Kilio cha shujaa dhidi ya ndoa za utotoni
-
0:01 - 0:03Nitaanza leo
-
0:03 - 0:05kwa kuigawana shairi
-
0:05 - 0:08iliyoandikiwa na rafiki yangu mmalawi,
-
0:08 - 0:10Eileen Piri.
-
0:10 - 0:14Eileen ana miaka 13 tu,
-
0:14 - 0:19lakini tulipoangalia diwani ya ushairi tuliyoandika,
-
0:19 - 0:22Niliona shairi yake ilinivuta sana,
-
0:22 - 0:24ilitia motisha sana.
-
0:24 - 0:26Basi nitakusomeeni.
-
0:27 - 0:31Ameiita shairi yake
"Nitaolewa ninapotaka" -
0:31 - 0:33(Kicheko)
-
0:33 - 0:36"Nitaolewa ninapotaka.
-
0:36 - 0:41Mama yangu hatonilazimisha kuolewa.
-
0:41 - 0:44Baba yangu hatonilazimisha kuolewa.
-
0:46 - 0:48Mjomba, Shangazi,
-
0:48 - 0:51Kaka au dada,
-
0:51 - 0:53Hawawezi kunilazimisha.
-
0:54 - 0:56Hakuna mtu duniani
-
0:56 - 1:00awezaye kunilazimisha kuolewa.
-
1:00 - 1:02Nitaolewa ninapotaka.
-
1:02 - 1:05Hata ukinipiga,
-
1:05 - 1:08hata ukinifukuza
-
1:08 - 1:11hata ukinifanya vibaya,
-
1:11 - 1:14Nitaolewa ninapotaka.
-
1:14 - 1:17Nitaolewa ninapotaka,
-
1:17 - 1:21lakini sio kabla sijapata elimu nzuri
-
1:21 - 1:25na sio kabla sijakua mtu mzima
-
1:25 - 1:28Nitaolewa ninapotaka."
-
1:29 - 1:32Shairi inaonekana isiyo ya kawaida
-
1:32 - 1:35kuandikwa na msichana wa miaka 13,
-
1:35 - 1:40lakini tunapotoka mimi na Eileen,
-
1:40 - 1:44shairi hiyo, niliyoikusomeeni,
-
1:44 - 1:48ni sauti ya shujaa.
-
1:48 - 1:51Ninatoka Malawi.
-
1:51 - 1:55Malawi ni nchi ya maskini,
-
1:55 - 1:58maskini sana,
-
1:58 - 2:03ambapo usawa wa kijinsi sio hakika.
-
2:03 - 2:05Kukua katika nchi ile,
-
2:05 - 2:08Sikuweza kujichagulia katika maisha.
-
2:08 - 2:10Sikuweza hata kuzichungua
-
2:10 - 2:13nafasi za kibinafsi katika maisha yangu.
-
2:13 - 2:16Nitakuambieni hadithi
-
2:16 - 2:18ya wasichana wawili tofauti,
-
2:18 - 2:22wasichana wawili warembo.
-
2:22 - 2:25Hawa wasichana walikua
-
2:25 - 2:27chini ya paa moja.
-
2:27 - 2:29Walikula chakula sawa sawa.
-
2:29 - 2:32Wakati wengine, wangezigawana nguo,
-
2:32 - 2:35na hata viatu.
-
2:35 - 2:40Lakini maisha zao ziliishia tofauti,
-
2:40 - 2:42kwa njia mbili tofauti.
-
2:43 - 2:47Yule msichana mwengine ni dada yangu mdogo.
-
2:47 - 2:52Dada yangu alikuwa na miaka 11
-
2:52 - 2:54alipopata mimba.
-
2:56 - 3:00Ni jambo la kuumiza.
-
3:01 - 3:05Si kama ilimwumiza pekee, lakini mimi pia.
-
3:05 - 3:08Nilikuwa na wakati wa tafrani pia.
-
3:08 - 3:12Kwa sasa katika utamaduni wangu,
-
3:12 - 3:15ukifika ubalehe,
-
3:15 - 3:19inabidi uende makambi ya kuanzisha.
-
3:19 - 3:21Katika makambi haya,
-
3:21 - 3:25unafundishwa vipi umfurahishe mwanamume kwa kijinsia.
-
3:25 - 3:27Kuna siku maalum,
-
3:27 - 3:30wanayoiita "Siku maalum sana"
-
3:30 - 3:33ambapo mwanamume anaajiriwa na jamii
-
3:33 - 3:35anakuja kambini
-
3:35 - 3:38na anafanya mapenzi na watoto wadogo.
