Return to Video

Simulizi letu la ubakaji na maridhiano

  • 0:00 - 0:03
    [Majadiliano yana lugha na maelezo ya ukatili wa kijinsia
  • 0:03 - 0:05
    Mtazamaji anatahadharishwa]
  • 0:05 - 0:08
    Tom Stranger: Mwaka 1996,
    nilipokuwa nina miaka 18,
  • 0:08 - 0:11
    Nilipata fursa ya kusoma nchi ngeni,
  • 0:12 - 0:16
    La kushangaza mimi ni mzaliwa wa Australia anayependa baridi ya haswa,
  • 0:16 - 0:21
    hivyo nilikuwa na furaha na njonzi
    nilipopanda ndege kwenda Iceland,
  • 0:21 - 0:24
    baada ya kuwaaga wazazi wangu na ndugu.
  • 0:25 - 0:28
    Nilikaribishwa katika familia nzuri ya wana Iceland
  • 0:28 - 0:29
    ambao walinichukua katika matembezi,
  • 0:29 - 0:32
    na kunisaidia kuielewa lugha ya tuni ya wana Iceland.
  • 0:33 - 0:36
    Mwanzo nilipambana na hisia za kutamani kurudi nyumbani
  • 0:36 - 0:38
    Baada ya shule, nilicheza mchezo wa kuteleza juu ya barafu
  • 0:38 - 0:40
    na kulala sana.
  • 0:40 - 0:44
    Masaa mawili ya Kemia katika lugha ambayo bado hujaielewa,
  • 0:44 - 0:46
    inaweza kukuweka kulala vizuri.
  • 0:46 - 0:47
    (Vicheko)
  • 0:49 - 0:51
    Mwalimu wangu ilipendekeza
    nishiriki katika igizo shuleni,
  • 0:51 - 0:54
    ilinijumuike na wengine shuleni.
  • 0:54 - 0:57
    Hata kama sikuwa sehemu ya igizo,
  • 0:57 - 0:59
    hapo nilikutana na Thordis.
  • 0:59 - 1:02
    Tulifurahia simulizi letu la penzi la ujanani,
  • 1:02 - 1:04
    tulikula wote mchana, ili tu kushika mikono
  • 1:04 - 1:06
    na kutembea jiji la Reykjavík.
  • 1:07 - 1:10
    Nilikutana na familia yake,
    naye alikutana na marafiki zangu.
  • 1:11 - 1:13
    Tulikuwa katika urafiki karibia zaidi ya mwezi
  • 1:13 - 1:16
    wakati shule iliandaa sherehe ya Krismasi
  • 1:18 - 1:21
    Thordis Elva: Nilikuwa miaka 16
    na nimekutana penzi langu la kwanza.
  • 1:22 - 1:24
    Kwenda pamoja kwa sherehe ya Krismasi
  • 1:24 - 1:26
    Ilikuwa uthibitisho wa uhusiano wetu,
  • 1:26 - 1:29
    na nilijisikia kama msichana mwenye bahati sana duniani.
  • 1:29 - 1:32
    Sio tena mtoto, lakini mwanamke.
  • 1:33 - 1:35
    mkakamavu katika upevu wangu mpya,
  • 1:35 - 1:39
    Niliamini kuwa kujaribu kunywa
    kilo kwa mara ya kwanza,
  • 1:39 - 1:42
    ulikuwa uamuzi mbaya.
  • 1:42 - 1:43
    Niliumwa sana,
  • 1:43 - 1:45
    kupoteza fahamu na kutojielewa
  • 1:45 - 1:48
    katika misukosuko ya kutapika.
  • 1:48 - 1:51
    Walinzi walitaka kuniitia gari la wagonjwa,
  • 1:51 - 1:54
    lakini Tom aliatokea kuwa mkombezi wangu,
  • 1:54 - 1:56
    na kuwaambia atanipeleka nyumbani.
