Hadithi nne tunazoambia nafsi zetu kuhusu kifo
-
0:00 - 0:02Nina swali:
-
0:02 - 0:06Ni wakina nani hapa walishawahi tambua lini
-
0:06 - 0:09watakufa?
-
0:09 - 0:12Natambua.Nilikuwa mvulana mdogo,
-
0:12 - 0:15na babu yangu alikuwa amefariki,
-
0:15 - 0:19na nakumbuka siku chache baadaye nikiwa nimelala kitandani wakati wa usiku
-
0:19 - 0:22nikijaribu kujiuliza kipi kilichotokea.
-
0:22 - 0:25Ilimaanisha nini kwamba amekufa?
-
0:25 - 0:27Atakuwa ameenda wapi?
-
0:27 - 0:30Ilikuwa ni kama shimo limefunguka
-
0:30 - 0:32na likammeza.
-
0:32 - 0:35Na swali la kushtua likanijia:
-
0:35 - 0:38Kama amekufa,inaweza ikanitokea na mimi?
-
0:38 - 0:42Hilo shimo litafunguka na kunimeza?
-
0:42 - 0:44Litafunguka chini ya kitanda changu
-
0:44 - 0:47na kunimeza wakati nimelala?
-
0:47 - 0:51Katika namna fulani,watoto wote wanakuja gundua kuhusu kifo.
-
0:51 - 0:53Kinaweza kutokea katika njia nyingi tofauti,
-
0:53 - 0:55na kawaida huja kwa hatua.
-
0:55 - 0:58Mawazo yetu kuhusu kifo yanakua kadiri tunavyozidi kuzeeka.
-
0:58 - 1:01Na kama ukifika katika kona za giza
-
1:01 - 1:03za kumbukumbu yako,
-
1:03 - 1:06utakumbuka kitu fulani kama nilichohisi mimi
-
1:06 - 1:09wakati babu yangu alipofariki na nilipogundua
-
1:09 - 1:11inaweza kunitokea na mimi pia,
-
1:11 - 1:13hiyo maana iliyopo nyuma ya haya yote
-
1:13 - 1:17ubatili unangojea.
-
1:17 - 1:19Na haya maendeleo katika utoto
-
1:19 - 1:22yanaakisi maendeleo ya aina yetu.
-
1:22 - 1:25Kama kulivyokuwa na alama katika maendeleo yako
-
1:25 - 1:29kama mtoto wakati utambuzi wako wa nafsi na muda
-
1:29 - 1:31ulivyokuja kuchanganyika vya kutosha
-
1:31 - 1:35kiasi cha wewe kutambua haitaishi milele,
-
1:35 - 1:38kwa hiyo katika hali fulani ya mabadiliko yetu,
-
1:38 - 1:41baadhi ya utambuzi wa binadamu wa nafsi na muda
-
1:41 - 1:44ukaja jichanganya vya kutosha.
-
1:44 - 1:47kwa wao kuja kuwa binadamu wa kwanza kutambua,
-
1:47 - 1:50"naelekea kufa"
-
1:50 - 1:52Kama unapenda,laana yetu.
-
1:52 - 1:56Ni gharama tunayolipa kwa kuwa werevu wajinga.
-
1:56 - 1:59Tunatakiwa kuishi katika maarifa
-
1:59 - 2:01hicho ni kitu kibaya kinachoweza kutokea
-
2:01 - 2:03siku moja kwa uhakika,
-
2:03 - 2:04mwisho wa miradi yetu,
-
2:04 - 2:08matumaini yetu,ndoto zetu,katika dunia ya kila mmoja.
-
2:08 - 2:11Tunaishi katika kivuli cha
-
2:11 - 2:13kuwaza mwisho wa dunia.
-
2:13 - 2:16Na inaogopesha.Na kutisha.
-
2:16 - 2:18Kwa hiyo tunatafuta njia ya kujinasua.
-
2:18 - 2:21Kwa upande wangu,nilipokuwa na miaka mitano,
-
2:21 - 2:24hii ilimaanisha kumuuliza mama yangu.
-
2:24 - 2:27Sasa nilipoanza kuuliza
-
2:27 - 2:29kipi kinatokea tukifarikia,
-
2:29 - 2:31watu wazima waliokuwa wananizunguka wakati huo
-
2:31 - 2:34walijibu katika mchanganyiko wa kiingereza na ulio mgumu kuelewa.
