, -
0:35 - 0:38maneno ya kwanza mjomba wangu
alisema yalikuwa, "Ulikamatwaje?" -
0:38 - 0:40Nikasema, "Mzee, mkoba
ulikuwa mzito sana." -
0:40 - 0:43Akasema, "Mzee,
hukutakiwa kuchukua sarafu zote." -
0:43 - 0:46Nikasema, "Mzee, zilikuwa ndogo.
Ningefanyaje?" -
0:46 - 0:51na dakika 10 baadaye, alinipeleka kuiba
kwenye mashine nyingine ya mchezo. -
0:51 - 0:53Tulihitaji pesa ya petroli kufika maskani.
-
0:53 - 0:55Hayo ndiyo yalikuwa maisha yangu.
-
0:55 - 0:57Nimekulia Oakland, Kalifornia,
-
0:57 - 1:00na mama yangu
na ndugu wa karibu wa familia -
1:00 - 1:01walevi wa madawa ya kulevya ya kokeini .
-
1:02 - 1:06Mazingira yangu yalijumuisha
kuishi na familia, marafiki, -
1:07 - 1:09na makazi kwa wasio-na-makazi.
-
1:09 - 1:13Mara nyingi, mlo wa jioni tuliupata
kwenye foleni za vyakula vya msaada. -
1:13 - 1:15Mjomba aliniambia hivi:
-
1:15 - 1:17pesa inatawala dunia
-
1:17 - 1:19na kila kitu ndani yake.
-
1:19 - 1:21Na katika hii mitaa, pesa ni Mfalme.
-
1:21 - 1:23Na ikiwa utafuata pesa,
-
1:23 - 1:25itakupeleka kwa mtu mbaya au mtu mzuri.
-
1:26 - 1:29Baadaye kidogo,
nilifanya uhalifu wangu wa kwanza, -
1:29 - 1:32na ndiyo mara ya kwanza
nilipoambiwa kuwa nina kipaji -
1:32 - 1:34na nikajisikia kuwa kuna mtu ananiaminia.
-
1:34 - 1:37Hakuna aliyewahi-niambia kuwa
ningeweza kuwa mwanasheria, -
1:37 - 1:38daktari au mhandisi.
-
1:38 - 1:42Yaani, ningewezaje kufanya hivyo?
Sikuweza kusoma, kuandika wala kutahajia. -
1:42 - 1:43Sikuwa mtu aliyesoma.
-
1:43 - 1:46Kwahiyo, mara zote nilifikiri
uhalifu ndio njia ya kwenda. -
1:47 - 1:49Na kisha siku moja
-
1:49 - 1:50Nilikuwa naongea na mtu
-
1:50 - 1:54na alikuwa ananiambia juu ya
huu wizi ambao tungeweza fanya. -
1:55 - 1:56Na tukaufanya.
-
1:57 - 1:59Ukweli ni kwamba nilikuwa nakulia
-
1:59 - 2:01kwenye nchi yenye uwezo mkubwa
wa kifedha duniani, -
2:01 - 2:03Marekani,
-
2:03 - 2:07huku nikiangalia mama yangu,
akisimama kwenye foleni ya benki ya damu -
2:09 - 2:12kuuza damu yake kwa Dola 40
kujaribu tu kulisha wanae. -
2:13 - 2:17Bado ana alama za sindano
mikononi mwake leo kudhihirisha hilo. -
2:17 - 2:19Kwa hiyo sikuijali jumuiya yangu,
-
2:19 - 2:21Hawakujali maisha yangu.
-
2:21 - 2:24Kila mtu pale alifanya anachotaka fanya kupata alichotaka,
-
2:24 - 2:26wauza mihadarati,
wezi, benki ya damu. -
2:26 - 2:28Kila mtu alichukua fedha ya damu.
-
2:28 - 2:30Hivyo nilipata yangu
kwa njia yoyote ile. -
2:30 - 2:32Nilipata yangu.
-
2:32 - 2:34Elimu ya fedha
kweli ilitawala dunia, -
2:35 - 2:37na nilikuwa mtoto mtumwa kwake
-
2:37 - 2:38nikifuata mtu mbaya.
