Return to Video

Kwa nini waathirika wa unyanyasaji majumbani hawaondoki

  • 0:01 - 0:04
    Leo niko hapa kuongea kuhusu swala nyeti,
  • 0:04 - 0:08
    ambalo lina jibu tatanishi.
  • 0:08 - 0:11
    Swala langu ni zile siri za ugomvi nyumbani,
  • 0:11 - 0:14
    na swali nitakalokabiliana nalo
  • 0:14 - 0:18
    ni lile swali moja kila mmoja huliuliza kila mara:
  • 0:18 - 0:19
    Kwa nini muathirika hubakia?
  • 0:19 - 0:23
    Kwa nini mtu yeyote abaki na mume ampigaye?
  • 0:23 - 0:26
    Mie si daktari wa akili, mfanyakazi wa ustawi wa jamii
  • 0:26 - 0:29
    au mtaalam wa ugomvi wa nyumbani.
  • 0:29 - 0:32
    Mimi ni mwanamke mwenye hadithi ya kusimulia.
  • 0:32 - 0:36
    Nilikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili. Nilikuwa nimehitimu tu kutoka chuo cha Harvard.
  • 0:36 - 0:39
    Nilikuwa nimehamia mjini New York kwa ajili ya kazi yangu ya kwanza
  • 0:39 - 0:42
    kama mwandishi na mhariri wa gazeti la Seventeen.
  • 0:42 - 0:44
    Nilikuwa na nyumba yangu ya kwanza,
  • 0:44 - 0:48
    kadi yangu ya kwanza ya American Express,
  • 0:48 - 0:51
    na nilikuwa na siri moja kubwa sana.
  • 0:51 - 0:54
    Siri yangu ilikuwa kwamba kulikuwa na bunduki
  • 0:54 - 0:58
    iliyojaa risasi iliyoelekezwa kichwani mwangu
  • 0:58 - 1:00
    na mwanamme niliyefikiria alikuwa mpenzi wangu,
  • 1:00 - 1:04
    mara kadhaa.
  • 1:04 - 1:07
    Mwanamme huyu niliyempenda kuliko yeyote duniani
  • 1:07 - 1:11
    alielekeza bunduki kichwani mwangu na kutishia kuniua
  • 1:11 - 1:15
    mara nyingi kuliko zile ningeweza kukumbuka.
  • 1:15 - 1:17
    Niko hapa kuwapa hadithi ya upendo wa kupindukia,
  • 1:17 - 1:20
    mtego wa kisaikolojia uliofichwa kama mapenzi,
  • 1:20 - 1:23
    ambao mamilioni ya wanawake na hata wanaume wengine
  • 1:23 - 1:26
    hutumbukia kila mwaka.
  • 1:26 - 1:28
    Inaweza hata kuwa hadithi yako.
  • 1:28 - 1:32
    Sionekani kama mtu niliyenusurika na ugomvi katika mahusiano.
  • 1:32 - 1:34
    Nina shahada ya sanaa katika Kiigereza kutoka chuo cha Harvard,
  • 1:34 - 1:36
    na shahada ya juu katika mauzo kutoka kwa chuo cha biashara cha Wharton.
  • 1:36 - 1:39
    Nimetumia muda mrefu maishani nikifanya kazi kwenye kampuni bora duniani
  • 1:39 - 1:44
    zikiwemo Johnson & Johnson, Leo Burnett na The Washington Post.
  • 1:44 - 1:48
    Nimeolewa takriban miaka ishirini kwa mme wangu wa pili
  • 1:48 - 1:50
    na tuna wana watatu pamoja
  • 1:50 - 1:55
    Mbwa wangu ni mweusi, na mie huendesha gari ndogo la Honda Odyssey.
  • 1:55 - 1:57
    (Kicheko)
  • 1:57 - 2:00
    Kwa hivyo ujumbe wangu wa kwanza kwenu ni kwamba ugomvi wa nyumbani
  • 2:00 - 2:02
    humtokea yeyote--
  • 2:02 - 2:06
    kila jamii,dini, kila kipato na ngazi ya kimasomo.
  • 2:06 - 2:08
    Iko kila mahali.
  • 2:08 - 2:11
    Na ujumbe wangu wa pili ni kwamba kila mtu hufikiri
  • 2:11 - 2:13
    ugomvi wa nyumbani huwaathiri wanawake,
  • 2:13 - 2:15
    ati ni swala la wanawake.
  • 2:15 - 2:17
    Si sahihi.
  • 2:17 - 2:21
    Zaidi ya asili mia 85 ya wanyanyasaji ni wanaume, na ugomvi wa nyumbani
  • 2:21 - 2:27
    hutokea haswa katika mahusiano ya undani, ya kutegemeana na yale ya muda mrefu,
  • 2:27 - 2:30
    yaani, katika familia,
  • 2:30 - 2:33
    mahali tusipotaka au kutarajia kupata ugomvi,
  • 2:33 - 2:38
    ndio sababu tuhuma za kinyumbani ni tatanishi hivi.