-
2:34 - 2:37na mkristo mwenye nusu moyo,
-
2:37 - 2:39na kipande cha sentensi ninachosikia mara nyingi
-
2:39 - 2:40ilikuwa kwamba babu kwa sasa
-
2:40 - 2:43"yuko juu akituangalia sisi"
-
2:43 - 2:46na kama nikifa pia,
-
2:46 - 2:49na mimi pia nitaenda juu,
-
2:49 - 2:51hiki kinafanya kifo kionekane kama
-
2:51 - 2:53lifti isiyoonekana kwa macho lakini inafanya kazi.
-
2:53 - 2:56Lakini hii haikuonekana kama ina ukweli sana.
-
2:56 - 2:59Nilizoea kuangalia habari za watoto wakati huo,
-
2:59 - 3:02na huu ulikuwa wakati wa kujifunza kuhusu unajimu.
-
3:02 - 3:04Kulikuwa na roketi zinakwenda juu angani,
-
3:04 - 3:07zinakwenda huko.
-
3:07 - 3:09Hamna mnajimu ambaye alirudi
-
3:09 - 3:12na akasema kwamba amekutana na babu yangu
-
3:12 - 3:15au mtu yoyote aliyekufa.
-
3:15 - 3:16Lakini nilikuwa naogopa,
-
3:16 - 3:18wazo la kupanda lifti ya kifo
-
3:18 - 3:20kumuona babu yangu
-
3:20 - 3:21naona ni bora zaidi kuliko kwenda kumezwa
-
3:21 - 3:24wakati nimelala.
-
3:24 - 3:27na nikaamini,
-
3:27 - 3:29pamoja haikuleta maana sana.
-
3:29 - 3:32Na hili wazo nililokuwa nalo
-
3:32 - 3:34wakati nikiwa mtoto,nimekuwa nalo kwa muda sana
-
3:34 - 3:36hadi nikiwa mtu mzima,
-
3:36 - 3:38ni zao ambalo wanasaikolojia wanaita
-
3:38 - 3:40upendeleo.
-
3:40 - 3:43Sasa upendeleo ni njia ambayo
-
3:43 - 3:45hufanya vitu kimakosa,
-
3:45 - 3:48njia ambazo tunakosea kukokotoa,kutoa maamuzi,
-
3:48 - 3:51kuharibu uhalisia,au kuona tunachotaka kuona,
-
3:51 - 3:53na upendeleo ninaoongelea
-
3:53 - 3:55unafanya kazi kama hivi:
-
3:55 - 3:57Kumfata mtu na ukweli
-
3:57 - 3:59kwamba atakufa
-
3:59 - 4:02na wataamini kuhusu hadithi yoyote
-
4:02 - 4:04ambayo inawaambia sio kweli
-
4:04 - 4:06na badala yake,wanaweza kuishi milele,
-
4:06 - 4:10hata kama inamaanisha watapanda lifti.
-
4:10 - 4:14Sasa tunaweza kuona huu ni upendeleo kupita wote.
-
4:14 - 4:17Imeelezew katika zaidi ya masomo 400
-
4:17 - 4:19ya undani.
-
4:19 - 4:22masomo haya ni ya werevu,lakini ni rahisi.
-
4:22 - 4:23Yanafanya kazi kama hivi.
-
4:23 - 4:25Unachukua makundi mawili ya watu
-
4:25 - 4:28ambao wako sawasawa katika kila kitu,
-
4:28 - 4:30na unawaambia kundi moja kwamba watafariki
-
4:30 - 4:33wengine huwaambii,unalinganisha tabia zao.
-
4:33 - 4:37Kwa hiyo unaangalia jinsi gani unafanya tabia zao kuwa
-
4:37 - 4:41watu wanapoanza kugundua kuhusu vifo vyao.
-
4:41 - 4:44Na kila wakati,unapata matokeo yaleyale:
-
4:44 - 4:47Watu ambao tayari washatambua kuhusu vifo vyao
-
4:47 - 4:49wako tayari kuamini hadithi
-
4:49 - 4:51ambazo zinawaambia wanaweza kukwepa kifo
-
4:51 - 4:52na kuishi milele.