-
2:40 - 2:43Nikiwa na miaka 17,
nilikamatwa kwa wizi na mauaji -
2:43 - 2:47na punde nikajifunza kuwa fedha jela
zinatawala zaidi ya zilivyo mitaani, -
2:47 - 2:49Hivyo nilitaka kuingia.
-
2:50 - 2:53Siku moja, nilikurupuka kushika
ukurasa wa michezo katika gazeti -
2:53 - 2:54ili mfungwa mwenzangu anisomee,
-
2:55 - 2:57na kwa bahati mbaya
nikachukua sehemu ya biashara. -
2:57 - 3:00Na huyu mzee akasema,
"Hey, kijana, umechukua hisa?" -
3:00 - 3:01Na nikasema, "Ndio nini hicho?"
-
3:02 - 3:05Akasema, "Hiyo ndiyo sehemu ambayo
watu weupe huweka pesa yao yote." -
3:05 - 3:06(Kicheko)
-
3:06 - 3:10Na ilikuwa ndiyo mara ya kwanza
nilipata ono fupi la tumaini, -
3:10 - 3:11siku za baadaye.
-
3:11 - 3:14Alinipa maelezo mafupi
ya hisa zilikuwa ni nini, -
3:15 - 3:16lakini ilikuwa ni muhtasari tu.
-
3:18 - 3:20Yaani, ningewezaje kuifanya?
-
3:20 - 3:22Sikuweza kusoma, kuandika wala kutahajia.
-
3:23 - 3:25Ujuzi niliokuwa nimeukuza
kuficha kutokusoma kwangu -
3:25 - 3:27haukufanya kazi tena
katika mazingira haya. -
3:27 - 3:30Nilikuwa nimenaswa kwenye kizimba
mateka kati ya watekaji, -
3:30 - 3:32nikipigania uhuru ambao sijawahi kuwa nao.
-
3:32 - 3:34Nilikuwa nimepotea, nimechoka,
-
3:34 - 3:36na sikuwa na machaguzi.
-
3:37 - 3:39Kwa hiyo nikiwa na miaka 20,
-
3:39 - 3:42nilifanya kitu kigumu kuliko vyote
nilivyowahi kufanya maishani mwangu. -
3:42 - 3:43Nilichukua kitabu,
-
3:45 - 3:48na ilikuwa ni kipindi kigumu sana
maishani mwangu. -
3:49 - 3:51kujaribu kujifunza jinsi ya kusoma,
-
3:51 - 3:54kutengana na familia yangu,
-
3:54 - 3:55na rafiki zangu.
-
3:56 - 3:58Ilikuwa shida, mzee.
-
3:58 - 3:59Ilikuwa ni mahangaiko.
-
3:59 - 4:01Lakini sikufahamu japo kidogo kuwa
-
4:01 - 4:04nilikuwa napata zawadi kubwa kuliko zote
nilizowahi kuziota, -
4:04 - 4:06kujithamini,
-
4:06 - 4:08maarifa, nidhamu.
-
4:09 - 4:13Nilisisimka mno kusoma, kiasi kwamba
nilisoma kila kitu nilichokitia mkononi: -
4:13 - 4:16makaratasi ya pipi, nembo za nguo,
alama za barabarani, kila kitu. -
4:16 - 4:17Nilikuwa nikisoma tu vitu!
-
4:17 - 4:18(Makofi na Vifijo)
-
4:18 - 4:20kusoma tu vitu.
-
4:21 - 4:25Nilisisimka sana kujua jinsi ya kusoma
na kujua jinsi ya kutahajia. -
4:25 - 4:27Rafiki alikuja, akaniuliza,
"Mzee, unakula nini?" -
4:27 - 4:29Nikasema, "P-I-P-I, pipi."
-
4:29 - 4:31(Kicheko)
-
4:31 - 4:34Akasema, "Nipe kidogo."
Nikasema, "L-A. La." -
4:34 - 4:35(Kicheko)
-
4:35 - 4:36Ilikuwa babukubwa.
-
4:36 - 4:39Yaani, sasa naweza, kwa mara ya kwanza
katika maisha yangu, kusoma. -
4:39 - 4:41Hisia niliyoipata, ni ya kustaajabu sana.
