Return to Video

Jinsi nilivyojifunza kusoma --na biashara ya hisa -- gerezani

  • 0:01 - 0:03
    Nilikuwa na umri wa miaka 14
  • 0:03 - 0:05
    nikiwa kwenye jumba la michezo,
  • 0:05 - 0:06
    nikiiba kwenye mashine ya mchezo,
  • 0:07 - 0:09
    na nilipokuwa nikitoka nje ya jengo
  • 0:09 - 0:11
    mlinzi alikamata mkono wangu,
    hivyo nikakimbia.
  • 0:12 - 0:15
    Nilikimbilia mtaani,
    na nikaruka juu ya uzio.
  • 0:15 - 0:16
    Na nilipofika juu,
  • 0:16 - 0:19
    uzito wa sarafu 3,000 kwenye mkoba wangu
  • 0:19 - 0:20
    ulinielemea na kunivuta chini.
  • 0:21 - 0:24
    Niliponyanyuka, mlinzi
    alikuwa amesima juu yangu,
  • 0:24 - 0:27
    na akasema, "Siku nyingine nyinyi vibaka,
    ibeni vitu mnavyoweza kubeba."
  • 0:27 - 0:29
    (Kicheko)
  • 0:29 - 0:32
    Nilipelekwa kwenye mahabusu ya watoto
  • 0:32 - 0:34
    na nilipoachiliwa
    chini ya dhamana ya mama yangu,
  • 0:35 - 0:38
    maneno ya kwanza mjomba wangu
    alisema yalikuwa, "Ulikamatwaje?"
  • 0:38 - 0:40
    Nikasema, "Mzee, mkoba
    ulikuwa mzito sana."
  • 0:40 - 0:43
    Akasema, "Mzee,
    hukutakiwa kuchukua sarafu zote."
  • 0:43 - 0:46
    Nikasema, "Mzee, zilikuwa ndogo.
    Ningefanyaje?"
  • 0:46 - 0:51
    na dakika 10 baadaye, alinipeleka kuiba
    kwenye mashine nyingine ya mchezo.
  • 0:51 - 0:53
    Tulihitaji pesa ya petroli kufika maskani.
  • 0:53 - 0:55
    Hayo ndiyo yalikuwa maisha yangu.
  • 0:55 - 0:57
    Nimekulia Oakland, Kalifornia,
  • 0:57 - 1:00
    na mama yangu
    na ndugu wa karibu wa familia
  • 1:00 - 1:01
    walevi wa madawa ya kulevya ya kokeini .
  • 1:02 - 1:06
    Mazingira yangu yalijumuisha
    kuishi na familia, marafiki,
  • 1:07 - 1:09
    na makazi kwa wasio-na-makazi.
  • 1:09 - 1:13
    Mara nyingi, mlo wa jioni tuliupata
    kwenye foleni za vyakula vya msaada.
  • 1:13 - 1:15
    Mjomba aliniambia hivi:
  • 1:15 - 1:17
    pesa inatawala dunia
  • 1:17 - 1:19
    na kila kitu ndani yake.
  • 1:19 - 1:21
    Na katika hii mitaa, pesa ni Mfalme.
  • 1:21 - 1:23
    Na ikiwa utafuata pesa,
  • 1:23 - 1:25
    itakupeleka kwa mtu mbaya au mtu mzuri.
  • 1:26 - 1:29
    Baadaye kidogo,
    nilifanya uhalifu wangu wa kwanza,
  • 1:29 - 1:32
    na ndiyo mara ya kwanza
    nilipoambiwa kuwa nina kipaji
  • 1:32 - 1:34
    na nikajisikia kuwa kuna mtu ananiaminia.
  • 1:34 - 1:37
    Hakuna aliyewahi-niambia kuwa
    ningeweza kuwa mwanasheria,
  • 1:37 - 1:38
    daktari au mhandisi.
  • 1:38 - 1:42
    Yaani, ningewezaje kufanya hivyo?