  • 1:57 - 1:58
    Ilikuwa kama simulizi za vichimbakazi,
  • 1:59 - 2:00
    mikono yake yenye nguvu ikinishikilia,
  • 2:00 - 2:03
    kuniweka katika usalama wa kitanda changu.
  • 2:04 - 2:08
    Lakini shukrani yang kwake iligeuka haraka kuwa woga
  • 2:08 - 2:13
    aliponivua nguo na kupanda juu yangu.
  • 2:13 - 2:15
    nilikuwa nimepata fahamu,
  • 2:15 - 2:18
    lakini mwili wangu ulikuwa bado
    dhaifu mno kupambana,
  • 2:18 - 2:20
    na maumivu yalikuwa makali.
  • 2:21 - 2:23
    Nilidhani nimegawanywa mara mbili.
  • 2:24 - 2:25
    Ili kubaki timamu,
  • 2:25 - 2:29
    nilihesabu sekunde kwenye saa yangu.
  • 2:30 - 2:31
    Na tangu usiku huo,
  • 2:31 - 2:37
    Nimejua kwamba kuna sekunde 7200 katika masaa mawili.
  • 2:39 - 2:42
    Pamoja na kuchechmea na kulia kwa mawiki,
  • 2:42 - 2:47
    tukio hili halikuwakilisha mawazo yangu kuhusu ubakaji kama nilivyoona kwenye TV.
  • 2:47 - 2:49
    Tom hakuwa mwendawazimu mwenye silaha;
  • 2:49 - 2:51
    alikuwa mpenzi wangu.
  • 2:51 - 2:54
    Na haikutokea katika mahali pa ajabu,
  • 2:54 - 2:56
    ilitokea katika kitanda changu mwenyewe.
  • 2:57 - 3:00
    nilipotambua kwamba nimebakwa,
  • 3:00 - 3:02
    alikuwa amemaliza masomo yake
  • 3:02 - 3:04
    na kurudi kwao Australia.
  • 3:05 - 3:08
    Hivyo nilijiambia kuwa hakuna maana kufuatilia kilichotokea.
  • 3:08 - 3:09
    Na zaidi,
  • 3:09 - 3:12
    ilibidi iwe kosa langu.
  • 3:13 - 3:15
    Nilikulia katika dunia
    ambapo wasichana hufundishwa
  • 3:15 - 3:17
    kwamba wakibakwa ni kwa sababu.
  • 3:18 - 3:20
    sketi zao ni fupi mno,
  • 3:20 - 3:23
    tabasamu zao kubwa mno,
  • 3:23 - 3:25
    pumzi yao inanuka kileo.
  • 3:26 - 3:29
    Nilikuwa na hatia ya mambo hayo yote,
  • 3:29 - 3:31
    hivyo aibu ilibidi iwe yangu.
  • 3:32 - 3:33
    Ilinichukua miaka kutambua
  • 3:33 - 3:37
    kwamba jambo moja tu ilngeweza kuzuia mimi kubakwa,
  • 3:37 - 3:39
    haikuwa sketi yangu,
  • 3:39 - 3:41
    haikuwa tabasamu langu,
  • 3:41 - 3:43
    haikuwa imani yangu ya kitoto.
  • 3:44 - 3:48
    Kitu pekee ambacho kingeweza kuzuia kubakwa
  • 3:48 - 3:50
    ni aliyenibaka --
  • 3:50 - 3:52
    kama angejizuia.
  • 3:53 - 3:55
    TS: Sina kumbukumbu nzuri ya siku ya pili
  • 3:56 - 3:58
    athari ya kileo,
  • 3:58 - 4:01
    utupu niliojaribu kukandamiza.
  • 4:02 - 4:03
    Hakuna cha ziada.
  • 4:04 - 4:06
    Lakini sikuenda kwa Thordis.
  • 4:07 - 4:09
    Sasa, ni muhimu kusema
  • 4:09 - 4:12
    kwamba sikuona tendo langu kwa ubaya wake..
  • 4:13 - 4:16
    Neno "ubakaji" halikuwepo katika mawazo yangu kama ilivyotakiwa,
  • 4:17 - 4:20
    sikujisulibisha kwa kumbukumbu ya usiku uliopita.