  • 2:38 - 2:41
    Ningekuambia kwamba ningekuwa mtu wa mwisho duniani
  • 2:41 - 2:44
    kukaa na mwanaume anayenipiga,
  • 2:44 - 2:47
    lakini kusema kweli nilikuwa mwathirika kwa sababu ya umri wangu.
  • 2:47 - 2:51
    Nilikuwa mwenye umri wa miaka ishirini na mbili na Marekani,
  • 2:51 - 2:54
    wanawake wenye umri kati ya miaka kumi na sita hadi ishirini na nne wana uwezekano wa mara tatu zaidi
  • 2:54 - 2:57
    kuwa waathirika wa ugomvi wa nyumbani
  • 2:57 - 3:00
    ikilinganishwa na wanawake wa umri mwingine,
  • 3:00 - 3:03
    vilevile zaidi ya wanawake mia tano na wasichana wa umri huu
  • 3:03 - 3:07
    huuawa kila mwaka na wapenzi wanyanyasaji,
  • 3:07 - 3:11
    wapenzi, na waume zao Marekani.
  • 3:11 - 3:15
    Nilikuwa muathirika kwa sababu sikujua chochote
  • 3:15 - 3:19
    kuhusu ugomvi wa nyumbani, maonyo yake ama mifano yake.
  • 3:19 - 3:24
    Nilikutana na Conor usiku mmoja wenye baridi na mvua, mwezi wa Januari.
  • 3:24 - 3:27
    Alikaa kando yangu kwenye treni katika mji wa New York,
  • 3:27 - 3:29
    na alianza kuniongelesha.
  • 3:29 - 3:31
    Aliniambia mambo mawili.
  • 3:31 - 3:35
    La kwanza kuwa, yeye pia, alikuwa amehitimu kutoka kwa kati ya zile shule bora zaidi Marekani,
  • 3:35 - 3:39
    na kwamba alifanya kazi kwenye benki moja ya kuvutia sana huko Wall Street.
  • 3:39 - 3:43
    Lakini kile kilichonivutia zaidi siku hiyo
  • 3:43 - 3:46
    ni kuwa alikuwa mwerevu na mcheshi
  • 3:46 - 3:48
    na alionekana kuwa kijana wa mashambani.
  • 3:48 - 3:50
    Alikuwa na haya mashavu makubwa, haya mashavu makubwa ya waridi
  • 3:50 - 3:52
    na hii nywele za rangi kama ya ngano,
  • 3:52 - 3:55
    na alionekana kuwa mwema sana.
  • 3:55 - 3:59
    Jambo moja la busara Conor alilofanya, kutoka mwanzoni,
  • 3:59 - 4:04
    lilikuwa kufanya kana kwamba nilikuwa mwenye ushawishi mkubwa katika huo uhusiano.
  • 4:04 - 4:07
    Alifanya hivi haswa hapo mwanzo
  • 4:07 - 4:09
    kwa kunihusudu.
  • 4:09 - 4:13
    Tukaanza kutoka pamoja, na alipenda kila kitu kunihusu,
  • 4:13 - 4:14
    ati nilikuwa mwerevu, ati nilisomea chuo cha Harvard,
  • 4:14 - 4:17
    ati nilikuwa mwenye shauku kusaidia wasichana wadogo, na kazi yangu.
  • 4:17 - 4:20
    Alitaka kujua kila kitu kuhusu familia yangu
  • 4:20 - 4:23
    na utoto wangu na matarajio na ndoto zangu.
  • 4:23 - 4:26
    Conor alikuwa na imani nami, kama mwandishi na mwanamke,
  • 4:26 - 4:30
    kwa njia ambayo yeyote mwengine alikuwa hajawahi.
  • 4:30 - 4:34
    Na alileta uaminifu kati yetu
  • 4:34 - 4:37
    kwa kunieleza siri yake,
  • 4:37 - 4:41
    ambayo ilikuwa, alipokuwa mvulana mdogo sana akiwa na umri wa miaka minne
  • 4:41 - 4:44
    alipigwa vibaya sana mara kwa mara
  • 4:44 - 4:46
    na babake wa kambo,
  • 4:46 - 4:50
    na unyanyasaji ulizidi kuwa mbaya zaidi hadi ikambidi aache shule akiwa daraja la nane,
  • 4:50 - 4:52
    ingawa alikuwa mwerevu sana,
  • 4:52 - 4:56
    na kwamba alitumia takriban miaka ishirini kujenga maisha yake upya.
  • 4:56 - 4:59
    Ndiyo sababu hiyo shahada yake kutoka zile shule bora zaidi Marekani,
  • 4:59 - 5:02
    na kazi yake Wall Street na maisha yake mazuri siku za usoni
  • 5:02 - 5:04
    zilikuwa za umuhimu mkubwa sana kwake.