    Sikuweza kusoma, kuandika wala kutahajia.
  • 1:42 - 1:43
    Sikuwa mtu aliyesoma.
  • 1:43 - 1:46
    Kwahiyo, mara zote nilifikiri
    uhalifu ndio njia ya kwenda.
  • 1:47 - 1:49
    Na kisha siku moja
  • 1:49 - 1:50
    Nilikuwa naongea na mtu
  • 1:50 - 1:54
    na alikuwa ananiambia juu ya
    huu wizi ambao tungeweza fanya.
  • 1:55 - 1:56
    Na tukaufanya.
  • 1:57 - 1:59
    Ukweli ni kwamba nilikuwa nakulia
  • 1:59 - 2:01
    kwenye nchi yenye uwezo mkubwa
    wa kifedha duniani,
  • 2:01 - 2:03
    Marekani,
  • 2:03 - 2:07
    huku nikiangalia mama yangu,
    akisimama kwenye foleni ya benki ya damu
  • 2:09 - 2:12
    kuuza damu yake kwa Dola 40
    kujaribu tu kulisha wanae.
  • 2:13 - 2:17
    Bado ana alama za sindano
    mikononi mwake leo kudhihirisha hilo.
  • 2:17 - 2:19
    Kwa hiyo sikuijali jumuiya yangu,
  • 2:19 - 2:21
    Hawakujali maisha yangu.
  • 2:21 - 2:24
    Kila mtu pale alifanya anachotaka fanya kupata alichotaka,
  • 2:24 - 2:26
    wauza mihadarati,
    wezi, benki ya damu.
  • 2:26 - 2:28
    Kila mtu alichukua fedha ya damu.
  • 2:28 - 2:30
    Hivyo nilipata yangu
    kwa njia yoyote ile.
  • 2:30 - 2:32
    Nilipata yangu.
  • 2:32 - 2:34
    Elimu ya fedha
    kweli ilitawala dunia,
  • 2:35 - 2:37
    na nilikuwa mtoto mtumwa kwake
  • 2:37 - 2:38
    nikifuata mtu mbaya.
  • 2:40 - 2:43
    Nikiwa na miaka 17,
    nilikamatwa kwa wizi na mauaji
  • 2:43 - 2:47
    na punde nikajifunza kuwa fedha jela
    zinatawala zaidi ya zilivyo mitaani,
  • 2:47 - 2:49
    Hivyo nilitaka kuingia.
  • 2:50 - 2:53
    Siku moja, nilikurupuka kushika
    ukurasa wa michezo katika gazeti
  • 2:53 - 2:54
    ili mfungwa mwenzangu anisomee,
  • 2:55 - 2:57
    na kwa bahati mbaya
    nikachukua sehemu ya biashara.
  • 2:57 - 3:00
    Na huyu mzee akasema,
    "Hey, kijana, umechukua hisa?"
  • 3:00 - 3:01
    Na nikasema, "Ndio nini hicho?"
  • 3:02 - 3:05
    Akasema, "Hiyo ndiyo sehemu ambayo
    watu weupe huweka pesa yao yote."
  • 3:05 - 3:06
    (Kicheko)
  • 3:06 - 3:10
    Na ilikuwa ndiyo mara ya kwanza
    nilipata ono fupi la tumaini,
  • 3:10 - 3:11
    siku za baadaye.
  • 3:11 - 3:14
    Alinipa maelezo mafupi
    ya hisa zilikuwa ni nini,
  • 3:15 - 3:16
    lakini ilikuwa ni muhtasari tu.
  • 3:18 - 3:20
    Yaani, ningewezaje kuifanya?
  • 3:20 - 3:22
    Sikuweza kusoma, kuandika wala kutahajia.
  • 3:23 - 3:25
    Ujuzi niliokuwa nimeukuza
    kuficha kutokusoma kwangu
  • 3:25 - 3:27
    haukufanya kazi tena
    katika mazingira haya.