-
3:39 - 3:42Wazeni kiwewe wasichana hawa
-
3:42 - 3:45wanachokisikia kila siku.
-
3:47 - 3:50Wasichana wengi wanapata mimba.
-
3:50 - 3:53Na hata wanashikwa na ukimwi
-
3:53 - 3:55na magonjwa mengine ya zinaa.
-
3:56 - 4:01Kwa dadangu mdogo,
alipata mimba. -
4:01 - 4:05Leo, ana miaka 16
-
4:05 - 4:08na ana watoto watatu.
-
4:08 - 4:11Ndoa yake ya kwanza haijaishi,
-
4:11 - 4:15wala ndoa yake ya pili.
-
4:15 - 4:19Kwa upande wengine, kuna msichana huyo.
-
4:19 - 4:21Anashangaza.
-
4:21 - 4:23(Kicheko)
-
4:23 - 4:26(Makofi)
-
4:28 - 4:30Nasema anashangaza kwa sababu ni kweli.
-
4:30 - 4:33Ni zaidi ya mzuri.
-
4:33 - 4:37Msichana yule ni mimi. (Kicheko)
-
4:37 - 4:40Nilipokuwa na miaka 13,
-
4:40 - 4:43Niliambiwa, umekua mzima,
-
4:43 - 4:46sasa umebalehe,
-
4:46 - 4:50inadhaniwa uende kambi la kuanzisha.
-
4:50 - 4:53Nilisema, "Nini?
-
4:53 - 4:57Siendi kwa yale makambi ya kuanzisha."
-
4:58 - 5:01Unajua nini mwanamke yule aliniambia?
-
5:01 - 5:05"Wewe ni mpumbavu. Mkaidi.
-
5:05 - 5:12Huziheshimu desturi za jamii yetu, za jumuia yetu."
-
5:12 - 5:16Nilikataa kwa sababu nilijua wapi nilipokwenda.
-
5:16 - 5:18Nilijua nilivyotaka katika maisha yangu.
-
5:20 - 5:23Nilikuwa na matumaini mengi nilipokuwa mtoto.
-
5:24 - 5:28Nilitaka kupata elimu nzuri
-
5:28 - 5:30Kutafuta kazi nzuri wakati wa badae.
-
5:30 - 5:32Nilikuwa najifikiria kama mwanasheria,
-
5:32 - 5:35kukaa katika kiti kile kikubwa.
-
5:35 - 5:37Yale yalikuwa mawazo
-
5:37 - 5:40yaliokuwa katika akili yangu kila siku.
-
5:40 - 5:42Na nilijua kwamba siku moja
-
5:42 - 5:47Ningesaidia kupa kitu,
kitu kidogo kwa jumuia yangu. -
5:47 - 5:49Lakini kila siku baada ya kukataa,
-
5:49 - 5:51wanawake wangeniambia,
-
5:51 - 5:55"Jitazama, umekua mtu mzima.
Dadako mdogo amepata mtoto. -
5:55 - 5:56Vipi wewe?"
-
5:56 - 6:01Ile ilikuwa muziki
niliyoisikia kila siku, -
6:01 - 6:05na ile ni muziki
wasichana wanayoisikia kila siku -
6:05 - 6:09wasipolifanya jambo
ambalo jumuia inawatakia wafanye. -
6:12 - 6:15Nilipozilinganisha hadithi hizo mbili
kati ya mimi na dadangu, -
6:15 - 6:20Nilisema, "Mbona nisiweze kufanya kitu?"
-
6:20 - 6:25Kwa nini nisiweze kubadilisha jambo
lililotokea kwa muda mrefu -
6:25 - 6:28katika jamii yetu?"
-
6:28 - 6:30Wakati ule niliwaita wasichana wengine
-
6:30 - 6:33kama dadangu, ambao wamepata watoto,
-
6:33 - 6:36waliokwenda darasani lakini
wamesahau kusoma na kuandika. -
6:36 - 6:38Nilisema "Njoo, tukumbushane
-
6:38 - 6:40je kusoma na kuandika tena,
-
6:40 - 6:44kuikamata kalamu vipi,
kusomaje, kuzuia kitabu." -
6:44 - 6:48Ilikuwa wakati nzuri sana nao.
-
6:48 - 6:52Sio kwamba nilifundishwa kidogo kuhusu wale,
-
6:52 - 6:56lakini pia waliweza kuniambia
hadithi zao za kibinafsi, -
6:56 - 6:57waliyokabiliana kila siku
-
6:57 - 7:00kama mama wadogo.
