Return to Video

Unaweza kujua kweli kama mtoto anadanganya?

  • 0:01 - 0:02
    Habari
  • 0:02 - 0:05
    Ngoja niiulize hadhira swali:
  • 0:05 - 0:07
    Ulishawahi kudanganya ukiwa mtoto?
  • 0:07 - 0:10
    Kama uliwahi, unaweza
    kunyanyua mkono tafadhali?
  • 0:11 - 0:15
    Wow! hili ni kundi la watu wakweli
    kuliko wote niliowahi kukutana nao.
  • 0:15 - 0:17
    (Kicheko)
  • 0:17 - 0:18
    Hadi sasa kwa miaka 20 iliyopita,
  • 0:18 - 0:22
    Nimekuwa nikisoma
    jinsi watoto wanavyojifunza kudanganya.
  • 0:22 - 0:24
    Na leo, nitawashirikisha
  • 0:24 - 0:26
    baadhi ya ugunduzi tulioupata.
  • 0:27 - 0:32
    Ila kwa kuanza, nitawaambia
    hadithi kutoka kwa Bwana Richard Messina,
  • 0:32 - 0:35
    ambaye ni rafiki yangu na mkuu wa
    shule ya msingi.
  • 0:35 - 0:37
    Alipokea simu siku moja.
  • 0:39 - 0:40
    Aliyepiga akasema,
  • 0:40 - 0:44
    "Bwana Messina, mtoto wangu Johnny
    hatakuja shuleni leo
  • 0:44 - 0:46
    kwasababu anaumwa."
  • 0:46 - 0:48
    Bwana Messina akauliza,
  • 0:48 - 0:50
    "Naongea na nani, tafadhali?"
  • 0:51 - 0:52
    Na aliyepiga akasema,
  • 0:52 - 0:54
    "Mimi ni baba yangu."
  • 0:54 - 0:57
    (Kicheko)
  • 0:58 - 1:00
    Sasa hadithi hii --
  • 1:00 - 1:01
    (Vicheko)
  • 1:01 - 1:06
    inajumlisha vizuri sana
    imani tatu zilizo zoeleka tulizonazo
  • 1:06 - 1:08
    kuhusu watoto na kudanganya.
  • 1:08 - 1:13
    Moja, watoto huja tu kusema uongo
  • 1:13 - 1:15
    baada ya kuingia shule ya msingi.
  • 1:16 - 1:18
    Mbili, watoto hawadanganyi vizuri.
  • 1:18 - 1:21
    Watu wazima twaweza kugundua uwongo wao.
  • 1:21 - 1:25
    Na tatu, kama watoto watadanganya
    katika umri mdogo sana,
  • 1:25 - 1:28
    lazima watakuwa na makosa
    kitabia,
  • 1:28 - 1:32
    na watakuja kuwa
    wagonjwa wa kudanganya maishani.
  • 1:33 - 1:35
    Hivyo inaonekana kwamba
  • 1:35 - 1:37
    imani zote tatu hazikuwa sahihi.
  • 1:39 - 1:41
    Tumekuwa tukifanya mchezo wa kukisia
  • 1:41 - 1:43
    na watoto dunia nzima.
  • 1:43 - 1:45
    Huu ni mfano
  • 1:45 - 1:49
    Hivyo katika mchezo huu, tunauliza watoto
    kukisia namba kwenye kadi.
  • 1:50 - 1:53
    Na tunawaambia wakishinda mchezo,
  • 1:53 - 1:55
    watapata zawadi kubwa.
  • 1:56 - 1:57
    Lakini katikati ya mchezo,
  • 1:57 - 2:00
    tunatoa udhuru na kutoka kwenye chumba.
  • 2:02 - 2:04
    Na kabla ya kutoka kwenye chumba,
  • 2:04 - 2:07
    tunawaambia wasichungulie kwenye kadi.
  • 2:08 - 2:09
    Bila shaka,
  • 2:09 - 2:11
    tuna kamera zilizofichwa katika chumba
  • 2:11 - 2:13
    kuangalia kila hatua yao.