-
4:52 - 4:55Huu ni mfano:Tafiti moja ya hivi karibuni
-
4:55 - 4:57ilichukua makundi mawili ya wapagani,
-
4:57 - 4:59hao ni watu ambao hawana maamuzi
-
4:59 - 5:02katika kuamini dini.
-
5:02 - 5:05Sasa,kundi moja liliambiwa kufikiria kuhusu kufa.
-
5:05 - 5:07Kundi lingine likaambiwa kufikiria kuhusu
-
5:07 - 5:09kuwa mpweke.
-
5:09 - 5:11Waliulizwa tena kuhusu imani zao za kidini.
-
5:11 - 5:14Wale walioambiwa kufikiria kuhusu kifo
-
5:14 - 5:18walikuwa wakielezea mara mbili zaidi hisia zao
-
5:18 - 5:19kuhusu Mungu na Yesu.
-
5:19 - 5:21Mara mbili zaidi.
-
5:21 - 5:24Pamoja na kwamba wote walikuwa wapagani.
-
5:24 - 5:26Lakini weka uoga wa kifo ndani yao,
-
5:26 - 5:30watakimbila kwa Yesu.
-
5:30 - 5:33Sasa,hii inaonesha kwamba kuwakumbusha watu kuhusu kifo
-
5:33 - 5:36inawachochea kuamini,bila kujali ukweli,
-
5:36 - 5:38na sio kwa dini tu,
-
5:38 - 5:41katika imani yoyote ile
-
5:41 - 5:44ambayo inaeleza kifo katika njia tofauti tofauti,
-
5:44 - 5:46haijalishi kama inakuwa maarufu
-
5:46 - 5:47au kuwa na watoto
-
5:47 - 5:49au utaifa,
-
5:49 - 5:52ambayo inasema utaishi siku zote.
-
5:52 - 5:54Huu ni upendeleo uliotengeneza umbile
-
5:54 - 5:57na historia y binadamu.
-
5:57 - 5:59Sasa,fikra iliyopo katika upendeleo huu
-
5:59 - 6:01katika tafiti 400
-
6:01 - 6:03inaitwa fikra ya usimamizi wa uoga,
-
6:03 - 6:06na wazo ni rahisi.Ni hivi.
-
6:06 - 6:08Tunakuza mawazo yetu kuhusu dunia,
-
6:08 - 6:10hivyo,hadithi tunazoambia nafsi zetu
-
6:10 - 6:13kuhusu dunia na sehemu yetu
-
6:13 - 6:15ili kusaidia kusimamia
-
6:15 - 6:18hofu ya kifo.
-
6:18 - 6:20Na hizi hadithi za kifo
-
6:20 - 6:23zina maelfu ya shuhuda tofauti tofauti,
-
6:23 - 6:27lakini naamini nyuma ya utofauti uliopo
-
6:27 - 6:29kuna aina nne za muhimu
-
6:29 - 6:33ambazo hizi hadithi za vifo zinahusiana.
-
6:33 - 6:35Na tunaweza kuona zinajirudia
-
6:35 - 6:38katika historia,na utofauti mdogo sana
-
6:38 - 6:41kuakisi msamiati wa siku.
-
6:41 - 6:43Sasa nitatoa muhtasari wa hizi aina nne
-
6:43 - 6:45kuu za hadithi za kifo,
-
6:45 - 6:47na ninataka kujaribu kukuonesha maana
-
6:47 - 6:49ni jinsi gani vinaelezewa kwa kuirudia katika kila utamaduni
-
6:49 - 6:51au kizazi
-
6:51 - 6:53kwa kutumia msamiati wa siku.
-
6:53 - 6:56Sasa,hadithi ya kwanza ni rahisi sana.
-
6:56 - 6:58Tunataka kukwepa kifo,
-
6:58 - 7:00na ndoto ya kufanya hicho katika mwili huu
-
7:00 - 7:02katika hii dunia milele
-
7:02 - 7:05ni hadithi ya kwanza na rahisi ya kifo,
-
7:05 - 7:08na inaweza kuonekana isiyo na maana kwa mara ya kwanza,
-
7:08 - 7:12lakini kiukweli,karibia kila tamaduni katika historia ya binadamu
-
7:12 - 7:14ilikuwa na mzimu au kiongozi mkongwe
-
7:14 - 7:16wa kutupa maisha au kurudisha wazee katika ujana
-
7:16 - 7:19au kitu kinachotuahidi sisi kuendelea mbele
-
7:19 - 7:22milele.