-
7:00 - 7:02Wakati ule nilidhani,
-
7:02 - 7:06"Kwa nini tusiweze kuangalia mambo hayo
yanayotuathiri -
7:06 - 7:10na kuyaonesha na kuwaambia mama zao,
viongozi wetu wa jadi, -
7:10 - 7:12kwamba mambo hayo ni maovu?"
-
7:12 - 7:14Ilikuwa jambo la hofu,
-
7:14 - 7:16kwa sababu viongozi hawa wa jadi,
-
7:16 - 7:18wameshayazoea mambo
-
7:18 - 7:21yaliyokuwepo kwa muda mrefu.
-
7:21 - 7:22Ni jambo ambalo ni ngumu kubadilisha,
-
7:22 - 7:25lakini nzuri kujitahidi.
-
7:25 - 7:27Kwa hiyo tulijitahidi.
-
7:27 - 7:30Ilikuwa ngumu sana, lakini tulivumulia.
-
7:30 - 7:33Na mimi nipo kwa kusema kwamba katika jumuia yangu,
-
7:33 - 7:36ilikuwa jumuia ya kwanza baada ya wasichana
-
7:36 - 7:39walijitahidi sana kumthibitishia kiongozi wa jadi wetu,
-
7:39 - 7:43na kiongozi wetu alitutetea
na akasema hakuna msichana
alazimishwaye kuolewa -
7:43 - 7:46kabla hajafika miaka 18.
-
7:46 - 7:50(Makofi)
-
7:54 - 7:55Katika jumuia yangu
-
7:55 - 7:58Ilikuwa mara ya kwanza kwa jumuia,
-
7:58 - 8:00ilibidi watazame sheria ndogo,
-
8:00 - 8:04ya kwanza iliyowalinda wasichana
-
8:04 - 8:06katika jumuia yetu.
-
8:06 - 8:08Hatukumaliza na hivyo.
-
8:08 - 8:11Tuliendelea.
-
8:11 - 8:15Tulikusudia kuwapigania wasichana
sio katika jamii yangu tu -
8:15 - 8:17lakini kwenye jamii nyingine.
-
8:17 - 8:22Wakati muswada wa ndoa za watoto
iliwasilishwa mwezi wa pili -
8:22 - 8:25tulikuwepo kwenye mahakama ya bunge.
-
8:25 - 8:29Kila siku, wakati wabunge
walipoingia, -
8:29 - 8:32tulikuwa tukiwaambia,
"Tafadhali uitegemee muswada hii?" -
8:32 - 8:37Na hatuna
teknolojia nyingi kama huku, -
8:37 - 8:39lakini tunazo simu zetu ndogo.
-
8:39 - 8:44Kwa hiyo tulisema, "Mbona tusiweze kupata
namba zao na kuwatumia text?" -
8:44 - 8:47Kwa hiyo tulifanya hivyo.
Na ilikuwa jambo zuri -
8:47 - 8:49(Makofi)
-
8:49 - 8:52Kwa hiyo muswada ilipokubalika,
tuliwajibia na text, -
8:52 - 8:55"Asante kwa kutegemea muswada."
-
8:55 - 8:56(Kicheko)
-
8:56 - 8:59Na muswada iliposajilika
na Rais, -
8:59 - 9:03kwa kuifanya kuwa sheria, ilikuwa ziada.
-
9:03 - 9:08Sasa, katika Malawi, miaka 18 ni umri wa
kisheria kuolewa, kutoka 15 hadi 18. -
9:08 - 9:12(Makofi)
-
9:14 - 9:18Ni jambo zuri kulijua
kwamba muswada imakubalika, -
9:18 - 9:21lakini nikuambieni:
-
9:21 - 9:26Kuna nchi ambako miaka 18
ni umri wa kisheria kuolewa, -
9:26 - 9:30lakini sio tunasikia kilio
za wanawake na wasichana kila siku? -
9:30 - 9:35Kila siku, maisha ya wasichana
yanashuka thamani. -
9:35 - 9:42Ni wakati muhimu kwa viongozi waiheshimu ahadi yao.
-
9:42 - 9:44Kwa kuiheshimu ahadi hiyo,
-
9:44 - 9:50inamaanisha kuyaweka maswala ya wasichana
moyoni kila mara. -
9:50 - 9:54Tusitiishiwe kama duni,
-
9:54 - 9:58lakini wajue kwamba wanawake,
kama sisi chumbani humu, -
9:58 - 10:01sisi sio wanawake tu,
sisi sio wasichana tu, -
10:01 - 10:03sisi ni wa ajabu.
