Return to Video

Ukweli 12 niliojifunza kupitia maisha na uandishi

  • 0:01 - 0:04
    Chumba cha mjukuu wangu mwenye miaka saba kipo karibu na changu
  • 0:05 - 0:06
    mara nyingi huamka asubuhi
  • 0:06 - 0:08
    na kusema,
  • 0:08 - 0:10
    "Unajua, leo inaweza kuwa siku bora kuliko zote. "
  • 0:11 - 0:13
    Na mara nyingine, usiku wa manane,
  • 0:13 - 0:16
    huita kwa sauti za woga
  • 0:16 - 0:19
    "Nana, utaumwa na kufa siku moja?"
  • 0:19 - 0:24
    Nadhani hili linasema mengi kwangu na watu wengi ninaowajua,
  • 0:24 - 0:27
    kwamba sisi ni mchanganyiko
    wa matarajio yenye furaha
  • 0:27 - 0:28
    na hofu.
  • 0:29 - 0:33
    Hivyo, siku chache kabla ya kutimiza miaka 61, nilitafakari
  • 0:33 - 0:37
    nikaamua kukusanya orodha ya kila kitu ninachojua.
  • 0:38 - 0:41
    Kuna ukweli mchache sana katika utamaduni wetu,
  • 0:41 - 0:44
    na ni vizuri tuwe na uhakika na mambo machache.
  • 0:45 - 0:48
    Kwa mfano, umri wangu sio 47 tena,
  • 0:49 - 0:52
    Ingawa ndio umri ninaojisikia,
  • 0:52 - 0:54
    au umri ningependa kufikiri niko.
  • 0:55 - 0:58
    Rafiki yangu Paulo alisema katika miaka yake ya 70
  • 0:58 - 1:01
    kwamba alihisi kama kijana mwenye matatizo mengi tu.
  • 1:01 - 1:05
    (Vicheko)
  • 1:05 - 1:08
    Nafsi yetu ya kweli ipo nje ya muda na sehemu
  • 1:08 - 1:09
    lakini nikiangalia nyaraka,
  • 1:09 - 1:13
    Naweza, kwa kweli, kuona kwamba nilizaliwa mwaka wa 1954
  • 1:13 - 1:16
    Hisia zangu binafsi zipo nje ya muda na sehemu.
  • 1:16 - 1:18
    Haina umri.
  • 1:18 - 1:22
    Nina kila umri ambao nimewahi kuwa,na wewe pia,
  • 1:22 - 1:24
    Ingawa siwezi kuepuka kusema,
  • 1:24 - 1:27
    kwamba ingesaidia kama nisingefuata
  • 1:27 - 1:30
    kanuni za huduma ya ngozi za miaka ya 60,
  • 1:30 - 1:33
    ambayo ilihusisha kuota jua kama iwezekanavyo
  • 1:33 - 1:36
    nikijisiliba mafuta ya mtoto
  • 1:36 - 1:40
    na kumeremeta chini ya foii ya aluminium
  • 1:40 - 1:42
    (Vicheko)
  • 1:42 - 1:44
    Nilijisikia uhuru sana, ingawa,
    nilbidi kuutizama ukweli
  • 1:44 - 1:48
    kwamba sikuwa tena katika miaka ya mwisho ya rika la kati,
  • 1:48 - 1:52
    hivyo niliamua kuandika
    kila kitu nilichojua.
  • 1:52 - 1:55
    Siku hizi watu wamejisikia wameelemewa,
  • 1:55 - 1:58
    na huniuliza ukweli ni upi.
  • 1:58 - 2:05
    Hivyo, natumaini orodha ya vitu ninavzo fahamu kwau fasaha
  • 2:05 - 2:08
    itatoa misingi ya uendeshaji
  • 2:08 - 2:11
    kwa mtu yeyote anayehisi
    kuelemewa au kuchanganyikiwa.