  • 4:22 - 4:24
    Hata haikuwa mimi kukataa kwa fahamu,
  • 4:24 - 4:27
    ila zaidi kuwa kukiri ukweli wowote ni haramu.
  • 4:28 - 4:32
    Tafsiri yangu ya matendo yangu yalikanusha kutambua
  • 4:33 - 4:35
    madhara nilyomfanyia Thordis.
  • 4:36 - 4:38
    Kusema ukweli,
  • 4:38 - 4:42
    Nilikemea kitendo chote siku za baadaye
  • 4:43 - 4:44
    na wakati nilikuwa natenda.
  • 4:45 - 4:50
    Niliukataa ukweli kwa kuJIshawishi
    ilikuwa ngono sio ubakaji.
  • 4:51 - 4:55
    Na huu ni uongo umekuwa ukiniwinda.
  • 4:56 - 4:58
    Niliachana na Thordis siku kadhaa baadaye,
  • 4:58 - 5:00
    nilimuona mara kadhaa
  • 5:00 - 5:02
    katika muda wangu uliobaki Iceland,
  • 5:02 - 5:05
    nilijisikia vibaya na roho nzito kila wakati.
  • 5:06 - 5:10
    Ndani, nilijua nimekosa vibaya mno.
  • 5:11 - 5:14
    Lakini bila kukusudia, nilikandamiza kumbukumbu yote
  • 5:14 - 5:16
    ilikusahau kabisa.
  • 5:18 - 5:20
    Kilichofuata ni miaka tisa
  • 5:20 - 5:23
    ya "Kuukana na kuukimbia ukweli."
  • 5:24 - 5:28
    Nilipopata nafasi ya kutambua
    uhalisi wa unyama niliotenda,
  • 5:29 - 5:31
    sikuweza kustahamili.
  • 5:32 - 5:34
    Nilihekaheka, iwe kwa
  • 5:34 - 5:36
    matumizi ya madawa,
  • 5:36 - 5:37
    kutafuta hatari
  • 5:37 - 5:41
    au kukandamika hisia zangu,
  • 5:41 - 5:43
    Nilikataa kukaa tuli na kimya.
  • 5:45 - 5:46
    Na sauti hiyo,
  • 5:46 - 5:49
    nilitafakari katika sehemu nyingine za maisha yangu
  • 5:49 - 5:52
    ili kujenga picha ya mimi ni nani.
  • 5:53 - 5:54
    Nilikuwa surfer,
  • 5:54 - 5:56
    mwanafunzi wa sayansi za jami,
  • 5:56 - 5:58
    rafiki kwa watu wema,
  • 5:58 - 6:00
    kaka mpendwa na mwana,
  • 6:00 - 6:02
    kiongozi wa burudani za nje ,
  • 6:02 - 6:03
    na hatimaye, mfanyakazi wa mambo ya vijana.
  • 6:04 - 6:08
    Nilshikilia imani kuwa sikuwa mtu mbaya.
  • 6:09 - 6:12
    Sikudhani nilikuwa na ukatili katika mifupa yangu.
  • 6:12 - 6:14
    Nilidhani nilikuwa tofauti.
  • 6:15 - 6:16
    Katika malezi yangu,
  • 6:16 - 6:19
    upendo wa familia na jamaa,
  • 6:20 - 6:22
    watu wa karibu walikuwa wakarimu na wakweli
  • 6:22 - 6:23
    katika heshima yao kwa wanawake.
  • 6:25 - 6:30
    Ilinichukua muda mrefu kuangalia kona ya kiza changu,
  • 6:30 - 6:31
    na kujiuliza maswali hayo.
  • 6:34 - 6:36
    TE: Miaka tisa tangu ile sherehe ya Krismasi,
  • 6:36 - 6:38
    Nilikuwa nina miaka 25,
  • 6:38 - 6:40
    ninaelekea kuchanganyikiwa.