-
7:22 - 7:24Wahenga wa Kimisri walikuwa na huo mzimu,
-
7:24 - 7:26Wahenga wa Babylon,wa India.
-
7:26 - 7:29Katika historia ya ulaya,tunawaona katika kazi ya wanakemia wa kizamani,
-
7:29 - 7:32na mpaka leo tunaamini,
-
7:32 - 7:35tunahdithia hizi hadithi kwa kutumia msamiati
-
7:35 - 7:36wa sayansi.
-
7:36 - 7:38Miaka 100 iliyopita,
-
7:38 - 7:40homoni zilikuwa zimegunduliwa,
-
7:40 - 7:41na watu wakatumaini kwamba matibabu ya homoni
-
7:41 - 7:44yatatibu uzee na magonjwa,
-
7:44 - 7:47na sasa tunaweka matumaini yetu katika kiini shina
-
7:47 - 7:49uhandisi wa gene,na teknolojia ya nano.
-
7:49 - 7:53Lakini wazo kwamba sayansi inaweza kuponya kifo
-
7:53 - 7:56liko sura moja mbele zaidi katika hadithi
-
7:56 - 7:58ya maajabu ya kuweza kuishi milele,
-
7:58 - 8:02hadithi ambayo ni ya zamani kama ulivyo ustaarabu.
-
8:02 - 8:05Lakini kuweka mawazo yote katika kufikiria kutafuta kuishi milele
-
8:05 - 8:06na kukaa wazima siku zote
-
8:06 - 8:08ni mkakati wenye hatari sana.
-
8:08 - 8:10Tukiangalia nyuma katika historia
-
8:10 - 8:13wale waliotafuta kuishi milele huko nyuma,
-
8:13 - 8:15kitu kimoja ambacho wote wanacho
-
8:15 - 8:18ni kwamba wote wameshakufa.
-
8:18 - 8:21Kwa hiyo tunahitaji mpango wa kutukomboa,na mpango huu mbadala
-
8:21 - 8:25ni ambao aina ya pili ya kifo inaelezea,
-
8:25 - 8:27ni kufufuka.
-
8:27 - 8:29Na hiyo inakuwa ni wazo kwamba mimi ni huu mwili,
-
8:29 - 8:31Ni kiumbe kamili.
-
8:31 - 8:33Kinakubali kwamba kitakufa
-
8:33 - 8:35lakini kinasema,pamoja na hilo,
-
8:35 - 8:37Ninaweza amka na nikaishi tena.
-
8:37 - 8:40Katika maneno mengine,naweza fanya kama alichofanya Yesu.
-
8:40 - 8:42Yesu alikufa,akakaa siku tatu kaburini,
-
8:42 - 8:45na baada ya hapo akafufuka na kuamka tena.
-
8:45 - 8:48Na wazo ambalo tunaishi nalo ni kwamba wote sisi tunaweza fufuka na kuishi tena
-
8:48 - 8:50hata waimani ya Orthodox wanaamini,si kwa wakristo tu
-
8:50 - 8:53hata Wayahudi na Waislamu.
-
8:53 - 8:55Lakini tamaa yetu katika kuamini hizi hadithi
-
8:55 - 8:57imefungamana kiundani sana
-
8:57 - 8:59kwamba tunaivumbua tena
-
8:59 - 9:01kwa enzi za kisayansi,
-
9:01 - 9:04kwa mfano,kwa kutumia wazo la kutumia mazingira ya joto dogo sana ili kuweza kutunza kiumbe kirudi katika uhai
-
9:04 - 9:05Wazo ni kwamba ukifa,
-
9:05 - 9:07unaweza kujigandisha mwenyewe,
-
9:07 - 9:10na baadaye,katika namna fulani teknolojia
-
9:10 - 9:11imekua vya kutosha,
-
9:11 - 9:13unaweza kutengenezwa na tena kurudi katika uhai
-
9:13 - 9:14kwa kufufuka.