  • 2:12 - 2:14
    Namba moja:
  • 2:14 - 2:18
    Jambo la kwanza na ukweli kabisa ni kwamba ukweli wote ni kitendawili.
  • 2:18 - 2:22
    Maisha yana thamani, na zawadi nzuri sana kupita maelezo,
  • 2:22 - 2:27
    na haiwezekani kutelezeka kwa kiumbe cha mwili.
  • 2:27 - 2:28
    Imekuwa uwiano mbaya sana
  • 2:28 - 2:32
    kwa wale ambao tulizaliwa nyeti sana.
  • 2:32 - 2:35
    Ni vigumu sana na ni ajabu
    kwamba wakati mwingine tunajiuliza
  • 2:35 - 2:36
    kama tunataniwa.
  • 2:37 - 2:42
    Imejazwa na wema na uzuri wa umbo,
  • 2:42 - 2:44
    umasikini,
  • 2:44 - 2:47
    Mafuriko na watoto na chunusi na Mozart,
  • 2:47 - 2:49
    vyote vilibiringizwa pamoja.
  • 2:50 - 2:52
    Sidhani ni mfumo mzuri.
  • 2:52 - 2:55
    (Vicheko)
  • 2:55 - 2:59
    Namba mbili: karibia kila kitu kitafanya kazi tena
  • 2:59 - 3:01
    ukikichomoa kwa dakika chache --
  • 3:01 - 3:04
    (Vicheko)
  • 3:04 - 3:07
    (Makofi)
  • 3:07 - 3:09
    hata na wewe.
  • 3:11 - 3:14
    Tatu: karibia, hakuna chochote nje ya wewe
  • 3:14 - 3:17
    kitakachokusaidia kwa njia yoyote ya kudumu,
  • 3:17 - 3:19
    isipokuwa kama unasubiria kiungo.
  • 3:20 - 3:25
    Huwezi kununua, kutekeleza au kuchumbia utulivu na amani.
  • 3:25 - 3:29
    Huu ni kweli ya kutisha,
    na ninauchukia.
  • 3:30 - 3:32
    Lakini ni kazi ya ndani,
  • 3:32 - 3:35
    na hatuwezi kupanga amani
    au uboreshaji wa kudumu
  • 3:35 - 3:37
    kwa ajili ya watu tunaowapenda duniani.
  • 3:37 - 3:39
    Wanapaswa kutafuta njia yao wenyewe,
  • 3:39 - 3:41
    majibu wenyewe.
  • 3:41 - 3:44
    Huwezi kuenda pamoja na
    watoto wako wakubwa
  • 3:44 - 3:49
    kwenye safari yao ya kishujaa.
  • 3:49 - 3:51
    Unapaswa kuwaacha huru.
  • 3:51 - 3:54
    Sio heshima kuwavunga.
  • 3:55 - 3:57
    Na kama ni tatizo la mtu mwingine,
  • 3:57 - 3:59
    labda hata wewe hauna jibu, pia.
  • 3:59 - 4:00
    (Vicheko)
  • 4:01 - 4:03
    Msaada wetu mara nyingi hausaidii.
  • 4:04 - 4:06
    Msaada wetu mara nyingi ni sumu.
  • 4:07 - 4:10
    Na msaada ni upande chanya wa udhibiti.
  • 4:11 - 4:13
    Acha kusaidia sana.
  • 4:13 - 4:17
    Usisambaze msaada wako na wema kwa kila mtu.
  • 4:17 - 4:19
    (Vicheko)
  • 4:19 - 4:21
    (Makofi)
  • 4:21 - 4:23
    Hii inatuleta kwa namba nne:
  • 4:23 - 4:27
    kila mtu amevunjika,
    amevunjwa, ana wivu na hofu zake,
  • 4:27 - 4:30
    hata wanaoonekana kuwa pamoja zaidi.