-
10:03 - 10:05Tunaweza kufanya zaidi.
-
10:05 - 10:08Na kitu chengine kwa Malawi,
-
10:08 - 10:11na si kwa Malawi pekee lakini nchi nyingine pia:
-
10:11 - 10:15Sheria zinazowepo,
-
10:15 - 10:20mnajua sheria sio sheria
mpaka inatekeleza? -
10:20 - 10:24Sheria iliyokubalika juzi
-
10:24 - 10:26na sheria ambazo katika nchi nyingine
zimekuwepo, -
10:26 - 10:30zinahitajika kutangazwa
kwa njia za kienyeji, -
10:30 - 10:33katika jamii,
-
10:33 - 10:38ambako maswala ya wasichana yako wazi.
-
10:38 - 10:43Wasichana wanakabiliana na maswala,
maswala magumu, katika jamii zao kila siku. -
10:43 - 10:48Kwa hiyo ikiwa wajue kwamba
kuna sheria ziwalindazo, -
10:48 - 10:51wataweza kusimama
na kujilinda -
10:51 - 10:55kwa sababu watajua kwamba
kuna sheria ziwalindazo. -
10:57 - 11:01Na kitu chengine nisemacho ni kwamba
-
11:01 - 11:06sauti za wasichana na wanawake
-
11:06 - 11:09ni nzuri sana, na zipo,
-
11:09 - 11:12lakini hatuwezi kufanya peke yetu.
-
11:12 - 11:15watetezi wa kiume, washirikiana,
-
11:15 - 11:17wajihusishe na tufanye kazi pamoja.
-
11:17 - 11:19ni kazi ya umoja.
-
11:19 - 11:22Tunavyohitaji ni vile vihitajikavyo
na wasichana wa sehemu zote: -
11:22 - 11:28elimu nzuri, na juu ya yote,
ni kutoolewa wakiwa na miaka 11. -
11:30 - 11:33Na zaidi ya hayo,
-
11:33 - 11:36Najua kwamba pamoja,
-
11:36 - 11:40tunaweza kubadilisha mifumo ya kisheria,
-
11:40 - 11:43kiutamaduni na kisiasa
-
11:43 - 11:48inayozikanusha haki za wasichana.
-
11:48 - 11:53Nasimama hapa leo
-
11:53 - 12:00na kutangaza kwamba tunaweza
kuisha ndoa za watoto katika kizazi kimoja. -
12:01 - 12:03Sasa ni wakati
-
12:03 - 12:07ambapo msichana na msichana,
na millioni za wasichana duniani, -
12:07 - 12:10wataweza kusema,
-
12:10 - 12:13"Nitolewa ninapotaka."
-
12:13 - 12:16(Makofi)
-
12:23 - 12:25Asante. (Makofi)
- Title:
- Kilio cha shujaa dhidi ya ndoa za utotoni
- Speaker:
- Memory Banda
- Description:
-
Maisha ya Memory Banda yalichukua njia ya tofauti na maisha ya dada yake. Dada yake alipovunja ungo, alipelekwa katika kambi ya awali ambayo inafundisha wasichana "jinsi ya kumridhisha mwanaume kimapenzi" Akapata uja uzito huko - akiwa na umri wa miaka 11. Lakini Banda akakataa kwenda. Badala yake , akaandaa wengine na akamuomba kiongozi wa jamii yake kupitisha sheria ndogo inayozuia wasichana kulazimishwa kuolewa kabla ya kufikisha miaka 18. Akaendeleza mapambano haya mpaka katika ngazi ya kitaifa ... akipata matokeo ya ajabu sana kwa wasichana wote , katika nchi yote ya Malawi.
- Video Language:
- English
- Team:
- closed TED
- Project:
- TEDTalks
- Duration:
- 12:38
Joachim Mangilima approved Swahili subtitles for A warrior’s cry against child marriage | ||
Joachim Mangilima accepted Swahili subtitles for A warrior’s cry against child marriage | ||
Joachim Mangilima edited Swahili subtitles for A warrior’s cry against child marriage | ||
Louise Joanne edited Swahili subtitles for A warrior’s cry against child marriage | ||
Louise Joanne edited Swahili subtitles for A warrior’s cry against child marriage | ||
Louise Joanne edited Swahili subtitles for A warrior’s cry against child marriage | ||
Louise Joanne edited Swahili subtitles for A warrior’s cry against child marriage | ||
Louise Joanne edited Swahili subtitles for A warrior’s cry against child marriage |