  • 6:41 - 6:45
    thamani yangu ilizikwa na usiri
  • 6:45 - 6:48
    ulionitenga kutoka kwa kila mtu niliyemjali,
  • 6:48 - 6:51
    na chuki na hasira
  • 6:51 - 6:53
    niliyoelekeza kwangu mwenyewe.
  • 6:54 - 6:56
    Siku moja, nilitoka nje
    kwa hasira na machozi
  • 6:56 - 6:58
    baada ya kugombana na mpendwa,
  • 6:58 - 7:00
    na kuingia katika café,
  • 7:00 - 7:02
    ambapo niliomba kalamu.
  • 7:03 - 7:04
    Daima nilikuwa daftari pamoja nami,
  • 7:05 - 7:08
    nikidai ilikuwa ni kwa ajili ya kuandika mawazo mapya,
  • 7:08 - 7:13
    lakini ukweli ni kwamba nilihitaji
    daima kuriaria,
  • 7:13 - 7:14
    kwa sababu katika wakati wa utulivu,
  • 7:14 - 7:17
    nilijikuta nikihesabu sekunde tena.
  • 7:18 - 7:23
    Lakini siku hiyo, nilistaajabu
    jinsi maneno yalitoka kwenye kalamu yangu,
  • 7:23 - 7:26
    kuandika barua muhimu maishani
  • 7:26 - 7:28
    kwa Tom.
  • 7:28 - 7:32
    Pamoja na nakala ya ukatili alionitendea,
  • 7:32 - 7:35
    maneno, "Nataka kutafuta msamaha"
  • 7:35 - 7:37
    yalinishangaa,
  • 7:37 - 7:39
    kunishangaza mimi hasa.
  • 7:40 - 7:44
    Lakini ndani, niligundua hio
    Ilikuwa ni njia ya kujikomboa mateso yangu,
  • 7:44 - 7:48
    kwa sababu, bila kujali kama alistahili msamaha wangu au la,
  • 7:48 - 7:51
    mimi nilistahili amani.
  • 7:51 - 7:54
    Kipindi changu cha aibu kimefika kikomo.
  • 7:56 - 7:58
    Kabla ya kutuma barua,
  • 7:58 - 8:00
    nilijitayarisha kwa kila aina
    ya majibu hasi,
  • 8:00 - 8:04
    kuliko vote:
    sikutarajia kupata jibu lolote.
  • 8:05 - 8:08
    Tokeo ambalo sikujiandaa tu
  • 8:08 - 8:10
    ndilo nililopata-
  • 8:10 - 8:15
    barua ya kukiri kutoka Tom, iliyojaa majuto.
  • 8:16 - 8:20
    Yeye pia alikuwa amefungwa katika ukimya.
  • 8:20 - 8:24
    Na huo ndio mwanzo wa mawasiliano ya yetu yaliyodumu miaka nane
  • 8:24 - 8:27
    Mungu anajua haikuwa rahisi kamwe,
  • 8:27 - 8:29
    lakini daima ukweli.
  • 8:30 - 8:33
    Nilitua dhulma yote niliyobeba,
  • 8:33 - 8:37
    na yeye, kwa moyo wote
    alikiri alichofanya.
  • 8:37 - 8:40
    Mabadilishano yetu yakawa jukwaa la
  • 8:40 - 8:42
    kuchambua matokeo ya usiku ule,
  • 8:42 - 8:45
    na ilikuwa kila kitu,
    kutoka maneno yaliyoumiza
  • 8:45 - 8:47
    hadi uponyaji kupita maelezo.
  • 8:48 - 8:52
    Na bado, haikuwa kunipa amani.
  • 8:52 - 8:56
    Labda kwa sababu barua pepe haikua binafsi ya kutosha,
  • 8:56 - 8:58
    labda kwa sababu ni rahisi kuwa jasiri
  • 8:58 - 9:02
    wakati unajificha nyuma ya kompyuta upande wa pili wa dunia
  • 9:02 - 9:04
    Lakini tulianza mjadala
  • 9:04 - 9:08
    niliyohisi ni lazima kuchunguza kikamilifu.