  • 4:30 - 4:32
    Wako kama wewe kuliko unavzoweza kuamini,
  • 4:32 - 4:37
    hivyo usilinganisha undani wako na nje za watu wengine.
  • 4:37 - 4:40
    Itakufanya ujisikie ovyo kuliko ulivyo tayari.
  • 4:40 - 4:43
    (Vicheko)
  • 4:44 - 4:48
    Pia, huwezi kuwaokoa, kurekebisha au kuwakomboa
  • 4:48 - 4:50
    au kumpatia mtu yeyote busara.
  • 4:50 - 4:53
    Kilichosaidia kupata nafuu na kukaa safi na madawa kwa miaka 30 iliyopita
  • 4:53 - 4:56
    ilikuwa janga la tabia na fikra zangu.
  • 4:56 - 4:58
    Hivyo niliomba msaada kwa marafiki,
  • 4:58 - 5:00
    na nikamrudia muumbaji.
  • 5:00 - 5:04
    Kifupisho kimoja cha Mungu ni "zawadi ya kukata tamaa,"
  • 5:04 - 5:06
    M-U-N-G-U,
  • 5:06 - 5:08
    Au kama rafiki yangu mmoja alivyoiweka,
  • 5:08 - 5:13
    mwishoni nilikuwa nikipungukiwa kuliko nilivyoweza kupunguza viwango vyangu.
  • 5:13 - 5:19
    (Vicheko)
  • 5:19 - 5:21
    Kwa hiyo Mungu anaweza kumaanisha, katika kesi hii,
  • 5:21 - 5:25
    "mimi kuishiwa na mawazo yoyote mazuri zaidi."
  • 5:26 - 5:30
    Wakati kurekebisha na kuokoa
    na kujaribu kuokoa ni bure,
  • 5:30 - 5:33
    Kujitegemea na kujitunza ni quantum,
  • 5:33 - 5:37
    na hujiangaza katika mazingira yako
  • 5:37 - 5:38
    kama hewa safi.
  • 5:38 - 5:41
    Ni zawadi kubwa kwa duniani.
  • 5:41 - 5:46
    Watu wanapojibu kwa kusema,
    "Mmh, mtizame anavyojisikia,"
  • 5:46 - 5:49
    tabasamu tu kama vile Mona Lisa
  • 5:49 - 5:52
    na kuwatengenezea kikombe cha chai.
  • 5:53 - 5:57
    Kuonyesha upendo kikamilifu
    kwa uzuzu wa mtu, ubinafsi,
  • 5:57 - 6:00
    ukimwa, usumbufu wako
  • 6:00 - 6:01
    ni nyumbani.
  • 6:01 - 6:03
    Ndipo amani ya dunia huanzia.
  • 6:05 - 6:07
    Namba tano:
  • 6:07 - 6:12
    chokoleti yenye asilimia 75 kakao sio kweli chakula.
  • 6:12 - 6:16
    (Vicheko)
  • 6:16 - 6:20
    Matumizi yake bora ni katika mitego ya nyoka
  • 6:20 - 6:25
    au kusawazisha miguu ya viti vinavyotetema.
  • 6:25 - 6:28
    Haikuwahi kumaanishwa kama chakula.
  • 6:30 - 6:31
    Namba sita
  • 6:31 - 6:35
    (Vicheko)
  • 6:35 - 6:36
    Kuandika.
  • 6:37 - 6:41
    Kila mwandishi unayemjua huanaandika rasimu mbaya za mwanzo,
  • 6:41 - 6:43
    Lakini hutuliza kitako kwenye kiti.
  • 6:43 - 6:45
    Hiyo ndio siri ya maisha.
  • 6:45 - 6:48
    Hiyo labda ndio tofauti kuu
    kati yako na wao.
  • 6:48 - 6:50
    Wanafanya tu.
  • 6:50 - 6:52
    Wanafanya kwa makubaiano na wao wenyewe.
  • 6:53 - 6:55
    Wanafanya katika deni la heshima yao.
