Return to Video

Jinsi gani habari za uongo huleta madhara ya kweli

  • 0:01 - 0:04
    Nataka niwaambie kisa
    kuhusu msichana mmoja.
  • 0:05 - 0:07
    Lakini siwezi kuwaambia jina lake halisi.
  • 0:07 - 0:09
    Hivyo tufanye kumuita Hadiza.
  • 0:10 - 0:11
    Hadiza ana miaka 20.
  • 0:12 - 0:13
    Ana aibu,
  • 0:13 - 0:16
    lakini ana tabasamu zuri
    ambalo hufanya uso wake kung'aa
  • 0:17 - 0:19
    Lakini yuko katika maumivu wakati wote.
  • 0:21 - 0:24
    Na anaweza kuwa
    mtu wa matibabu maisha yake yote.
  • 0:25 - 0:27
    Je wataka kujua kwa nini?
  • 0:28 - 0:31
    Hadiza ni msichana wa Chibok,
  • 0:31 - 0:34
    na mnamo Aprili 14, 2014, alitekwa
  • 0:34 - 0:36
    na magaidi wa Boko Haram.
  • 0:36 - 0:39
    Ingawa alijaribu kutoroka,
  • 0:39 - 0:42
    kwa kuruka toka kwenye gari lililokuwa limebeba wasichana.
  • 0:42 - 0:46
    Lakini alipotua chini, alivunjika miguu yako yote miwili,
  • 0:46 - 0:49
    na alihitaji kutambaa kwa tumbo kujificha kichakani.
  • 0:49 - 0:53
    Aliniambia aliogopa sana
    kuwa Boko Haram wangeweza kumrudia.
  • 0:54 - 0:58
    Alikuwa mmoja wa wasichana 57 waliotoroka
    kwa kuruka toka kwenye magari siku ile.
  • 0:58 - 1:01
    Kisa hiki, hakika, kilisambaa kama mawimbi
  • 1:01 - 1:02
    duniani kote.
  • 1:02 - 1:06
    Watu kama Michelle Obama,
    Malala na wengine
  • 1:06 - 1:08
    walitoa sauti zao wakipinga,
  • 1:08 - 1:11
    na wakati huo huo --
    nilikuwa nikiishi London wati huo
  • 1:11 - 1:16
    Nilitumwa kutoka London kwenda Abuja
    kupata habari za Jukwaa la Uchumi Duniani
  • 1:16 - 1:18
    ambapo Naijeria ilikuwa mwenyeji
    kwa mara ya kwanza
  • 1:19 - 1:23
    Lakini nilipofika, ilikuwa dhahiri
    kwamba kulikuwa na habari moja tu mjini.
  • 1:24 - 1:26
    Tuliiiweka serikali kwenye shinikizo.
  • 1:26 - 1:28
    Tuliuliza maswali magumu
    juu ya nini wanafanya
  • 1:28 - 1:30
    kuwarudisha wasichana hawa.
  • 1:30 - 1:32
    Ilieleweka hakika,
  • 1:32 - 1:35
    hawakuwa na furaha juu ya maswali yetu,
  • 1:35 - 1:39
    na tuseme tu tulipata mgao mzuri
    wa "ukweli mbadala".
  • 1:39 - 1:41
    (Kicheko)
  • 1:41 - 1:45
    Wanaijeria wenye ushawishi mkubwa
    walikuwa wakituambia wakati ule
  • 1:45 - 1:47
    kuwa tulikuwa washamba.
  • 1:47 - 1:50
    hatukuelewa hali ya siasa ya Naijeria.
  • 1:51 - 1:53
    Lakini pia walituambia
  • 1:53 - 1:56
    kuwa habari ya wasichana wa Chibok
  • 1:56 - 1:57
    illikuwa mzaha.
  • 1:58 - 2:01
    Cha kusikitisha ni kuwa
    habari hii ya mzaha imedumu
  • 2:01 - 2:03
    na bado kuna watu Naijeria leo
  • 2:03 - 2:06
    wanaoamini
    wasichana wa Chibok hawakutekwa.
  • 2:07 - 2:09
    Bado, nilikuwa nikiongea na watu kama hawa
  • 2:10 - 2:12
    wazazi wenye huzuni kubwa,
  • 2:12 - 2:16
    ambao walituambia
    siku Boko Haram waliwateka binti zao,
  • 2:16 - 2:21
    walikimbia mpaka Msitu wa Sambisa