  • 9:08 - 9:10
    Hivyo, baada ya miaka nane ya kuandikiana,
  • 9:10 - 9:14
    na karibia miaka 16 tangia usiku ule,
  • 9:14 - 9:18
    nilikwamua ujasiri kupendekeza:
  • 9:18 - 9:19
    kwamba tukutane uso kwa uso
  • 9:19 - 9:22
    kuongelea historia yetu na kumalizana kabisa.
  • 9:25 - 9:28
    TS: Kijiografia, Iceland na Australia zipo hivi.
  • 9:29 - 9:31
    Katikati, ni Afrika Kusini.
  • 9:32 - 9:35
    Tuliamua kukutana mji wa Cape Town,
  • 9:35 - 9:37
    kwa wiki moja.
  • 9:38 - 9:42
    mji wenyewe ulikuwa ni uthibitisho fika kwa mazingira
  • 9:42 - 9:45
    ya kufikia maridhiano
    na msamaha.
  • 9:46 - 9:48
    Hakuna mahali pengine ambapo uponyaji wa mahusiano yamejaribiwa
  • 9:49 - 9:50
    kama nchini Afrika Kusini.
  • 9:51 - 9:55
    Kama taifa, Afrika Kusini walitaka
    kuishi katika ukweli wa historia,
  • 9:55 - 9:57
    na kuwasikiliza maelezo ya historia yake.
  • 9:59 - 10:03
    Kujua hii tu, athari ya Cape Town iliongezeka kwetu .
  • 10:04 - 10:05
    Katika kipindi cha wiki hio,
  • 10:05 - 10:08
    tulisimuliana hadithi ya maisha yetu kwa kila mmoja,
  • 10:08 - 10:11
    kuanzia manzo hai mwisho.
  • 10:11 - 10:14
    Na kuchambua historia yetu wenyewe.
  • 10:16 - 10:18
    Tulifuata sera kali ya kuwa wakweli,
  • 10:18 - 10:21
    hii ilimaanisha kujiweka wazi,
  • 10:21 - 10:23
    uwazi kuhusu kasoro na mapungufu yetu.
  • 10:24 - 10:26
    Kulikuwa na kukiri,
  • 10:26 - 10:29
    na wakati ambapo sote hatukuweza kudhania kabisa
  • 10:29 - 10:31
    maaumivu ya mwingine.
  • 10:32 - 10:37
    Madhara ya ukatili wa kijinsia
    yalisemwa kwa sauti na hisia,
  • 10:37 - 10:39
    uso kwa uso.
  • 10:40 - 10:41
    Wakati mwingine,
  • 10:42 - 10:44
    tuligundua ubayana uliyongezeka,
  • 10:45 - 10:50
    na hata vicheko visivyotarajiwa
    lakini vilitukomboa .
  • 10:51 - 10:53
    Ki ukweli,
  • 10:53 - 10:56
    tulijitahidi kusikilizana kwa makini.
  • 10:57 - 11:03
    Na hali halisi yetu binafsi ziliwasilihwa kwa uhalisia wake
  • 11:03 - 11:06
    kwamba hatukuweza kufanya lolote
    kuliko kurahisha uzito wa nafsi.
  • 11:09 - 11:13
    TE: Kutaka kulipiza kisasi
    ni hisia ya kawaida kama binadamu --
  • 11:13 - 11:14
    ya kiasili, hata.
  • 11:15 - 11:17
    Nilichotaka kufanya kwa miaka yote
  • 11:17 - 11:21
    ni kumdhuru Tom kama alivyoniumiza.
  • 11:22 - 11:25
    Lakini sikupata njia ya kutoa chuki na hasira yangu,
  • 11:25 - 11:27
    sina hakika kama ningekuwa nasimama hapa leo.
  • 11:28 - 11:32
    Hivyo siyo kusema kwamba sikuwa na mashaka yangu njiani.