  • 6:55 - 6:58
    Wanasimulia hadithi kutokea kwao
  • 6:58 - 7:00
    siku moja banda ya nyingine, kidogo kidogo.
  • 7:00 - 7:02
    Kaka yangu alipokuwa darasa la nne,
  • 7:02 - 7:06
    alitakiwa kuwasilisha insha juu ya ndege kesho yake,
  • 7:06 - 7:09
    Na hakuanza bado.
  • 7:09 - 7:13
    Basi baba akaketi naye na kitabu cha Audubon,
  • 7:13 - 7:15
    karatasi, penseli na brads -
  • 7:15 - 7:21
    kwa wale ambao mmekuwaa wadogo kidogo na mna kukumbuka brads -
  • 7:21 - 7:24
    na akamwambia kaka yangu,
  • 7:24 - 7:26
    "Chukua tu ndege kwa ndege, rafiki.
  • 7:26 - 7:29
    Soma tu juu ya Mwari
  • 7:29 - 7:33
    na kisha andika kuhusu Mwari kwa sauti yako mwenyewe.
  • 7:33 - 7:36
    Na kisha soma kuhusu chickadee,
  • 7:36 - 7:38
    na utuambie kwa sauti yako mwenyewe.
  • 7:39 - 7:40
    Na kisha bata bukini. "
  • 7:40 - 7:44
    Hivyo vitu viwili muhimu kuhusu kuandika ni: ndege kwa ndege
  • 7:44 - 7:47
    na kwa kweli rasimu ovyo za mwanzo.
  • 7:48 - 7:50
    Kama hujui uanzie wapi
  • 7:50 - 7:53
    kumbuka unamiliki kila kitu kilichokutokea
  • 7:53 - 7:54
    na unaweza kusimulia.
  • 7:55 - 7:58
    Ikiwa watu walitaka uandike mazuri kuhusu wao,
  • 7:58 - 8:00
    wangemudu tabia zao vizuri zaidi.
  • 8:00 - 8:03
    (Vicheko)
  • 8:03 - 8:06
    (Makofi)
  • 8:07 - 8:10
    Utajisikia ovyo siku moja utakapoamka
  • 8:10 - 8:12
    na hujaandika juu ya mambo
  • 8:12 - 8:15
    yanazo anazokukereketa, unayotunza moyoni:
  • 8:15 - 8:19
    hadithi zako, kumbukumbu,
    maono na nyimbo -
  • 8:19 - 8:20
    Ukweli wako,
  • 8:20 - 8:22
    mtizamo wako wa vitu -
  • 8:22 - 8:24
    katika sauti yako mwenyewe.
  • 8:24 - 8:26
    Hicho pekee ndicho unachokubui kutupatia,
  • 8:26 - 8:29
    Hiyo ndiyo sababu ulizaliwa.
  • 8:30 - 8:35
    Saba: kuchapishwa na mafanikio ya ubunifu ya muda mfupi
  • 8:35 - 8:37
    ni kitu ambacho unapaswa kuponywa kutoka.
  • 8:38 - 8:41
    Vinaua watu wengi kama visivo.
  • 8:41 - 8:43
    Vitakuumiza, kukuharibu na kukubadilisha
  • 8:43 - 8:45
    kwa njia ambazo huwezi kufikiria.
  • 8:46 - 8:49
    Watu dhilifu na waovu kuliko wote niliowahi kujua
  • 8:49 - 8:52
    ni waandishi wa kiume walioandika vitabu vilivyo uza vizuri mno.
  • 8:53 - 8:57
    Na bado, tukurudia namba moja, kwamba ukweli wote ni kitendawili,
  • 8:57 - 9:00
    Pia ni muujiza kupata kazi yako kuchapishwa,
  • 9:00 - 9:03
    Ili hadithi zako zisomwe na kusikika.