-
4:43 - 4:46Kisha, nikiwa na miaka 22,
nikijisikia mwenyewe, -
4:47 - 4:49nikijiamini,
-
4:49 - 4:50Nilikumbuka kile yule mzee aliniambia.
-
4:52 - 4:55Kwa hiyo nilichukua
kurasa za biashara za gazeti. -
4:56 - 4:57Nilitaka kuwatafuta hawa matajiri weupe.
-
4:57 - 4:59(Kicheko)
-
5:01 - 5:02Kwa hiyo nilitafuta ule muhtasari.
-
5:03 - 5:05Nilipokuwa nikijiendeleza kikazi
-
5:05 - 5:09nikifundisha wengine namna ya
kusimamia fedha na kuwekeza, -
5:09 - 5:12punde nikajifunza kuwa
nilihitaji kuwajibika kwa matendo yangu. -
5:12 - 5:15Kweli,
nilikulia kwenye mazingira tata sana, -
5:15 - 5:17lakini nilichagua kufanya uhalifu,
-
5:17 - 5:19na nilipaswa kukiri hilo.
-
5:19 - 5:22Nilipaswa kuwajibika kwa hilo,
na nilifanya hivyo. -
5:22 - 5:25Nilikuwa nikiunda mtaala ambao
ungeweza kuwafundisha wafungwa -
5:25 - 5:27namna ya kusimamia fedha
kupitia ajira za gerezani. -
5:29 - 5:32Kutiisha mtindo wetu wa maisha
kungeweza kutoa zana zihamishikazo -
5:32 - 5:35ambazo tunaweza kuzitumia kusimamia fedha
tunapoirudi kwenye jamii, -
5:35 - 5:39kama watu wengi walivyofanya
ambao hawakufanya uhalifu. -
5:39 - 5:40Kisha niligundua
-
5:41 - 5:43kulingana takwimu ya MarketWatch,
-
5:43 - 5:45zaidi ya asilimia 60 ya wakazi wa Marekani
-
5:45 - 5:47wana chini ya Dola 1,000 katika akiba.
-
5:48 - 5:51Michezo ilielezea kwamba zaidi ya asilimia 60 ya wachezaji wa NBA
-
5:51 - 5:53na wachezaji wa NFL hufilisika.
-
5:53 - 5:56Asilimia 40 ya matatizo ya ndoa
hutokana na masuala ya kifedha. -
5:57 - 5:58Balaa gani?
-
5:58 - 6:00(Kicheko)
-
6:00 - 6:03Unataka kuniambia,
watu wamefanya kazi maisha yao yote, -
6:03 - 6:06wakinunua magari, nguo, nyumba
na vitu mbalimbali -
6:06 - 6:08lakini walikuwa waliishi hundi kwa hundi?
-
6:08 - 6:12Ni namna gani duniani wanajamii
wangekwenda kuwasaidia wafungwa -
6:12 - 6:14kurudi kwenye jamii
-
6:14 - 6:16ikiwa hawakuweza kusimamia
mambo yao wenyewe? -
6:16 - 6:17Tumevurugwa.
-
6:17 - 6:19(Kicheko)
-
6:19 - 6:21Nahitaji mpango mzuri zaidi.
-
6:23 - 6:25Hii haitakwenda kufanya kazi vizuri.
-
6:25 - 6:26Hivyo ...
-
6:28 - 6:29Nilifikiria.
-
6:32 - 6:35Sasa nilikuwa na wajibu kukutana
na wale waliokuwa kwenye mkondo huo -
6:36 - 6:38na kuwasaidia,
-
6:38 - 6:41na ilikuwa ni ajabu sababu
sasa nilijali jumuiya yangu -
6:41 - 6:43Lo, hebu fikiria.
Nilijali kuhusu jumuiya yangu. -
6:45 - 6:47Ujinga juu ya Fedha ni ugonjwa
-
6:47 - 6:50ambao umedhohofisha wachache
na walio chini katika jamii yetu -
6:50 - 6:52kwa vizazi na vizazi,
-
6:52 - 6:55na tunapaswa kukasirika juu ya hilo.