  • 11:33 - 11:36
    Ndege ilipotua Cape Town,
  • 11:36 - 11:38
    Nakumbuka kufikiri,
  • 11:38 - 11:42
    "Kwa nini sikujipatia mtaalamu na chupa ya vodka
  • 11:42 - 11:44
    kama mtu wa kawaida? "
  • 11:44 - 11:47
    (Vicheko)
  • 11:47 - 11:51
    Wakati mwingine, utafiti wetu
    wa uelewa Cape Town
  • 11:51 - 11:53
    ulionekana kama jitihada isiyowezekana,
  • 11:53 - 11:55
    na nilitaka kukata tu tamaa
  • 11:55 - 11:57
    na kurudi nyumbani kwa mume wangu mpenzi, Vidir,
  • 11:57 - 11:58
    na mtoto wetu.
  • 12:00 - 12:02
    Lakini licha ya matatizo yetu,
  • 12:02 - 12:07
    safari hii ilileta hisia ya ushindi
  • 12:07 - 12:10
    kwamba mwanga umeshinda giza,
  • 12:11 - 12:15
    kwamba kitu chema kinaweza kujengwa kutoka kwa magofu.
  • 12:17 - 12:18
    Nilisoma mahali fulani
  • 12:18 - 12:22
    kwamba unapaswa kujaribu na kuwa mtu uliyehitaji ulipokuwa mtoto.
  • 12:22 - 12:23
    Na nilipokuwa kijana,
  • 12:23 - 12:27
    Ningependa kujua kwamba aibu haikuwa yangu,
  • 12:27 - 12:30
    kwamba kuna matumaini baada ya kubakwa,
  • 12:30 - 12:31
    kwamba unaweza hata kupata furaha,
  • 12:31 - 12:33
    kama niliyonayo na mume wangu leo.
  • 12:34 - 12:38
    Ndiyo maana niliaanza kuandika niliporudi kutoka Cape Town,
  • 12:38 - 12:41
    kitabu na mwandishi mwenzangu Tom,
  • 12:41 - 12:44
    kwamba tuna imani kinaweza kuwa msaada kwa pande zote mbili,
  • 12:44 - 12:47
    aliyetendwa na kutenda.
  • 12:47 - 12:49
    Vinginevyo,
  • 12:49 - 12:53
    ni hadithi tulipaswa kusikia tulipokuwa vijana.
  • 12:55 - 12:57
    Kutokana na hali ya hadithi yetu,
  • 12:57 - 12:59
    Najua maneno ambayo huambatana nayo -
  • 13:00 - 13:02
    muathirika, mbakaji --
  • 13:03 - 13:05
    na majina yanayotumika kuapanga dhana,
  • 13:05 - 13:09
    lakini wanaweza pia huvua utu katika vidokezo yanavyomaanisha.
  • 13:10 - 13:12
    Mtu anapoonyeshwa kama muathirika,
  • 13:12 - 13:17
    ni rahisi sana kumpuuza kama bidhaa mbovu,
  • 13:17 - 13:19
    fedheha,
  • 13:19 - 13:20
    isiyo na thamani.
  • 13:21 - 13:23
    Na vivyo hivyo, mara moja mtu
    anapoitwa mbakaji,
  • 13:23 - 13:26
    ni rahisi zaidi kumuita zimwi -
  • 13:27 - 13:28
    mnyama.
  • 13:29 - 13:32
    Lakini ni jinsi gani tutaelewa
    nini katika jamii
  • 13:32 - 13:33
    kinazalisha ukatili
  • 13:33 - 13:38
    kama sisi kunataa kutambua
    utu katika wale wanaoufanya?
  • 13:39 - 13:40

    Na jinsi -
  • 13:40 - 13:42
    (Makofi)
  • 13:42 - 13:47
    Na tunawezaje kuwawezesha waliopitia taabu kama hatuwathamini?
  • 13:48 - 13:51
    Jinsi gani tunaweza kujadili ufumbuzi
    kwa moja ya vitisho kubwa
  • 13:52 - 13:55
    katika maisha ya wanawake na watoto
    duniani kote,
  • 13:55 - 13:59
    kama majina tunayotumia
    ni sehemu ya tatizo?