    wakifukuza magari laliyobeba binti zao.
  • 2:21 - 2:25
    Wao walikuwa na mapanga kama silaha,
    lakini walilazimika kurudi
  • 2:25 - 2:26
    sababu Boko Haram walikuwa na bunduki.
  • 2:27 - 2:31
    Kwa miaka miwili, pasipo kuepukika,
    ajenda za habari zilisonga mbele,
  • 2:31 - 2:33
    na kwa miaka miwili,
  • 2:33 - 2:36
    hatukusikia sana
    kuhusu wasichana wa Chibok.
  • 2:36 - 2:38
    Kila moja alidhania wamekwishakufa.
  • 2:38 - 2:40
    Lakini Aprili mwaka jana,
  • 2:40 - 2:42
    niliweza kupata video hii.
  • 2:43 - 2:45
    Hii ni picha-mnato toka kwenye video
  • 2:45 - 2:48
    ambayo Boko Haram walirekodi
    kama ushahidi kuwa wako hai,
  • 2:49 - 2:51
    na kupitia chanzo kimoja,
    nilipata video hii.
  • 2:52 - 2:54
    Lakini kabla sijaichapisha,
  • 2:54 - 2:57
    Nilihitaji kusafiri
    kwenda kaskazini mashariki mwa Naijeria
  • 2:57 - 2:59
    kuzungumza na wazazi, kuihakikisha.
  • 2:59 - 3:03
    Sikuhitaji kusubiri sana
    kupata uthibitisho.
  • 3:04 - 3:07
    Mmoja wa wamama,
    alipoangalia hiyo video, aliniambia
  • 3:07 - 3:10
    kama angeweza kuifika ndani ya kompyuta
  • 3:10 - 3:14
    na kumvuta na kumtoa nje mtoto wake
    kutoka kwenye kompyuta,
  • 3:14 - 3:15
    angefanya hivyo.
  • 3:16 - 3:19
    Kwa wale kati yenu ambao ni wazazi,
    kama mimi, katika wasikilizaji.
  • 3:19 - 3:22
    Mnaweza tu kufikiria uchungu
  • 3:22 - 3:24
    ambao yule mama aliusikia
  • 3:26 - 3:32
    Video hii iliendelea hadi kuanzisha
    mjadala wa mazungumzo na Boko Haram.
  • 3:32 - 3:36
    Na seneta mmoja wa Kinaijeria aliniambia
    kuwa kwa sababu ya video hii
  • 3:36 - 3:38
    waliingia katika yale mazungumzo,
  • 3:38 - 3:42
    kwa sababu muda mrefu walidhani
    wasichana wa Chibok walishakufa.
  • 3:43 - 3:47
    Wasichana 21 waliachiwa huru
    mwezi Oktoba mwaka jana.
  • 3:47 - 3:51
    Cha kusikitisha, karibu 200 kati yao
    bado hawajapatikana.
  • 3:52 - 3:56
    Ni lazima nikiri,
    sijawa mwangalizi niliyependelea
  • 3:56 - 3:57
    kuzungumzia habari hii.
  • 3:57 - 4:01
    Nakuwa na hasira ninapofikiria
    juu ya fursa zinazopotea
  • 4:02 - 4:03
    kuwaokoa wasichana hawa.
  • 4:03 - 4:07
    Nakuwa na hasira ninapofikiria
    juu ya kile wazazi wameniambia,
  • 4:07 - 4:10
    kuwa ingekuwa mabinti hawa
    ni wa matajiri na wenye nguvu,
  • 4:10 - 4:12
    wangepatikana mapema zaidi.
  • 4:14 - 4:16
    Na nina hasira
  • 4:16 - 4:18
    kwamba simulizi la mzaha
  • 4:18 - 4:20
    ambalo naamini hakika
  • 4:20 - 4:22
    limesababisha kuchelewa;
  • 4:22 - 4:25
    lilikuwa ni sehemu ya sababu
    ya ucheleweshwaji wa kurudi kwao.
  • 4:27 - 4:31
    Hii inaonesha kwangu
    hatari kubwa ya habari za uongo.
  • 4:31 - 4:33
    Nini twaweza kufanya juu ya hili?
  • 4:34 - 4:36
    Kuna watu werevu sana,
  • 4:36 - 4:38
    wahandisi werevu huko Google na Facebook,