-
6:55 - 6:56Ebu jiulize:
-
6:56 - 7:00Inawezekanaje asilimia 50
ya wakazi wa Marekani -
7:00 - 7:04wasiwe na elimu ya fedha katika nchi
inayoendeshwa kwa ustawi wa kifedha? -
7:05 - 7:08Kupatikana kwa haki kwetu,
hadhi yetu ya kijamii, -
7:08 - 7:11hali ya maisha, usafirishaji na chakula
-
7:11 - 7:14vyote vinategemea fedha
ambayo watu wengi hawawezi kuisimamia. -
7:14 - 7:16Ni ajabu!
-
7:16 - 7:17Ni janga
-
7:17 - 7:20na hatari kubwa kwa usalama wa umma
kuliko suala jingine lolote. -
7:22 - 7:24Kadiri ya
Kitengo cha Urekebishaji cha Kalifornia, -
7:24 - 7:27zaidi ya asilimia 70 ya wale waliofungwa
-
7:27 - 7:30wamefanya au wameshtakiwa kwa uhalifu
uhusianao na fedha: -
7:30 - 7:35wizi wa kutumia nguvu, kuvunja nyumba,
kutapeli, uporaji, ghusubu -- -
7:36 - 7:37na orodha inaendelea.
-
7:38 - 7:39Angalia hii:
-
7:39 - 7:42Mfungwa wa kawaida
-
7:42 - 7:45huingia katika mfumo wa gereza
wa Kalifornia -
7:45 - 7:46pasipo kuwa na elimu ya fedha,
-
7:47 - 7:49hupata ujira wa senti 30 kwa saa,
-
7:49 - 7:51zaidi ya Dola 800 kwa mwaka,
-
7:51 - 7:54bila ya kuwa na matumizi yoyote
na kuweka akiba yoyote. -
7:55 - 7:59Anapopewa msamaha,
hupewa dola 200 pesa ya geti na kuambiwa, -
7:59 - 8:02"Wee, mafanikio mema, kaa mbali na
matatizo. Usirudi gerezani tena." -
8:03 - 8:06Bila kuwa na maandalizi yoyote ya maana
au mpango fedha wa muda mrefu, -
8:06 - 8:07anafanyaje ...?
-
8:09 - 8:10Akiwa na miaka 60?
-
8:11 - 8:12Apate kazi nzuri,
-
8:12 - 8:16au arudi kwenye tabia ile ile ya uhalifu
iliyompeleka gerezani kwanza? -
8:17 - 8:19Nyinyi walipakodi, chagueni wenyewe.
-
8:19 - 8:22Hakika, elimu yake
imeshamchagulia, pengine. -
8:23 - 8:25Kwa hiyo, tunatibuje ugonjwa huu?
-
8:26 - 8:28Nilishiriki kuanzisha programu
-
8:28 - 8:33tuliyoiita Elimu Hisia
ya Uwezeshaji wa Kifedha -
8:33 - 8:34tunaiita FEEL
-
8:34 - 8:37na inafundisha namna ya kutenganisha
maamuzi ya kihisia -
8:37 - 8:39na maamuzi ya kifedha,
-
8:39 - 8:43na sheria 4 aushi
za utawala fedha binafsi: -
8:43 - 8:44njia sahihi ya kuweka akiba,
-
8:46 - 8:47kudhibiti gharama zako za maisha,
-
8:48 - 8:50kukopa fedha kwenye ufanisi
-
8:50 - 8:54kutawanya fedha yako
kuruhusu fedha yako ikufanyie kazi -
8:54 - 8:56badala ya wewe kuifanyia kazi.
-
8:56 - 9:00Wafungwa wanahitaji ujuzi huu
kabla ya kuingia tena kwenye jamii. -
9:01 - 9:05Hatuwezi kubadilika kuwa na maisha
ya kawaida bila ujuzi huu wa maisha. -
9:05 - 9:09Hii dhana kuwa ni Weledi tu
wanaweza kuwekeza na kusimamia fedha -
9:09 - 9:11ni ya fedheha kabisa,
-
9:12 - 9:14na yeyote aliyewaambia hivyo anadanganya.