  • 14:02 - 14:04
    TS: Nilichojifunza,
  • 14:04 - 14:09
    matendo yangu usiku ule mwaka 1996
    yalikuwa ya kibinafsi.
  • 14:10 - 14:12
    Nilijisikia kustahili mwili wa Thordis.
  • 14:14 - 14:17
    Nilikuwa na misingi mizuri katika malezi na kijamii
  • 14:17 - 14:19
    na mifano ya tabia usawa.
  • 14:20 - 14:21
    Lakini katika tukio hilo,
  • 14:21 - 14:23
    Nilichagua kufuata mifano mibaya.
  • 14:24 - 14:27
    Ambayo wanawake walikuwa na thamani
    ya chini ,
  • 14:28 - 14:32
    na wanaume wana hati juu ya miili yao.
  • 14:34 - 14:37
    Misukumo hii ilitokea nje kwangu.
  • 14:38 - 14:40
    Ilikuwa mimi pekee katika chumba nifanya maamuzi,
  • 14:40 - 14:42
    hakuna mtu mwingine.
  • 14:43 - 14:45
    Unapokiri kosa
  • 14:45 - 14:47
    na kweli kuchukua hatia kwa matendo yako,
  • 14:48 - 14:51
    ninaamini mambo ya kushangaza yanaweza kutokea.
  • 14:51 - 14:54
    Hiko nachoita kitendawili cha umiliki.
  • 14:55 - 14:58
    Nilidhani ningeelemewa na uzito wa wajibu.
  • 14:58 - 15:01
    Nilidhani cheti changu
    cha ubinadamu kingechomwa moto.
  • 15:02 - 15:06
    Badala yake, nilipewa umiliki wa makosa yangu,
  • 15:07 - 15:10
    na kutambua kwamba haikumiliki ukamilifu wa mimi ni nani.
  • 15:11 - 15:13
    Kurahisisha,
  • 15:13 - 15:17
    kitendo ulichofanya haliwezi kuwa Jumla ya nafsi na utu wako.
  • 15:19 - 15:20
    Sauti katika kichwa changu zilikoma.
  • 15:21 - 15:25
    Anasa ya kujihurumia iliyokuwa imekosa oksijeni,
  • 15:25 - 15:29
    na kubadilishwa
    na hewa safi ya kukubalika -
  • 15:31 - 15:35
    kukubalika kwamba nilimdhuru binadamu huyu wa ajabu anayesimama karibu na mimi;
  • 15:35 - 15:41
    kukubalika kwamba mimi ni sehemu ya kundi kubwa la kutisha la wanaume
  • 15:41 - 15:43
    ambao wamekuwa wakatili kwa wapenzi wao.
  • 15:45 - 15:47
    Usidharau nguvu ya maneno.
  • 15:48 - 15:53
    Kutubu kwa Thordis kwamba nilimbaka
    ilibadili hiari yangu na mimi mwenyewe,
  • 15:53 - 15:54
    na pia na yeye.
  • 15:56 - 15:57
    Lakini muhimu zaidi,
  • 15:57 - 16:00
    lawama ilhamishwa kutoka kwa Thordis kwangu.
  • 16:01 - 16:02
    Mara nyingi mno,
  • 16:03 - 16:07
    wajibu ni ulitokana
    kwa waathirika wa kike wa ukatili wa kijinsia,
  • 16:07 - 16:10
    na si kwa wanaume ambao kutunga yake.
  • 16:11 - 16:12
    Mara nyingi mno,
  • 16:12 - 16:17
    kuukana ukweli huwaacha wahusika mbali na ukweli.
  • 16:19 - 16:22
    Kuna mazungumzo katika umma sasa,
  • 16:22 - 16:25
    na kama watu wengi,
  • 16:25 - 16:27
    tuna imanishwa na hamasa ndogo
  • 16:27 - 16:30
    kwa majadiliano haya magumu
    lakini muhimu.