  • 9:03 - 9:05
    Jaribu tu kujitahidi polepole na fantasia
  • 9:05 - 9:08
    ambayo itakuponya,
  • 9:08 - 9:12
    itajaza mashimo ya chizi ya Uswisi ndani yako.
  • 9:12 - 9:14
    haiwezekani.
  • 9:14 - 9:15
    haitokuwa.
  • 9:15 - 9:17
    Lakini uandishi unaweza.
  • 9:17 - 9:20
    Pia unaweza kuimba kwenye kwaya
    au bendi.
  • 9:20 - 9:24
    Pia uchoraji au ufugaji wa ndege
  • 9:24 - 9:27
    au kukuza mbwa wazee ambao hakuna mtu mwingine anataka.
  • 9:29 - 9:32
    Ya nane: familia.
  • 9:33 - 9:36
    Familia ni ngumu, ngumu, ngumu,
  • 9:36 - 9:39
    haijalishi namna gani tunaipenda au wavyotushangaza.
  • 9:39 - 9:42
    Tena, rudia namba moja
  • 9:42 - 9:43
    (Vicheko)
  • 9:43 - 9:47
    Katika mikusanyiko ya familia ambapo ghafla hujisikia kuua au kujiua --
  • 9:47 - 9:48
    (Vicheko)
  • 9:48 - 9:50
    Kumbuka kwamba katika hali zote,
  • 9:50 - 9:56
    Ni muujiza kwamba yeyote kati yetu hasa, alizaliwa.
  • 9:57 - 9:58
    Dunia ni shule ya msamaha.
  • 9:58 - 10:01
    Inaanza kwa kujisamehe,
  • 10:01 - 10:04
    na kisha unaweza pia kuanza kusamehe watu mezani.
  • 10:05 - 10:08
    Hivyo unaweza kufanya kazi hio katika hali tulivu.
  • 10:08 - 10:11
    (Vicheko)
  • 10:11 - 10:13
    William Blake aliposema kuwa tuko hapa
  • 10:13 - 10:16
    kujifunza kuhimili miale ya upendo,
  • 10:16 - 10:20
    alijua kwamba familia yako itakuwa sehemu kubwa ya hili,
  • 10:20 - 10:23
    Hata unapotaka kukimbia, kupiga kelele kwa ajili ya kimaisha chako.
  • 10:24 - 10:26
    Lakini ninakuahidi uko tiyari.
  • 10:26 - 10:30
    Unaweza, Sindereli, unaweza,
  • 10:30 - 10:32
    Na utashangaa.
  • 10:33 - 10:35
    Tisa: chakula.
  • 10:36 - 10:39
    Jaribu kufanya vizuri zaidi.
  • 10:39 - 10:41
    Nadhani unajua ninachmaanisha.
  • 10:41 - 10:45
    (Vicheko)
  • 10:51 - 10:52
    Namba 10 --
  • 10:52 - 10:55
    (Vicheko)
  • 10:55 - 10:56
    neema.
  • 10:56 - 11:00
    Neema ni WD-40 ya kiroho,
  • 11:00 - 11:01
    Au mabawa ya maji.
  • 11:01 - 11:07
    Fumbo la neema ni kwamba Mungu anapenda Henry Kissinger na Vladimir Putin
  • 11:07 - 11:08
    na mimi
  • 11:08 - 11:13
    sawa kama anavyompenda mjukuu wako mpya.
  • 11:13 - 11:14
    Embu fikiria.
  • 11:14 - 11:16
    (Vicheko)
  • 11:16 - 11:19
    Harakati ya neema ndio kinachotubadilisha, hutuponya
  • 11:19 - 11:21
    na huponya ulimwengu wetu.
  • 11:21 - 11:25
    Kuita neema, sema, "Nisaidie,"
    na kisha jiandae.
  • 11:25 - 11:28
    Neema hukukuta wewe mahali ulipo,
  • 11:28 - 11:30
    lakini haikuachi itakapokukuta.