  • 4:38 - 4:43
    wanaojaribu kutumia tekinolojia
    kuzuia kusambaa kwa habari za uongo.
  • 4:43 - 4:48
    Lakini zaidi ya hapo, nafikiri
    kila mmoja hapa -- wewe na mimi --
  • 4:48 - 4:50
    tuna nafasi ya kushiriki katika hilo.
  • 4:50 - 4:53
    Sisi ndio tunaoshirikishana maudhui
  • 4:53 - 4:55
    Sisi ndio tunaoshirikishana
    habari mitandaoni
  • 4:55 - 4:57
    Nyakati za leo, sisi sote ni wachapishaji,
  • 4:59 - 5:01
    na tuna jukumu.
  • 5:01 - 5:03
    Katika kazi yangu kama mwanahabari,
  • 5:03 - 5:05
    Ninaangalia, ninathibitisha,
  • 5:05 - 5:09
    Ninaamini hisia zangu,
    lakini nauliza maswali magumu.
  • 5:10 - 5:12
    Kwa nini huyu mtu ananiambia habari hii?
  • 5:13 - 5:16
    Nini atakachokipata
    kwa kunishirikisha taarifa hii?
  • 5:16 - 5:18
    Je, ana ajenda ya siri?
  • 5:19 - 5:24
    Ninaamini kabisa kuwa wote tunatakiwa
    kuanza kuuliza maswali magumu zaidi
  • 5:24 - 5:27
    kwa taarifa tunazozipata mtandaoni.
  • 5:30 - 5:35
    Utafiti unaonesha kwamba kati yetu
    kuna wasiosoma zaidi ya vichwa vya habari
  • 5:35 - 5:38
    kabla ya kushirikisha habari.
  • 5:38 - 5:39
    Nani hapa amefanya hivyo?
  • 5:40 - 5:41
    Najua mimi nimefanya.
  • 5:42 - 5:44
    Lakini ingekuwaje kama
  • 5:45 - 5:50
    tungeacha kuchukua taarifa tuipatayo jinsi ionekanavyo kijuujuu?
  • 5:50 - 5:54
    vipi kama tutasimama na kufikiria athari
  • 5:54 - 5:56
    za taarifa ambazo tunazisambaza
  • 5:56 - 6:00
    na uwezo wake wa kuchochea vurugu na chuki?
  • 6:01 - 6:05
    Vipi kama tutasimama na kufikiria juu ya athari kwenye maisha halisi
  • 6:05 - 6:07
    za taarifa tunazoshirikishana?
  • 6:08 - 6:10
    Ahsanteni sana kwa kunisikiliza.
  • 6:10 - 6:13
    (Makofi na vifijo)
Title:
Jinsi gani habari za uongo huleta madhara ya kweli
Speaker:
Stephanie Busari
Description:

Mnamo Aprili 14, 2014, shirika la kigaidi la Boko Haram liliteka zaidi ya wasichana wa shule 200 kutoka mji wa Chibok, Naijeria. Duniani kote, uhalifu huu ulifanywa mfano kwa kauli mbiu ya #BringBackOurGirls yaani "Rejesha Wasichana Wetu" -- lakini ndani ya Naijeria, maafisa wa serikali waliita uhalifu huu kuwa ni mzaha, kusababisha utata na kuchelewesha jitihada zozote za kuwakomboa wasichana hawa. Katika zungumzo hili shupavu, mwanahabari Stephanie Busari anaelekezea janga la Chibok kueleza hatari kubwa ya habari za uongo na nini tunaweza kufanya kuzizuia.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
06:26
Joachim Mangilima approved Swahili subtitles for How fake news does real harm
Joachim Mangilima accepted Swahili subtitles for How fake news does real harm
Clarence Bitegeko edited Swahili subtitles for How fake news does real harm
Clarence Bitegeko edited Swahili subtitles for How fake news does real harm
Clarence Bitegeko edited Swahili subtitles for How fake news does real harm

Swahili subtitles

Revisions