-
9:14 - 9:17Na watu wanaamini Mungu wa nguvu zote
-
9:17 - 9:19atawafufua na wataishi tena,
-
9:19 - 9:23na wengine wanaamini wanasayansci wenye nguvu na maarifa watawafufua nao pia.
-
9:23 - 9:26Lakini kwa wengine,wazo zima ni kuhusu kufufuka,
-
9:26 - 9:28kwa kutoka nje ya kaburi,
-
9:28 - 9:30ni kama zile sinema z kutisha za zombies.
-
9:30 - 9:33Mwili unakuwa mchafu sana,usiotamanika
-
9:33 - 9:35kwa kuwezesha maisha ya milele,
-
9:35 - 9:39Watu wanaweka matumaini yao katika hili swala la tatu,
-
9:39 - 9:41hadithi ya kifo iliyokaa kiroho zaidi,
-
9:41 - 9:43wazo kwamba tutaiacha miili yetu nyuma
-
9:43 - 9:45na kuishi kama roho.
-
9:45 - 9:47Sasa,watu wengi katika dunia
-
9:47 - 9:49wanaamini wana roho,
-
9:49 - 9:51na wazo hili ni kuu kwa dini nyingi.
-
9:51 - 9:54Lakini hata hivyo,katika mfumo wa sasa,
-
9:54 - 9:56katika utamaduni wake,
-
9:56 - 9:58wazo la roho ni maarufu sana,
-
9:58 - 9:59achilia yote hayo tunakuja tena
-
9:59 - 10:01kuvumbua wazo hili katika nyakati za kidigitali,
-
10:01 - 10:03kwa mfano
-
10:03 - 10:05unaweza kuacha mwili wako nyuma
-
10:05 - 10:07kwa kuwezesha akili yako,uhalisia wako,
-
10:07 - 10:09wewe halisi,kwenye kompyuta,
-
10:09 - 10:14na kuishi kama avatar.
-
10:14 - 10:16Lakini kuna wabishi ambao wanasema
-
10:16 - 10:18tukiangalia katika ukweli wa sayansi,
-
10:18 - 10:19hasa sayansi ya mishipa ya fahamu,
-
10:19 - 10:21inadokeza kwamba,akili yako
-
10:21 - 10:23uhalisi wako,
-
10:23 - 10:25vinategemea sana upande fulani
-
10:25 - 10:27wa mwili wako,ambao ni ubongo.
-
10:27 - 10:30Na aho wenye wasiwasi wanaweza pata faraja
-
10:30 - 10:32katika aina ya nne ya hadithi ya kifo,
-
10:32 - 10:34na huo ni urithi,
-
10:34 - 10:36wazo kwamba unaweza ishi
-
10:36 - 10:38mpaka kwenye mwangi unaiacha dunia,
-
10:38 - 10:41kama mwanajeshi hodari wa Kigiriki Achilles,
-
10:41 - 10:43aliyetoa sadaka ya maisha yake kwa Troy
-
10:43 - 10:46ili kupata umaarufu wa kifo.
-
10:46 - 10:48Na umaarufu ulisambaa
-
10:48 - 10:51na ni maarufu kama ilivyokuwa zamani,
-
10:51 - 10:52na katika nyakati hizi za kidigitali,
-
10:52 - 10:54ni rahisi sana kufanikiwa.
-
10:54 - 10:56Huitaji kuwa kama mwanajeshi hodari kama Achilles
-
10:56 - 10:58au kuwa mfalme hodari au shujaa.
-
10:58 - 11:03Unachohitaji ni mtandao wa intaneti na paka anayefurahisha(Vicheko)
-
11:03 - 11:05Lakini watu wengi wanapendelea kuacha vile vionekanavyo,
-
11:05 - 11:08urithi wa kibiolojia--watoto,kwa mfano.
-
11:08 - 11:10Au wapo hivi,wana imani,kuishi
-
11:10 - 11:12katika nafasi ya maisha yote,
-
11:12 - 11:14taifa au familia au kabila,
-
11:14 - 11:17gene zao.
-
11:17 - 11:18Lakini tena,wanakuwa na wasiwasi
-
11:18 - 11:20wana wasiwasi kwamba urithi
-
11:20 - 11:22kiuhalisia ni kuhusu kifo.