  • 2:14 - 2:18
    Kwasababu haja ya kushinda
    mchezo ni kubwa sana,
  • 2:18 - 2:21
    zaidi ya asilimia 90 ya watoto
    watachungulia
  • 2:21 - 2:23
    mara tutakapotoka chumbani.
  • 2:23 - 2:25
    (Kicheko)
  • 2:25 - 2:27
    Swali la msingi ni:
  • 2:27 - 2:30
    Tutakaporudi na kuuliza watoto
  • 2:30 - 2:32
    Kama wamechungulia au la,
  • 2:32 - 2:35
    watoto waliochungulia watakiri
  • 2:35 - 2:38
    au watadanganya kuhusu makosa yao?
  • 2:40 - 2:44
    Tuligundua kwamba bila kujali
    jinsia, nchi, au dini,
  • 2:45 - 2:47
    katika umri wa miaka miwili,
  • 2:47 - 2:49
    asilimia 30 hudanganya,
  • 2:49 - 2:53
    asilimia 70 husema ukweli
    kuhusu makosa yao.
  • 2:53 - 2:55
    Katika umri wa miaka mitatu,
  • 2:55 - 2:59
    asilimia 50 hudanganya na asilimia 50
    husema kweli.
  • 2:59 - 3:01
    Katika umri wa miaka minne,
  • 3:01 - 3:03
    zaidi ya asilimia 80 hudanganya.
  • 3:04 - 3:07
    Na baada ya miaka minne,
  • 3:07 - 3:08
    watoto wengi hudanganya.
  • 3:09 - 3:11
    Hivyo unaweza kuona,
  • 3:11 - 3:14
    kudanganya ni sehemu halisi
    ya kuendelea.
  • 3:14 - 3:17
    Na baadhi ya watoto huanza kusema uwongo
  • 3:17 - 3:19
    wakiwa na umri mdogo wa miaka miwili.
  • 3:20 - 3:24
    Hivyo sasa, tuangalie kwa ukaribu
    watoto wadogo.
  • 3:25 - 3:29
    Kwanini baadhi na sio wote
    watoto wadogo hudanganya?
  • 3:30 - 3:34
    Katika mapishi unahitaji viungo vizuri
  • 3:34 - 3:35
    kupika chakula kizuri.
  • 3:36 - 3:40
    Na uongo mzuri unahitaji
    viungo viwili vikuu.
  • 3:41 - 3:45
    Kiungo kikuu cha kwanza
    ni nadharia ya akili,
  • 3:45 - 3:47
    au uwezo wa kusoma- akili.
  • 3:48 - 3:50
    Kusoma akili ni uwezo wa kujua
  • 3:50 - 3:54
    kwamba watu tofauti wana
    ufahamu tofauti kuhusu hali fulani
  • 3:55 - 3:58
    na uwezo wa kutofautisha
    kati ya ninachojua
  • 3:58 - 4:00
    na kile unachojua
  • 4:00 - 4:02
    Kusoma akili ni muhimu kwa kudanganya
  • 4:02 - 4:06
    kwasababu ya msingi wa kudanganya ni najua
  • 4:06 - 4:07
    hujui
  • 4:07 - 4:08
    ninachojua.
  • 4:08 - 4:10
    Hivyo, naweza kukudanganya.
  • 4:11 - 4:16
    Kiungo cha pili muhimu
  • 4:16 - 4:20
    Ni uwezo wa kudhibiti maneno yako,
    kuonyesha hisia usoni
  • 4:20 - 4:22
    na lugha ya mwili,
  • 4:22 - 4:24
    ili kwamba unaweza kusema uongo thabiti.
  • 4:25 - 4:29
    Na tulikuta kwamba wale watoto wadogo
  • 4:29 - 4:34
    walio na uwezo mkubwa wa kusoma akili
    na uwezo wa kujidhibiti
  • 4:34 - 4:36
    husema uwongo mapema
  • 4:36 - 4:38
    na ni waongo wa kisasa.