  • 11:30 - 11:34
    Na neema haitofanana na Casper zimwi rafiki,
  • 11:34 - 11:35
    kwa bahati mbaya.
  • 11:35 - 11:38
    Lakini simu itapiga au barua itakuja
  • 11:38 - 11:39
    Na kisha dhidi ya vikwazo vyote,
  • 11:39 - 11:42
    utapata ucheshi wako kuhusu mwenyewe tena.
  • 11:43 - 11:46
    Kicheko kweli ni utakatifu wenye kaboni.
  • 11:47 - 11:50
    Inatusaidia kupumua tena na tena
  • 11:50 - 11:52
    Na kujipa tena,
  • 11:52 - 11:55
    Na hutupa imani katika maisha na wengine.
  • 11:56 - 12:00
    Na kumbuka - daima neema huja mwishoni.
  • 12:02 - 12:05
    Eleven: Mungu anamaanisha wema tu.
  • 12:05 - 12:07
    Hata haiogopeshi.
  • 12:07 - 12:12
    Ina maana ya kimungu au upendo,
    kimaarifa
  • 12:12 - 12:15
    au, kama tulivyojifunza kutoka kwa "Deteriorata" mkuu
  • 12:15 - 12:17
    "keki ya kikosmiki."
  • 12:18 - 12:21
    Jina jema la Mungu ni: "Sio mimi."
  • 12:22 - 12:25
    Emerson alisema mtu mwenye furaha zaidi duniani
  • 12:25 - 12:29
    ni anayejifunza ibada kutoka kwa mazingira.
  • 12:29 - 12:32
    Hivyo nenda nje na angalia juu.
  • 12:32 - 12:36
    Mchungaji wangu alisema unaweza kutega nyuki ndani ya glasi bila kufunika
  • 12:36 - 12:38
    kwa sababu hawaangalii juu,
  • 12:38 - 12:43
    hivyo wanatembea tu kwa huzuni na kuingia ndani ya glasi.
  • 12:43 - 12:45
    Nenda nje. Tazama juu
  • 12:45 - 12:46
    Siri ya maisha.
  • 12:47 - 12:49
    Na hatimaye: kifo.
  • 12:50 - 12:52
    Namba 12.
  • 12:53 - 12:54
    Wow na yikes.
  • 12:55 - 13:00
    Ni vigumu kuhimili kifo cha watu wachache tunaowapenda kwa dhati.
  • 13:00 - 13:03
    Kamwe huwezi kusahau hasara hizi, haijalishi utamaduni unasemaje,
  • 13:03 - 13:05
    hautakiwi.
  • 13:05 - 13:10
    Sisi wakristo tunapenda kufikiria kifo kama mabadiliko makubwa ya anwani,
  • 13:10 - 13:15
    Lakini katika hali yoyote, mtu huishi tena katika moyo wako
  • 13:15 - 13:17
    usipoufunga na sili.
  • 13:17 - 13:20
    Kama Leonard Cohen alisema, "Kuna nyufa katika kila kitu,
  • 13:20 - 13:22
    na ndio jinsi mwanga unavyoingia.
  • 13:22 - 13:25
    Na ndivyo tunavyojisikia wapendwa wetu wakiwa hai tena.
  • 13:27 - 13:31
    Pia, watu watakufanya ucheke kwa nguvu
  • 13:31 - 13:34
    katika mida isio sahihi,
  • 13:34 - 13:36
    na hiyo ndiyo habari njema.
  • 13:36 - 13:41
    Lakini kutokuwepo kwao pia utakuacha na ndoto mbaya na ukimisi nyumbani daima
  • 13:41 - 13:46
    Huzuni na marafiki, muda na machozi
    vitakuponya kwa kiasi fulani.
  • 13:46 - 13:50
    Machozi yatakuosha na kukubatiza
    na kukuhidrati na kukurutubisha
  • 13:50 - 13:52
    na ardhi unayotembelea.