-
11:22 - 11:24Kwa mfano,Woody Allen alisema,
-
11:24 - 11:27"Sitaki kuishi katika mioyo ya watu wa nchi yangu.
-
11:27 - 11:29Nataka kuishi katika nyumba yangu"
-
11:29 - 11:31Hizo ni
-
11:31 - 11:33aina nne kuu za hadithi za kifo,
-
11:33 - 11:34na nimejaribu kuonesha maana
-
11:34 - 11:37ni jinsi zinasemwa na kila jamii
-
11:37 - 11:38na utofauti mdogo sana
-
11:38 - 11:41kutosha fasheni ya siku.
-
11:41 - 11:44Na ukweli kwamba zinajirudia katika hii njia,
-
11:44 - 11:47katika mfumo uleule lakini katika aina tofauti za kuamini,
-
11:47 - 11:49Nadhani,
-
11:49 - 11:51tunatakiwa kuwa na wasiwasi wa ukweli
-
11:51 - 11:55katika aina yoyote ya hadithi hizi.
-
11:55 - 11:57Ukweli kwamba watu wanaamini
-
11:57 - 12:00mungu mwenye nguvu atawafufua na kuishi tena
-
12:00 - 12:03na wengine wanaamini wanasayansi wenye nguvu watawafufua na kuishi tena.
-
12:03 - 12:06inasema kwamba hamna anayeamini hili
-
12:06 - 12:09au nguvu ya ukweli.
-
12:09 - 12:11ila,tunaamini hadithi hizi
-
12:11 - 12:13kwa sababu tunachochewa kuziamini,
-
12:13 - 12:15na tunachochewa kuziamini
-
12:15 - 12:19kwa sababu tunaogopa kifo.
-
12:19 - 12:21Kwa hiyo swali ni,
-
12:21 - 12:25je,tunapotoshwa kuongoza maisha tuliyonayo
-
12:25 - 12:29katika njia ya uoga na kupotosha ukweli?
-
12:29 - 12:32au tunaweza kushinda huu uchochezi?
-
12:32 - 12:34Mphilosophia wa kigiriki Epicurus
-
12:34 - 12:36alifikiri tunaweza.
-
12:36 - 12:39Alihoji kwamba uoga wa kifo ni kitu cha asili,
-
12:39 - 12:42lakini sio cha mantiki.
-
12:42 - 12:45"kifo",alisema,"si kitu kwetu,
-
12:45 - 12:47kwa sababu tuko hapa,kifo hakipo,
-
12:47 - 12:51na wakati kifo kikiwa hapa,na sisi tunakuwa hatupo"
-
12:51 - 12:53Mara nyingi kauli hii huwa inanukuliwa,lakini ni vigumu
-
12:53 - 12:55kuielewa,kiundani zaidi,
-
12:55 - 12:57kwa sababu kiuhakika wazo hili la kuondoka
-
12:57 - 13:00ni gumu sana kulifikiria.
-
13:00 - 13:02Miaka 2000 baadaye,mphilosophia mwingine,
-
13:02 - 13:05Ludwig Wittgenstein,alisema:
-
13:05 - 13:08"Kifo sio tukio la maisha:
-
13:08 - 13:12Hatuishi ili kuzoea kifo.
-
13:12 - 13:13Akaongeza kwa kusema,
-
13:13 - 13:16"katika maana hii,maisha hayana mwisho"
-
13:16 - 13:19Kwa hiyo ilikuwa halisi kwa mimi kama mtoto
-
13:19 - 13:22kuogopa kumezwa na shimo la kifo,
-
13:22 - 13:23lakini haikuwa na mantiki,
-
13:23 - 13:25kwa sababu kumezwa na shimo la kifo
-
13:25 - 13:27sio kitu ambacho mtu yoyote kati yetu
-
13:27 - 13:31ataishi na kukutana nacho.
-
13:31 - 13:33Sasa,kukwepa uchochezi huu sio kitu rahisi kwa sababu
-
13:33 - 13:36hofu ya kifo imo ndani yetu,
-
13:36 - 13:41wakati huohuo tunaona uoga huna mantiki,
-
13:41 - 13:43na tunapoonyesha uoga
-
13:43 - 13:46katika njia ambazo tunachochewa bila kujitambua,
-
13:46 - 13:47angalau tunaweza kuanza
-
13:47 - 13:50kupunguza ule msukumo ulionao
-
13:50 - 13:52katika maisha yetu.