  • 3:27 - 3:30
    Nilikuwa nimenaswa kwenye kizimba
    mateka kati ya watekaji,
  • 3:30 - 3:32
    nikipigania uhuru ambao sijawahi kuwa nao.
  • 3:32 - 3:34
    Nilikuwa nimepotea, nimechoka,
  • 3:34 - 3:36
    na sikuwa na machaguzi.
  • 3:37 - 3:39
    Kwa hiyo nikiwa na miaka 20,
  • 3:39 - 3:42
    nilifanya kitu kigumu kuliko vyote
    nilivyowahi kufanya maishani mwangu.
  • 3:42 - 3:43
    Nilichukua kitabu,
  • 3:45 - 3:48
    na ilikuwa ni kipindi kigumu sana
    maishani mwangu.
  • 3:49 - 3:51
    kujaribu kujifunza jinsi ya kusoma,
  • 3:51 - 3:54
    kutengana na familia yangu,
  • 3:54 - 3:55
    na rafiki zangu.
  • 3:56 - 3:58
    Ilikuwa shida, mzee.
  • 3:58 - 3:59
    Ilikuwa ni mahangaiko.
  • 3:59 - 4:01
    Lakini sikufahamu japo kidogo kuwa
  • 4:01 - 4:04
    nilikuwa napata zawadi kubwa kuliko zote
    nilizowahi kuziota,
  • 4:04 - 4:06
    kujithamini,
  • 4:06 - 4:08
    maarifa, nidhamu.
  • 4:09 - 4:13
    Nilisisimka mno kusoma, kiasi kwamba
    nilisoma kila kitu nilichokitia mkononi:
  • 4:13 - 4:16
    makaratasi ya pipi, nembo za nguo,
    alama za barabarani, kila kitu.
  • 4:16 - 4:17
    Nilikuwa nikisoma tu vitu!
  • 4:17 - 4:18
    (Makofi na Vifijo)
  • 4:18 - 4:20
    kusoma tu vitu.
  • 4:21 - 4:25
    Nilisisimka sana kujua jinsi ya kusoma
    na kujua jinsi ya kutahajia.
  • 4:25 - 4:27
    Rafiki alikuja, akaniuliza,
    "Mzee, unakula nini?"
  • 4:27 - 4:29
    Nikasema, "P-I-P-I, pipi."
  • 4:29 - 4:31
    (Kicheko)
  • 4:31 - 4:34
    Akasema, "Nipe kidogo."
    Nikasema, "L-A. La."
  • 4:34 - 4:35
    (Kicheko)
  • 4:35 - 4:36
    Ilikuwa babukubwa.
  • 4:36 - 4:39
    Yaani, sasa naweza, kwa mara ya kwanza
    katika maisha yangu, kusoma.
  • 4:39 - 4:41
    Hisia niliyoipata, ni ya kustaajabu sana.
  • 4:43 - 4:46
    Kisha, nikiwa na miaka 22,
    nikijisikia mwenyewe,
  • 4:47 - 4:49
    nikijiamini,
  • 4:49 - 4:50
    Nilikumbuka kile yule mzee aliniambia.
  • 4:52 - 4:55
    Kwa hiyo nilichukua
    kurasa za biashara za gazeti.
  • 4:56 - 4:57
    Nilitaka kuwatafuta hawa matajiri weupe.
  • 4:57 - 4:59
    (Kicheko)
  • 5:01 - 5:02
    Kwa hiyo nilitafuta ule muhtasari.
  • 5:03 - 5:05
    Nilipokuwa nikijiendeleza kikazi
  • 5:05 - 5:09
    nikifundisha wengine namna ya
    kusimamia fedha na kuwekeza,
  • 5:09 - 5:12
    punde nikajifunza kuwa
    nilihitaji kuwajibika kwa matendo yangu.