  • 4:40 - 4:46
    Kama inavyokuwa, uwezo huu wa aina mbili
    ni muhimu pia kwetu sote
  • 4:46 - 4:48
    kuweza kufanya kazi katika jamii yetu.
  • 4:49 - 4:53
    Ki ukweli, kushindwa kusoma akili
    na uwezo wa kujidhibiti
  • 4:53 - 4:57
    vinahusianishwa na matatizo makubwa
    ya ukuaji,
  • 4:57 - 5:00
    kama ADHD na usonji.
  • 5:02 - 5:07
    Hivyo ukigundua mtoto wako wa miaka miwili
    anakudanganya kwa mara ya kwanza,
  • 5:07 - 5:09
    badala ya kushtushwa,
  • 5:09 - 5:11
    unatakiwa usherehekee--
  • 5:11 - 5:12
    (Kicheko)
  • 5:12 - 5:18
    kwasababu inaashiria kwamba mtoto wako
    amefikia hatua mpya
  • 5:18 - 5:20
    ya ukuaji wa kawaida.
  • 5:21 - 5:24
    Sasa, watoto hawadanganyi vizuri?
  • 5:25 - 5:28
    Unafikiri unaweza kugundua
    udanganyifu wao kirahisi?
  • 5:29 - 5:30
    Ungependa kujaribu?
  • 5:31 - 5:32
    Ndio? Sawa.
  • 5:32 - 5:35
    Sasa nitakuonyesha video mbili
  • 5:35 - 5:36
    Kwenye video,
  • 5:36 - 5:39
    watoto watajibu maswali ya
    utafiti,
  • 5:39 - 5:41
    "Ulichungulia?"
  • 5:41 - 5:42
    Sasa jaribu kuniambia
  • 5:42 - 5:44
    mtoto yupi anadanganya
  • 5:44 - 5:46
    na mtoto yupi anasema ukweli.
  • 5:46 - 5:48
    Huyu ni mtoto namba moja.
  • 5:49 - 5:50
    Uko tayari?
  • 5:51 - 5:53
    (Video) Mtu: Ulichungulia? Mtoto: Hapana
  • 5:54 - 5:56
    Kang Lee: Na huyu ni mtoto namba mbili.
  • 5:58 - 6:00
    (Video) Mtu: Ulichungulia? Mtoto: Hapana.
  • 6:01 - 6:05
    KL: OK, kama unafikiri
    mtoto namba moja anadanganya,
  • 6:05 - 6:07
    tafadhali inua mkono wako.
  • 6:08 - 6:12
    Na kama unafikiri mtoto namba mbili
    anadanganya, tafadhali inua mkono wako.
  • 6:14 - 6:16
    OK, kusema ukweli,
  • 6:16 - 6:19
    mtoto namba moja anasema ukweli,
  • 6:19 - 6:21
    mtoto namba mbili anadanganya.
  • 6:22 - 6:25
    Inaonekana wengi wenu sio wagunduzi
    wazuri wa uwongo wa watoto.
  • 6:25 - 6:28
    (Kicheko)
  • 6:28 - 6:31
    Sasa, tumeshiriki kwenye michezo sawasawa
  • 6:31 - 6:36
    na watu wazima wengi sana
    kutoka sehemu zote za maisha.
  • 6:37 - 6:39
    Na tunawaonyesha video nyingi.
  • 6:39 - 6:42
    Katika nusu ya video, watoto walidanganya.
  • 6:42 - 6:45
    Katika nusu ya video nyingine,
    watoto walisema ukweli.
  • 6:47 - 6:49
    Ngoja tuone
    watu wazima hawa walifanyaje.
  • 6:50 - 6:54
    Kwasababu kuna waongo wengi
    kama wasema kweli,
  • 6:54 - 6:57
    ukikisia kwa kubahatisha,
  • 6:57 - 7:01
    kunauwezekano wa asilimia 50
    ukapatia.
