Return to Video

Siri 8 za mafanikio

  • 0:00 - 0:03
    Huu ni mjadala wa kweli wa masaa mawili nilioutoa kwa wanafunzi wa sekondari,
  • 0:03 - 0:05
    unakatiza kwa dakika tatu.
  • 0:05 - 0:07
    Na yote yalianza siku moja nikiwa kwenye ndege, nikielekea TED,
  • 0:07 - 0:09
    miaka saba iliyopita.
  • 0:09 - 0:13
    Na katika siti iIiyopo pembeni yangu
    alikuwapo mwanafunzi wa sekondari, kijana,
  • 0:13 - 0:15
    alitokea katika familia masikini sana.
  • 0:15 - 0:18
    Na alitaka kujitengenezea maisha,
  • 0:18 - 0:20
    akaniuliza swali rahisi.
  • 0:20 - 0:22
    Alisema, "Ni nini husababisha mafanikio?"
  • 0:22 - 0:23
    Na nilijisikia vibaya sana,
  • 0:23 - 0:26
    kwa sababu sikuweza kumpa jibu zuri.
  • 0:26 - 0:28
    Hivyo nilitoka kwenye ndege, na kuja TED.
  • 0:28 - 0:32
    Na nikafikiri, lahaula, niko miongoni mwa watu wenye mafanikio!
  • 0:32 - 0:34
    Kwa nini nisiwaulize wao
    nini kiliwasaidia kufanikiwa,
  • 0:34 - 0:36
    na kuwaelimisha watoto?
  • 0:37 - 0:40
    Hivyo, miaka saba,
    mahojiano 500 baadaye,
  • 0:40 - 0:43
    nitawaambia nini hasa hupelekea mafanikio
  • 0:43 - 0:45
    yanayowasukuma wanaTED.
  • 0:45 - 0:47
    Na jambo la kwanza ni shauku.
  • 0:48 - 0:50
    Freeman Thomas anasema,
    "Ninaendeshwa na shauku yangu."
  • 0:51 - 0:53
    WanaTED hufanya yote kwa sababu ya upendo;
    hawafanyi kwa ajili ya fedha.
  • 0:53 - 0:57
    Carol Coletta anasema, "Ningelipa
    mtu kufanya ninachofanya. "
  • 0:57 - 0:58
    Na jambo la kushangaza ni:
  • 0:58 - 1:00
    ukifanya kwa upendo,
    pesa huja hata hivyo.
  • 1:01 - 1:04
    Kazi! Rupert Murdoch aliniambia, "Yote ni kazi ngumu.
  • 1:04 - 1:07
    Hakuna kitu kinakuja kwa urahisi.
    Lakini ninaifurahia kazi yangu. "
  • 1:07 - 1:10
    Amesema furaha? Rupert? Ndiyo!
  • 1:10 - 1:11
    (Vicheko)
  • 1:12 - 1:14
    WanaTED hufurahia kazi zao.
    Na hufanya kazi kwa bidii.
  • 1:14 - 1:17
    Niligundua, sio workaholics. Ni workafrolics.
  • 1:17 - 1:19
    (Vicheko)
  • 1:19 - 1:20
    Vyema!
  • 1:20 - 1:21
    (Makofi)
  • 1:21 - 1:24
    Alex Garden anasema, "Ili kufanikiwa, weka jitihada katika kitu kimoja
  • 1:24 - 1:26
    na kuwa mtaalamu kwenye hilo."
  • 1:26 - 1:28
    Hakuna mazingaombwe;
    ni mazoezi, mazoezi, mazoezi.
  • 1:28 - 1:29
    Na ni lengo.
  • 1:30 - 1:31
    Norman Jewison aliniambia,
  • 1:31 - 1:34
    "Nadhani huhusiana na kujishughulisha na jambo moja. "
  • 1:35 - 1:36
    Na kukazana!
  • 1:36 - 1:38
    Daudi Gallo anasema, "Jisukume.
  • 1:38 - 1:41
    Kimwili, kiakili,
    unapaswa kujisukuma, kujisukuma, kujisukuma."
  • 1:41 - 1:44
    Unahitaji kujisukuma kutoka katika aibu na mashaka.
  • 1:44 - 1:46
    Goldie Hawn anasema,
    "Siku zote nilikuwa na mashaka.
  • 1:46 - 1:48
    Sikuwa na ujuzi wakutosha;