  • 5:12 - 5:15
    Kweli,
    nilikulia kwenye mazingira tata sana,
  • 5:15 - 5:17
    lakini nilichagua kufanya uhalifu,
  • 5:17 - 5:19
    na nilipaswa kukiri hilo.
  • 5:19 - 5:22
    Nilipaswa kuwajibika kwa hilo,
    na nilifanya hivyo.
  • 5:22 - 5:25
    Nilikuwa nikiunda mtaala ambao
    ungeweza kuwafundisha wafungwa
  • 5:25 - 5:27
    namna ya kusimamia fedha
    kupitia ajira za gerezani.
  • 5:29 - 5:32
    Kutiisha mtindo wetu wa maisha
    kungeweza kutoa zana zihamishikazo
  • 5:32 - 5:35
    ambazo tunaweza kuzitumia kusimamia fedha
    tunapoirudi kwenye jamii,
  • 5:35 - 5:39
    kama watu wengi walivyofanya
    ambao hawakufanya uhalifu.
  • 5:39 - 5:40
    Kisha niligundua
  • 5:41 - 5:43
    kulingana takwimu ya MarketWatch,
  • 5:43 - 5:45
    zaidi ya asilimia 60 ya wakazi wa Marekani
  • 5:45 - 5:47
    wana chini ya Dola 1,000 katika akiba.
  • 5:48 - 5:51
    Michezo ilielezea kwamba zaidi ya asilimia 60 ya wachezaji wa NBA
  • 5:51 - 5:53
    na wachezaji wa NFL hufilisika.
  • 5:53 - 5:56
    Asilimia 40 ya matatizo ya ndoa
    hutokana na masuala ya kifedha.
  • 5:57 - 5:58
    Balaa gani?
  • 5:58 - 6:00
    (Kicheko)
  • 6:00 - 6:03
    Unataka kuniambia,
    watu wamefanya kazi maisha yao yote,
  • 6:03 - 6:06
    wakinunua magari, nguo, nyumba
    na vitu mbalimbali
  • 6:06 - 6:08
    lakini walikuwa waliishi hundi kwa hundi?
  • 6:08 - 6:12
    Ni namna gani duniani wanajamii
    wangekwenda kuwasaidia wafungwa
  • 6:12 - 6:14
    kurudi kwenye jamii
  • 6:14 - 6:16
    ikiwa hawakuweza kusimamia
    mambo yao wenyewe?
  • 6:16 - 6:17
    Tumevurugwa.
  • 6:17 - 6:19
    (Kicheko)
  • 6:19 - 6:21
    Nahitaji mpango mzuri zaidi.
  • 6:23 - 6:25
    Hii haitakwenda kufanya kazi vizuri.
  • 6:25 - 6:26
    Hivyo ...
  • 6:28 - 6:29
    Nilifikiria.
  • 6:32 - 6:35
    Sasa nilikuwa na wajibu kukutana
    na wale waliokuwa kwenye mkondo huo
  • 6:36 - 6:38
    na kuwasaidia,
  • 6:38 - 6:41
    na ilikuwa ni ajabu sababu
    sasa nilijali jumuiya yangu
  • 6:41 - 6:43
    Lo, hebu fikiria.
    Nilijali kuhusu jumuiya yangu.
  • 6:45 - 6:47
    Ujinga juu ya Fedha ni ugonjwa
  • 6:47 - 6:50
    ambao umedhohofisha wachache
    na walio chini katika jamii yetu
  • 6:50 - 6:52
    kwa vizazi na vizazi,
  • 6:52 - 6:55
    na tunapaswa kukasirika juu ya hilo.
  • 6:55 - 6:56
    Ebu jiulize:
  • 6:56 - 7:00
    Inawezekanaje asilimia 50
    ya wakazi wa Marekani
  • 7:00 - 7:04
    wasiwe na elimu ya fedha katika nchi
    inayoendeshwa kwa ustawi wa kifedha?