  • 7:01 - 7:04
    Hivyo ikiwa usahihi wako ni takriban
    asilimia 50,
  • 7:04 - 7:08
    inamaanisha wewe ni mgunduzi mbaya
    wa uwongo wa watoto.
  • 7:08 - 7:13
    Sasa tuanze na wanafunzi wa shahada
    ya kwanza na wanafunzi wa sheria,
  • 7:13 - 7:17
    ambao kwa ujumla
    hawana uzoefu na watoto.
  • 7:18 - 7:20
    Hapana hawawezi kugundua uwongo wa watoto
  • 7:20 - 7:22
    Utendaji wao ni wa kubahatisha
  • 7:22 - 7:27
    Sasa vipi kuhusu wafanyakazi za jamii
    na walinda haki za watoto,
  • 7:28 - 7:30
    wanaofanyakazi na watoto kila siku?
  • 7:30 - 7:32
    Wanaweza kugundua uwongo wa watoto?
  • 7:34 - 7:35
    Hapana, hawawezi,
  • 7:35 - 7:36
    (Kicheko)
  • 7:36 - 7:37
    Vipi kuhusu majaji,
  • 7:37 - 7:39
    maafisa forodha
  • 7:39 - 7:41
    na maafisa polisi,
  • 7:41 - 7:44
    wanaokutana na wadanganyifu kila siku?
  • 7:44 - 7:46
    Wanaweza kugundua uwongo wa watoto?
  • 7:47 - 7:48
    Hapana hawawezi.
  • 7:48 - 7:50
    Vipi kuhusu wazazi?
  • 7:50 - 7:53
    Wazazi wanaweza kugundua uwongo wa watoto
    wengine?
  • 7:54 - 7:55
    Hapana, hawawezi.
  • 7:56 - 7:59
    Inawezekana wazazi
    kugundua uwongo wa watoto wao wenyewe?
  • 8:01 - 8:02
    Hapana, hawawezi.
  • 8:02 - 8:06
    (Kicheko) (Makofi)
  • 8:06 - 8:07
    Hivyo sasa unaweza kuuliza
  • 8:09 - 8:12
    kwanini uwongo wa watoto
    ni vigumu kuugundua.
  • 8:13 - 8:16
    Ngoja niwaonyeshe hili
    na mtoto wangu mwenyewe, Nathan
  • 8:16 - 8:18
    Hii ni hisia za uso wake
  • 8:18 - 8:20
    anapodanganya.
  • 8:20 - 8:22
    (Kicheko)
  • 8:22 - 8:23
    Hivyo wakati watoto wanadanganya,
  • 8:23 - 8:27
    hisia za nyuso zao
    ni za kawaida.
  • 8:27 - 8:31
    Ingawa nyuma ya hii hisia ya kawaida,
  • 8:31 - 8:34
    mtoto kiukweli hupitia
    hisia nyingi,
  • 8:34 - 8:38
    kama hofu, hatia, fedheha
  • 8:38 - 8:41
    na pengine raha ya kudanganya kidogo.
  • 8:41 - 8:44
    (Kicheko)
  • 8:44 - 8:49
    Bahati mbaya, hisia za aina hiyo
    ni aidha za muda mfupi au zimejificha
  • 8:49 - 8:52
    Kwahiyo, ni ambazo hazionekani kwetu.
  • 8:52 - 8:53
    Kwa miaka mitano iliyopita,
  • 8:53 - 8:57
    tumekuwa tukijaribu kutafuta njia
    ya kuonyesha hisia hizi zilizojificha.
  • 8:57 - 8:58
    Kisha tukapata ugunduzi.
  • 8:59 - 9:02
    Tunajua kwamba chini ya ngozi
    za nyuso zetu,
  • 9:02 - 9:06
    kuna mtandao mkubwa wa mishipa ya damu.
  • 9:06 - 9:08
    Tunapopitia hisia tofauti,
  • 9:08 - 9:11
    msukumo wa damu usoni hubadilika
    bila kujua.