-
9:14 - 9:18(Makofi na Vifijo)
-
9:18 - 9:21Mweledi ni mtu
-
9:21 - 9:23anayejua kazi zake kuliko walio wengi,
-
9:23 - 9:28na hakuna mtu ajuaye kiasi gani cha fedha
wahitaji, unacho, au wataka zaidi ya wewe, -
9:28 - 9:30ikimaanisha kuwa wewe ni mweledi.
-
9:31 - 9:35Elimu ya fedha siyo stadi,
mabibi na mabwana. -
9:35 - 9:36Ni mtindo wa maisha.
-
9:38 - 9:42Uimara wa kifedha ni matokeo ya ziada
ya mtindo sahihi wa maisha. -
9:42 - 9:46Mfungwa mwenye elimu nzuri ya kifedha
anaweza kuwa mwananchi mlipakodi, -
9:47 - 9:50na mwananchi mlipakodi mwenye elimu
nzuri ya kifedha anaweza kubaki hivyo. -
9:50 - 9:55Hii inatuwezesha kuunda daraja
kati ya wale watu tunaowashawishi: -
9:55 - 9:57familia, marafiki na wale vijana
-
9:57 - 10:00ambao bado wanaamini
kuwa uhalifu na pesa vina uhusiano. -
10:02 - 10:05Kwa hiyo tupoteze uwoga na wasiwasi
-
10:05 - 10:06wa maneno makubwa ya kifedha
-
10:06 - 10:10na ujinga mwingine wote
ambao mmekuwa mkisikia huko nje. -
10:10 - 10:14Na tujikite kwenye kiini
kilichokuwa kinadhoofisha jamii yetu -
10:14 - 10:18kuanzia kutimiza wajibu wako
la kuwa meneja mzuri wa maisha. -
10:19 - 10:22Na tutoe mtaala mwepesi na rahisi kutumia
-
10:22 - 10:25ambao utaingia kwenye kiini, kiini
-
10:25 - 10:29cha ni nini ukweli wa
uwezeshaji wa kifedha na elimu ya hisia. -
10:29 - 10:31Sasa, ikiwa umekaa hapa kwa wasikilizaji
na umesema, -
10:32 - 10:34"Ndiyo, kweli, hiyo si mimi
na sikubaliani nayo," -
10:34 - 10:35basi njoo uchukue somo langu --
-
10:35 - 10:37(Kicheko)
-
10:37 - 10:41ili nikuoneshe ni kiasi gani cha pesa
inakugharimu kila unaposhikwa na hisia. -
10:42 - 10:45(Makofi na Vifijo)
-
10:48 - 10:49Asanteni sana. Asanteni.
-
10:49 - 10:50(Makofi na Vifijo)
- Title:
- Jinsi nilivyojifunza kusoma --na biashara ya hisa -- gerezani
- Speaker:
- Curtis 'Wall Street' Carroll
- Description:
-
Elimu ya fedha siyo stadi -- ni mtindo wa maisha. Chukua hiyo kutoka kwa Curtis "Wall Street" Carroll. Kama mfungwa, Carroll anajua nguvu ya dola(fedha). Akiwa gerezani, alijifunza jinsi ya kusoma na kufanya biashara ya hisa, na sasa anashirikisha ujumbe rahisi, na wenye nguvu: wote tuhanitaji kuwa werevu na pesa zetu.
- Video Language:
- English
- Team:
- closed TED
- Project:
- TEDTalks
- Duration:
- 10:50
Joachim Mangilima approved Swahili subtitles for How I learned to read -- and trade stocks -- in prison | ||
Joachim Mangilima edited Swahili subtitles for How I learned to read -- and trade stocks -- in prison | ||
Nelson Simfukwe accepted Swahili subtitles for How I learned to read -- and trade stocks -- in prison | ||
Nelson Simfukwe edited Swahili subtitles for How I learned to read -- and trade stocks -- in prison | ||
Clarence Bitegeko edited Swahili subtitles for How I learned to read -- and trade stocks -- in prison | ||
Clarence Bitegeko edited Swahili subtitles for How I learned to read -- and trade stocks -- in prison | ||
Clarence Bitegeko edited Swahili subtitles for How I learned to read -- and trade stocks -- in prison | ||
Clarence Bitegeko edited Swahili subtitles for How I learned to read -- and trade stocks -- in prison |