  • 16:31 - 16:35
    Ninasikia wajibu kuongeza sauti zetu.
  • 16:38 - 16:43
    TE: Tulichofanya sio formula tunayopendekeza kwa wengine.
  • 16:43 - 16:49
    Hakuna mtu ana haki ya kuwaambia mtu mwingine namna ya kushughulikia maumivu yao
  • 16:49 - 16:50
    au kosa lao mkuu.
  • 16:51 - 16:54
    Kuvunja ukimya yako si rahisi kamwe,
  • 16:54 - 16:56
    na kutegemea ni wapi katika dunia ulipo,
  • 16:56 - 16:59
    inaweza hata kuwa ni kifo
    kuzungumzia kuhusu ubakaji.
  • 17:00 - 17:04
    Nimetambua hata tukio baya la maisha yangu,
  • 17:04 - 17:07
    bado ni ushahidi wa upendeleo kwangu,
  • 17:07 - 17:10
    kwa sababu naweza kuzugumzia bila hofu ya unyanyapaa
  • 17:10 - 17:12
    au hata kuuawa.
  • 17:12 - 17:15
    Lakini pamoja na upendeleo wa kuwa na sauti
  • 17:15 - 17:18
    huja wajibu wa kuitumia.
  • 17:19 - 17:23
    Hiyo ni angalau mimi deni
    langu kwa wenzangu wasiyoweza.
  • 17:25 - 17:28
    hadithi tuliyowasilisha ni ya kipekee,
  • 17:28 - 17:33
    na bado ni ukatili wa kijinsia ni janga la kimataifa.
  • 17:33 - 17:35
    Lakini haifai kuwa njia hivyo.
  • 17:36 - 17:39
    Moja ya mambo nimeona muhimu
    katika safari yangu ya uponyaji
  • 17:39 - 17:41
    ni kujielimisha kuhusu ukatili wa kijinsia.
  • 17:41 - 17:44
    Na matokeo yake,
    Nimekuwa nikisoma, kuandika
  • 17:44 - 17:47
    na kuzungumzia suala hili kwa zaidi ya muongo mmoja sasa,
  • 17:47 - 17:49
    kwenda katika makongamano duniani kote.
  • 17:49 - 17:51
    Katika uzoefu wangu,
  • 17:51 - 17:56
    wanaohudhuria mijadala hayo
    ni karibia wanawake pekee.
  • 17:57 - 18:04
    Lakini ni wakati tuache kuona
    unyanyasaji wa kijinsia kama ya tatizo la wanawake tu.
  • 18:04 - 18:09
    (Makofi)
  • 18:17 - 18:21
    Ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na wanaume
  • 18:21 - 18:23
    unaofanywa na wanaume.
  • 18:23 - 18:27
    Na bado sauti zao haziwakilishwi ipasavyo katika mjadala huu.
  • 18:29 - 18:33
    Lakini sisi sote tunahitajika hapa.
  • 18:34 - 18:38
    Fikiria mateso tunaweza kupunguza
  • 18:38 - 18:42
    kama sisi alijitokeza uso suala hili kwa pamoja.
  • 18:43 - 18:44
    Asanteni.
  • 18:44 - 18:48
    (Makofi)
Title:
Simulizi letu la ubakaji na maridhiano
Speaker:
Thordis Elva, Tom Stranger
Description:

Mwaka 1996, Elva Thordis alifurahia penzi la utotoni na Tom Stranger, mwanafunzi kutoka Australia. Baada ya sherehe ya Krismasi shuleni, Tom alimbaka Thordis, nahawakukutani baada ya miaka mingi. Katika majadiliano hayo ya ajabu, Elva na Stranger wanazungumzia miaka ya kuishi katika aibu na usiri, na kutualika kujadili changamoto ya hii kimataifa juu ya unyanyasaji wa kijinsia katika uaminifu mpya.

Kwa mjadala, tembelea go.ted.com/thordisandtom.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
22:48

Swahili subtitles

Revisions