  • 9:12 - 9:16
    Na mabadiliko haya huendeshwa
    kwa mfumo wa autonomiki
  • 9:16 - 9:18
    ambayo ni nje ya uwezo wetu kudhibiti.
  • 9:18 - 9:22
    Kwa kuangalia mabadiliko ya msukumo
    wa damu usoni,
  • 9:22 - 9:25
    tunaweza kuonyesha hisia za watu
    zilizojificha.
  • 9:25 - 9:30
    Bahati mbaya, hisia hizo zinazohusiana
    na mabadiliko ya msukumo wa damu usoni
  • 9:30 - 9:33
    ni vigumu sana kugundua kwa macho yetu.
  • 9:34 - 9:37
    Hivyo kusaidia kuonyesha
    hisia za watu usoni,
  • 9:37 - 9:40
    tumeunda teknolojia mpya ya picha
  • 9:40 - 9:44
    tunaiita "tansderaml optical imaging"
  • 9:45 - 9:49
    Kufanya hivyo tunatumia kamera ya video
    ya kawaida kurekodi watu
  • 9:49 - 9:52
    wanapokuwa na hisia mbalimbali
    zilizojificha
  • 9:52 - 9:56
    Na kisha, kwa kutumia teknolojia
    ya usindikaji picha,
  • 9:57 - 10:02
    tunaweza kupata picha kupitia ngozi
    za mabadiliko ya msukumo wa damu usoni.
  • 10:04 - 10:09
    Kwa kuangalia video za picha
    kupitia ngozi,
  • 10:09 - 10:11
    sasa tunaweza kuona kwa urahisi
  • 10:12 - 10:17
    mabadiliko ya msukumo wa damu usoni
    yanayohusiana na hisia zilizojificha.
  • 10:18 - 10:20
    Na kwa kutumia teknolojia hii,
  • 10:20 - 10:24
    tunaweza kuonyesha hisia zilizojificha
    zinazohusiana na udanganyifu,
  • 10:24 - 10:27
    na kwahiyo kugundua uwongo wa watu.
  • 10:27 - 10:30
    tunaweza kufanya bila upasuaji,
  • 10:30 - 10:32
    kwa mbali, na gharama nafuu
  • 10:32 - 10:36
    kwa usahihi wa takriban asilimia 85
  • 10:36 - 10:38
    ambayo ni bora kuliko kubahatisha.
  • 10:39 - 10:43
    Na kwa kuongezea, tumegundua
    athari za Pinikio.
  • 10:44 - 10:46
    Hapana, sio athari za Pinokio huyu.
  • 10:46 - 10:47
    (Kicheko)
  • 10:47 - 10:50
    Hizi ni athari za kweli za Pinokio.
  • 10:50 - 10:51
    Wakati watu wanapodanganya,
  • 10:51 - 10:55
    msukumo wa damu usoni
    kwenye mashavu hupungua,
  • 10:55 - 10:58
    na msukumo wa damu usoni
    kwenye pua huongezeka.
  • 10:59 - 11:03
    Hata hivyo, kudanganya sio tukio pekee
  • 11:03 - 11:06
    ambalo litaamsha hisia zilizojificha.
  • 11:06 - 11:08
    Hivyo basi tukajiuliza wenyewe,
  • 11:08 - 11:10
    pamoja na kugundua uwongo,
  • 11:10 - 11:12
    teknolojia yetu inaweza kutumikaje?
  • 11:13 - 11:17
    Utumikaji wake mmoja ni kwenye elimu.
  • 11:17 - 11:21
    Kwa mfano, kwa kutumia teknolojia hii,
    tunaweza kumsaidia mwalimu huyu wa hesabu
  • 11:21 - 11:24
    kutambua wanafunzi darasani kwake
  • 11:24 - 11:29
    wanapata woga mkubwa
    kuhusu mada anayofundisha
  • 11:29 - 11:30
    ili iweze kumsaidia.
  • 11:31 - 11:34
    Na pia tunaweza kuitumia katika huduma
    za afya.