-
13:52 - 13:55Sasa,naona inasaidia kuona maisha
-
13:55 - 13:57ykifanana na kama kitabu:
-
13:57 - 13:59Kama kilivyozungukwa na kava,
-
13:59 - 14:00mwanzoni na mwishoni,
-
14:00 - 14:04kwa hiyo maisha yetu yamezungukwa kwa kuzaliwa na kifo,
-
14:04 - 14:08na hata kama kitabu kina mipaka mwanzoni na mwishoni,
-
14:08 - 14:10inaweza jumuisha mazingira ya mbali,
-
14:10 - 14:13maumbile ya kusisimua,matukio mazuri sana.
-
14:13 - 14:16Na hata kama kitabu kina mipaka mwanzoni na mwishoni,
-
14:16 - 14:18wahusika ndani yake
-
14:18 - 14:21hawajui mwisho wa upeo wa macho.
-
14:21 - 14:24Wanajua nyakati zinazohusu hadithi zao,
-
14:24 - 14:27hata kama kitabu kikifungwa.
-
14:27 - 14:29kwa wahusika katika kitabu
-
14:29 - 14:33hawaogopi kufika ukurasa wa mwisho.
-
14:33 - 14:35Long John Silver hakuogopi
-
14:35 - 14:38kumalizia nakala yako ya "Treasure Island"
-
14:38 - 14:39na itakuwa na sisi.
-
14:39 - 14:42Fikiria kitabu cha maisha yako,
-
14:42 - 14:44inakava,mwanzoni na mwishoni,kuzaliwa kwako na kufa kwako.
-
14:44 - 14:47Unaweza kujua nyakati,
-
14:47 - 14:48zinazofanya maisha yako.
-
14:48 - 14:50Haileti maana kwa wewe kuogopa
-
14:50 - 14:53kilicho nje ya kava,
-
14:53 - 14:54kama ni kabla ya kuzaliwa
-
14:54 - 14:56au baada ya kifo chako.
-
14:56 - 14:59Na hautakiwi kuwa na wasiwasi kitabu ni kirefu kiasi gani,
-
14:59 - 15:02au ni cha kichekesho au kinaelezea ukubwa wa kitu.
-
15:02 - 15:04Kitu kimoja cha msingi
-
15:04 - 15:07ni kwamba unaifanya iwe hadithi nzuri.
-
15:07 - 15:09Asante.
-
15:09 - 15:13(Makofi)
- Title:
- Hadithi nne tunazoambia nafsi zetu kuhusu kifo
- Speaker:
- Stephen Cave
- Description:
-
Mwanaphilosophia Steven Cave anaanza kwa swali lenye kazi lakini la kulazimisha kufikiria:Lini ulitambua utakuja kufa?Na cha kusisimua zaidi:Kwa nini wanadamu huwa tunakwepa kifo?Katika hotuba hii ya kuvutia Bwana Cave anachambua vitu vinne katika maisha ya binadamu ambapo huwa tunaambia nafsi zetu "ili kutusaidia kupambana na uoga wa kifo"
- Video Language:
- English
- Team:
- closed TED
- Project:
- TEDTalks
- Duration:
- 15:33
Joachim Mangilima approved Swahili subtitles for The 4 stories we tell ourselves about death | ||
Joachim Mangilima accepted Swahili subtitles for The 4 stories we tell ourselves about death | ||
Joachim Mangilima edited Swahili subtitles for The 4 stories we tell ourselves about death | ||
Joachim Mangilima edited Swahili subtitles for The 4 stories we tell ourselves about death | ||
Nelson Simfukwe edited Swahili subtitles for The 4 stories we tell ourselves about death | ||
Nelson Simfukwe edited Swahili subtitles for The 4 stories we tell ourselves about death | ||
Nelson Simfukwe edited Swahili subtitles for The 4 stories we tell ourselves about death | ||
Nelson Simfukwe edited Swahili subtitles for The 4 stories we tell ourselves about death |