    Sikukuwa na kipaji cha kutosha.
  • 1:48 - 1:50
    Sikufikiri ningeweza kufanikiwa."
  • 1:50 - 1:52
    Daima si rahisi kujisukuma,
  • 1:52 - 1:54
    na ndiyo maana tuna mama.
  • 1:54 - 1:55
    (Vicheko)
  • 1:55 - 1:57
    (Makofi)
  • 1:57 - 2:00
    Frank Gehry aliniambia,
  • 2:00 - 2:01
    "Mama yangu alinisukuma."
  • 2:01 - 2:03
    (Vicheko)
  • 2:03 - 2:04
    Tumikia!
  • 2:04 - 2:07
    Sherwin Nuland anasema,
    "Ilikuwa ni fursa kutumikia kama daktari."
  • 2:08 - 2:10
    Watoto wengi wanataka kuwa mamilionea.
  • 2:10 - 2:11
    Jambo la kwanza ninalosema ni:
  • 2:12 - 2:13
    "Sawa, vizuri huwezi kujihudumia mwenyewe;
  • 2:13 - 2:16
    unapaswa kutumikia wengine
    kitu cha thamani.
  • 2:16 - 2:18
    Kwa sababu hiyo ndiyo njia
    watu hupata utajiri. "
  • 2:19 - 2:20
    Mawazo!
  • 2:20 - 2:23
    MwanaTED Bill Gates anasema, "Nilikuwa na wazo:
  • 2:23 - 2:26
    kuanzisha kampuni ya kwanza ya programu za mikro-kompyuta."
  • 2:26 - 2:28
    Ningependa kusema ni wazo zuri sana.
  • 2:28 - 2:31
    Na hakuna miujiza katika ubunifu
    wa mawazo mapya --
  • 2:31 - 2:33
    ni kufanya baadhi ya mambo rahisi sana.
  • 2:33 - 2:35
    Na ninatoa ushahidi mwingi.
  • 2:35 - 2:36
    Stahimili!
  • 2:37 - 2:38
    Joe Kraus anasema,
  • 2:38 - 2:40
    "Ustahimilifu ni sababu namba
    moja ya mafanikio yetu. "
  • 2:41 - 2:44
    Unahitaji kustahimili unapofeli. Unahitaji kustahimili misukosuko!
  • 2:44 - 2:48
    Ambayo ni "Kukosolewa,
    Kukataliwa, Watu ovyo na Presha."
  • 2:48 - 2:51
    (Vicheko)
  • 2:51 - 2:54
    Hivyo, jibu kwa swali hili ni rahisi:
  • 2:54 - 2:57
    Lipa dola 4,000 na uje kwenye TED.
  • 2:57 - 2:58
    (Vicheko)
  • 2:58 - 3:01
    Au ukishindwa hilo, fanya
    mambo haya nane - na niamini,
  • 3:01 - 3:04
    haya ni mambo makuu nane
    ambayo huleta mafanikio.
  • 3:04 - 3:07
    Asanteni wanaTED
    kwa mahojiano yenu yote!
  • 3:07 - 3:10
    (Makofi)
Title:
Siri 8 za mafanikio
Speaker:
Richard St. John
Description:

Kwa nini watu wanafanikiwa? Je, ni kwa sababu wana akili? Au ni bahati tu? Wala. Mchambuzi Richard St. John anatoa muhtasari wa miaka ya mahojiano katika dakika 3 kuhusu siri halisi za mafanikio.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
03:13
Nelson Simfukwe approved Swahili subtitles for 8 secrets of success
Nelson Simfukwe accepted Swahili subtitles for 8 secrets of success
Nelson Simfukwe edited Swahili subtitles for 8 secrets of success
Sophia Mwema edited Swahili subtitles for 8 secrets of success
Sophia Mwema edited Swahili subtitles for 8 secrets of success
Sophia Mwema edited Swahili subtitles for 8 secrets of success
Sophia Mwema edited Swahili subtitles for 8 secrets of success
Sophia Mwema edited Swahili subtitles for 8 secrets of success
Show all

Swahili subtitles

Revisions