  • 7:05 - 7:08
    Kupatikana kwa haki kwetu,
    hadhi yetu ya kijamii,
  • 7:08 - 7:11
    hali ya maisha, usafirishaji na chakula
  • 7:11 - 7:14
    vyote vinategemea fedha
    ambayo watu wengi hawawezi kuisimamia.
  • 7:14 - 7:16
    Ni ajabu!
  • 7:16 - 7:17
    Ni janga
  • 7:17 - 7:20
    na hatari kubwa kwa usalama wa umma
    kuliko suala jingine lolote.
  • 7:22 - 7:24
    Kadiri ya
    Kitengo cha Urekebishaji cha Kalifornia,
  • 7:24 - 7:27
    zaidi ya asilimia 70 ya wale waliofungwa
  • 7:27 - 7:30
    wamefanya au wameshtakiwa kwa uhalifu
    uhusianao na fedha:
  • 7:30 - 7:35
    wizi wa kutumia nguvu, kuvunja nyumba,
    kutapeli, uporaji, ghusubu --
  • 7:36 - 7:37
    na orodha inaendelea.
  • 7:38 - 7:39
    Angalia hii:
  • 7:39 - 7:42
    Mfungwa wa kawaida
  • 7:42 - 7:45
    huingia katika mfumo wa gereza
    wa Kalifornia
  • 7:45 - 7:46
    pasipo kuwa na elimu ya fedha,
  • 7:47 - 7:49
    hupata ujira wa senti 30 kwa saa,
  • 7:49 - 7:51
    zaidi ya Dola 800 kwa mwaka,
  • 7:51 - 7:54
    bila ya kuwa na matumizi yoyote
    na kuweka akiba yoyote.
  • 7:55 - 7:59
    Anapopewa msamaha,
    hupewa dola 200 pesa ya geti na kuambiwa,
  • 7:59 - 8:02
    "Wee, mafanikio mema, kaa mbali na
    matatizo. Usirudi gerezani tena."
  • 8:03 - 8:06
    Bila kuwa na maandalizi yoyote ya maana
    au mpango fedha wa muda mrefu,
  • 8:06 - 8:07
    anafanyaje ...?
  • 8:09 - 8:10
    Akiwa na miaka 60?
  • 8:11 - 8:12
    Apate kazi nzuri,
  • 8:12 - 8:16
    au arudi kwenye tabia ile ile ya uhalifu
    iliyompeleka gerezani kwanza?
  • 8:17 - 8:19
    Nyinyi walipakodi, chagueni wenyewe.
  • 8:19 - 8:22
    Hakika, elimu yake
    imeshamchagulia, pengine.
  • 8:23 - 8:25
    Kwa hiyo, tunatibuje ugonjwa huu?
  • 8:26 - 8:28
    Nilishiriki kuanzisha programu
  • 8:28 - 8:33
    tuliyoiita Elimu Hisia
    ya Uwezeshaji wa Kifedha
  • 8:33 - 8:34
    tunaiita FEEL
  • 8:34 - 8:37
    na inafundisha namna ya kutenganisha
    maamuzi ya kihisia
  • 8:37 - 8:39
    na maamuzi ya kifedha,
  • 8:39 - 8:43
    na sheria 4 aushi
    za utawala fedha binafsi:
  • 8:43 - 8:44
    njia sahihi ya kuweka akiba,
  • 8:46 - 8:47
    kudhibiti gharama zako za maisha,
  • 8:48 - 8:50
    kukopa fedha kwenye ufanisi
  • 8:50 - 8:54
    kutawanya fedha yako
    kuruhusu fedha yako ikufanyie kazi
  • 8:54 - 8:56
    badala ya wewe kuifanyia kazi.
  • 8:56 - 9:00
    Wafungwa wanahitaji ujuzi huu
    kabla ya kuingia tena kwenye jamii.
  • 9:01 - 9:05
    Hatuwezi kubadilika kuwa na maisha
    ya kawaida bila ujuzi huu wa maisha.