  • 11:34 - 11:37
    Mfano, kila siku natumia huduma ya
    Skype kuwasilina na wazazi wangu,
  • 11:37 - 11:40
    wanaoishi maelfu ya maili mbali.
  • 11:40 - 11:42
    Na kwa kutumia teknolojia hii,
  • 11:42 - 11:46
    Sio tu najua kinachoendelea
    katika maisha yao
  • 11:46 - 11:52
    lakini pia sambamba na kuangalia mapigo
    yao ya moyo na kiwango cha msongo,
  • 11:52 - 11:55
    hali zao na kama wanapata
    au hawapati maumivu.
  • 11:56 - 11:58
    Na pengine kwa siku za mbele,
  • 11:58 - 12:01
    hatari za mshtuko wa moyo au
    shinikizo la damu
  • 12:02 - 12:03
    Na unaweza kuuliza:
  • 12:03 - 12:09
    Tunaweza kutumia hii pia
    kuonyesha hisia za wanasiasa?
  • 12:09 - 12:11
    (Kicheko)
  • 12:11 - 12:12
    Kwa mfano, wakati wa mijadala
  • 12:13 - 12:15
    Kwakweli, jibu ni ndio.
  • 12:15 - 12:17
    Kutumia kipande kinachorushwa
    kwenye TV,
  • 12:17 - 12:21
    tunaweza kugundua mapigo ya moyo
    ya mwanasiasa,
  • 12:21 - 12:23
    hali na msongo,
  • 12:23 - 12:27
    na pengine katika siku za mbele.
    iwe wanatudanganya au sivyo.
  • 12:27 - 12:30
    Tunaweza pia kutumia hii
    katika utafiti wa masoko,
  • 12:31 - 12:32
    kwa mfano, kujua
  • 12:32 - 12:37
    kama watu wanapenda au hawapendi
    bidhaa fulani za matumizi.
  • 12:37 - 12:39
    Tunaweza hata kutumia kwenye miadi.
  • 12:40 - 12:41
    Sasa kwa mfano
  • 12:41 - 12:44
    Ikiwa mliyeahidiana anakuonyesha tabasamu,
  • 12:44 - 12:46
    teknolojia hii inaweza kukusaidia kujua
  • 12:47 - 12:49
    kama anakupenda kweli
  • 12:49 - 12:51
    au anajaribu tu kuonyesha wema kwako.
  • 12:52 - 12:54
    Na kwa suala hili,
  • 12:54 - 12:55
    anajaribu kuonyesha wema kwako.
  • 12:55 - 12:58
    (Kicheko)
  • 12:59 - 13:03
    Hivyo teknolojia ya transdermal optical
    imaging
  • 13:03 - 13:06
    iko katika hatua za mwanzo za kuendelezwa.
  • 13:06 - 13:10
    Matumizi mengi mapya yatakuja
    ambayo hatuyajui leo.
  • 13:10 - 13:13
    Ingawa, kitu kimoja ninachojua kwa uhakika
  • 13:13 - 13:17
    ni kwamba kudanganya
    hakutakuwa kama zamani tena.
  • 13:17 - 13:18
    Asanteni sana.
  • 13:18 - 13:19
    Asanteni.
  • 13:19 - 13:23
    (Makofi)
Title:
Unaweza kujua kweli kama mtoto anadanganya?
Speaker:
Kang Lee
Description:

Je watoto hawadanganyi vizuri? Unafikiri unaweza kugundua uwongo wao kwa urahisi? Mtafiti wa maendeleo Kang Lee amechunguza nini kinatokea kisaikolojia kwa watoto wanapodanganya. Wanafanya mara nyingi kuanzia umri mdogo wa miaka miwili, na hakika wanafanya vizuri kweli. Lee anaelezea kwanini tusherehekee wakati watoto wanaanza kudanganya na kuwasilisha teknolojia mpya ya kugundua uwongo ambayo siku moja itaonyesha hisia zetu zilizojificha.

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
13:36

Swahili subtitles

Revisions