  • 13:52 - 13:55
    Unajua kitu cha kwanza Mungu amwambia Musa?
  • 13:56 - 13:59
    Anasema, "Vua viatu vyako."
  • 13:59 - 14:03
    Kwa sababu hii ni ardhi takatifu, ushahidi wote unakanua hili.
  • 14:03 - 14:06
    Ni vigumu kuamini, lakini ni jambo la ukweli kabisa nalojua .
  • 14:06 - 14:10
    Unapokuwa mzee kidogo, kama mtoto mie,
  • 14:10 - 14:14
    unatambua kifo ni takatifu kama kuzaliwa.
  • 14:15 - 14:18
    Na hujali tena - bali uendelea na maisha yako.
  • 14:18 - 14:23
    Karibu kila kifo ni rahisi na polepole
  • 14:23 - 14:26
    pamoja na wapendwa wakikuzunguka
  • 14:26 - 14:28
    kulingana na unavyohitaji.
  • 14:28 - 14:29
    Hautokuwa peke yako.
  • 14:31 - 14:34
    Watakusaidia kuvuka kwa chochote kinachokusubiri.
  • 14:35 - 14:37
    Kama Ram Dass alisema,
  • 14:37 - 14:38
    "Yote yakishasemwa na kutendwa,
  • 14:39 - 14:42
    tunatembea tu katika nyumba ya kila mmoja wetu. "
  • 14:43 - 14:45
    Nadhani nimemaliza,
  • 14:45 - 14:47
    lakini kama nikifikiria kitu kingine chochote,
  • 14:47 - 14:48
    Nitawajulisha.
  • 14:48 - 14:49
    Ahsante.
  • 14:49 - 14:51
    (Makofi)
  • 14:51 - 14:52
    Ahsante.
  • 14:52 - 14:54
    (Makofi)
  • 14:54 - 14:56
    Nilishangaa sana nilipoulizwa kuja hapa,
  • 14:56 - 14:59
    Kwa sababu sio eneo langu,
  • 14:59 - 15:01
    Teknolojia au tarakibu au burudani.
  • 15:01 - 15:05
    Yaani eneo langu ni imani na uandishi
  • 15:05 - 15:08
    na huambatana pamoja.
  • 15:08 - 15:09
    Na nilishangaa,
  • 15:09 - 15:14
    Lakini waliniuliza niwasilishe majadiliano, na nilikubali.
  • 15:14 - 15:16
    (Video) Kama hujui utaanzia wapi,
  • 15:16 - 15:19
    kukumbuka kwamba unamiliki kila kitu kilichokutokea
  • 15:19 - 15:20
    na una haki ya kusimulia.
  • 15:20 - 15:23
    Anne Lamott: Watu wana hofu sana na kuhisi kweli wamepotea
  • 15:23 - 15:25
    katika Amerika ya leo,
  • 15:25 - 15:28
    na nilitaka tu kuwasaidia watu
    kuuona ucheshi kuhusu hilo
  • 15:28 - 15:31
    na kutambua ni kiasi gani sio tatizo.
  • 15:31 - 15:35
    Ukikuchukua hatua,
  • 15:36 - 15:39
    chukua kweli hatua katika upendo, katika kirafiki,
  • 15:39 - 15:42
    utabaki na hisia za upendo na urafiki.
Title:
Ukweli 12 niliojifunza kupitia maisha na uandishi
Speaker:
Anne Lamott
Description:

Siku chache kabla ya kutimiza miaka 61, mwandishi Anne Lamott aliamua kuandika kuhusu kila kitu alichofahamu kwa hakika. Anazama katika mihangaiko ya mwanadamu anayeishi katika ulimwengu uliochanganika, wenye uzuri na hisia, unaompa hekima na ucheshi kuhusu familia, uandishi, maana ya Mungu, kifo na zaidi.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
15:55

Swahili subtitles

Revisions