  • 9:05 - 9:09
    Hii dhana kuwa ni Weledi tu
    wanaweza kuwekeza na kusimamia fedha
  • 9:09 - 9:11
    ni ya fedheha kabisa,
  • 9:12 - 9:14
    na yeyote aliyewaambia hivyo anadanganya.
  • 9:14 - 9:18
    (Makofi na Vifijo)
  • 9:18 - 9:21
    Mweledi ni mtu
  • 9:21 - 9:23
    anayejua kazi zake kuliko walio wengi,
  • 9:23 - 9:28
    na hakuna mtu ajuaye kiasi gani cha fedha
    wahitaji, unacho, au wataka zaidi ya wewe,
  • 9:28 - 9:30
    ikimaanisha kuwa wewe ni mweledi.
  • 9:31 - 9:35
    Elimu ya fedha siyo stadi,
    mabibi na mabwana.
  • 9:35 - 9:36
    Ni mtindo wa maisha.
  • 9:38 - 9:42
    Uimara wa kifedha ni matokeo ya ziada
    ya mtindo sahihi wa maisha.
  • 9:42 - 9:46
    Mfungwa mwenye elimu nzuri ya kifedha
    anaweza kuwa mwananchi mlipakodi,
  • 9:47 - 9:50
    na mwananchi mlipakodi mwenye elimu
    nzuri ya kifedha anaweza kubaki hivyo.
  • 9:50 - 9:55
    Hii inatuwezesha kuunda daraja
    kati ya wale watu tunaowashawishi:
  • 9:55 - 9:57
    familia, marafiki na wale vijana
  • 9:57 - 10:00
    ambao bado wanaamini
    kuwa uhalifu na pesa vina uhusiano.
  • 10:02 - 10:05
    Kwa hiyo tupoteze uwoga na wasiwasi
  • 10:05 - 10:06
    wa maneno makubwa ya kifedha
  • 10:06 - 10:10
    na ujinga mwingine wote
    ambao mmekuwa mkisikia huko nje.
  • 10:10 - 10:14
    Na tujikite kwenye kiini
    kilichokuwa kinadhoofisha jamii yetu
  • 10:14 - 10:18
    kuanzia kutimiza wajibu wako
    la kuwa meneja mzuri wa maisha.
  • 10:19 - 10:22
    Na tutoe mtaala mwepesi na rahisi kutumia
  • 10:22 - 10:25
    ambao utaingia kwenye kiini, kiini
  • 10:25 - 10:29
    cha ni nini ukweli wa
    uwezeshaji wa kifedha na elimu ya hisia.
  • 10:29 - 10:31
    Sasa, ikiwa umekaa hapa kwa wasikilizaji
    na umesema,
  • 10:32 - 10:34
    "Ndiyo, kweli, hiyo si mimi
    na sikubaliani nayo,"
  • 10:34 - 10:35
    basi njoo uchukue somo langu --
  • 10:35 - 10:37
    (Kicheko)
  • 10:37 - 10:41
    ili nikuoneshe ni kiasi gani cha pesa
    inakugharimu kila unaposhikwa na hisia.
  • 10:42 - 10:45
    (Makofi na Vifijo)
  • 10:48 - 10:49
    Asanteni sana. Asanteni.
  • 10:49 - 10:50
    (Makofi na Vifijo)
Title:
Jinsi nilivyojifunza kusoma --na biashara ya hisa -- gerezani
Speaker:
Curtis 'Wall Street' Carroll
Description:

Elimu ya fedha siyo stadi -- ni mtindo wa maisha. Chukua hiyo kutoka kwa Curtis "Wall Street" Carroll. Kama mfungwa, Carroll anajua nguvu ya dola(fedha). Akiwa gerezani, alijifunza jinsi ya kusoma na kufanya biashara ya hisa, na sasa anashirikisha ujumbe rahisi, na wenye nguvu: wote tuhanitaji kuwa werevu na pesa zetu.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
10:50

Swahili subtitles

Revisions