  • 5:04 - 5:06
    Kama ungeniuliza
  • 5:06 - 5:12
    kama huyu mwanamme mwerevu, mcheshi na mwenye kujali aliyenipenda sana
  • 5:12 - 5:16
    angekuja kuniamulia kama ningejipamba au la,
  • 5:16 - 5:18
    ufupi wa sketi zangu,
  • 5:18 - 5:20
    mahali ningeishi, kazi gani ningefanya,
  • 5:20 - 5:23
    marafiki zangu wangekuwa wepi na pale ningekulia Krisimasi
  • 5:23 - 5:25
    ningekucheka,
  • 5:25 - 5:28
    kwa sababu hakukuwa na ushahidi wowote wa tuhuma au uthibiti
  • 5:28 - 5:32
    au hasira kutoka kwa Conor hapo mwanzoni.
  • 5:32 - 5:35
    Sikujua kwamba daraja la kwanza
  • 5:35 - 5:37
    katika uhusiano wowote wenye ugomvi
  • 5:37 - 5:41
    ni kumvuta na kumpumbaza mwathirika
  • 5:41 - 5:46
    Pia sikujua kuwa daraja ya pili ni kumtenga mwathirika.
  • 5:46 - 5:50
    Conor hakuja nyumbani siku moja na kutangaza,
  • 5:50 - 5:53
    "Unajua huu uhusiano wetu kama wa Romeo na Julieti umekuwa mtamu,
  • 5:53 - 5:55
    lakini nataka kwenda katika hatua inayofuata
  • 5:55 - 5:59
    ambapo nitakutenga na kukunyanyasa" - (Kicheko) -
  • 5:59 - 6:01
    "kwa hivyo nataka kukuhamisha kutoka nyumba hii
  • 6:01 - 6:02
    ambapo majirani wanawezakusikia ukipiga mayowe
  • 6:02 - 6:05
    na kukupeleka nje ya mji huu ambapo una marafiki na familia
  • 6:05 - 6:08
    na wafanyakazi wenzako wanaoweza kuona hiyo michubuko."
  • 6:08 - 6:12
    Badala yake, Conor alikuja nyumbani jioni ya Ijumaa moja
  • 6:12 - 6:15
    na akaniambia kuwa alikuwa ameacha kazi siku hiyo,
  • 6:15 - 6:17
    kazi ya ndoto zake,
  • 6:17 - 6:22
    na akasema kwamba alikuwa ameacha kazi hiyo kwa sababu yangu,
  • 6:22 - 6:25
    kwa sababu nilimfanya ahisi usalama na kupendwa
  • 6:25 - 6:28
    ati hakuhitaji tena kujithibitisha huko Wall Street,
  • 6:28 - 6:30
    na alitaka tu kutoka mjini
  • 6:30 - 6:33
    na kukaa mbali na familia yake iliyomnyanyasa.
  • 6:33 - 6:36
    na kuhamia mji mdogo wa New England
  • 6:36 - 6:40
    ambapo angeweza kuanza upya maisha yake nikiwa kando yake.
  • 6:40 - 6:44
    Sikutaka kamwe kuhama kutoka New York,
  • 6:44 - 6:48
    na kuacha kazi ya ndoto zangu,
  • 6:48 - 6:50
    lakini nilifikiria mtu hujitoa muhanga kwa mpenzi wake,
  • 6:50 - 6:54
    kwa hivyo nikakubali na nikaacha kazi yangu,
  • 6:54 - 6:56
    na Conor na mimi tukaondoka Manhattan pamoja.
  • 6:56 - 7:01
    Sikuwai kufikiria kwamba penzi nililokuwa nalo halikuwa la kawaida,
  • 7:01 - 7:04
    na kwamba nilikuwa nikitembea bila habari ndani ya
  • 7:04 - 7:09
    mtego mzuri wa kimwili, kifedha na kiakili
  • 7:09 - 7:11
    Daraja ya pili katika ugomvi wa kimahusiano
  • 7:11 - 7:16
    ni kuleta tishio la vurugu
  • 7:16 - 7:18
    na kuangalia vile linavyomgusa.
  • 7:18 - 7:21
    Na hapa ndipo bunduki zinapoingia.
  • 7:21 - 7:24
    Muda tu tulipohamia New England--unajua,
  • 7:24 - 7:26
    mahali Connor aliposema pangemfanya ajisikie salama--
  • 7:26 - 7:29
    alinunua bunduki tatu.
  • 7:29 - 7:32
    Aliweka moja garini.
  • 7:32 - 7:35
    Aliweka moja chini ya mto kitandani mwetu,
  • 7:35 - 7:38
    na ya tatu alitembea nayo mfukoni nyakati zote.
  • 7:38 - 7:40
    Na alisema alihitaji bunduki hizo
  • 7:40 - 7:43
    kwa sababu ya uchungu aliopitia akiwa mchanga.
  • 7:43 - 7:46
    Alizihitaji kujisikia salama.
  • 7:46 - 7:49
    Lakini bunduki hizo zilikuwa ujumbe kwangu,
  • 7:49 - 7:51
    na ingawa hakuwai kuninyoshea mkono,
  • 7:51 - 7:57
    maisha yangu tayari yalikuwa hatarini kila dakika ya kila siku.
  • 7:57 - 8:01
    Kwanza Conor alinishambulia
  • 8:01 - 8:03
    siku tano kabla ya harusi yetu.
  • 8:03 - 8:08
    Ilikuwa saa moja asubuhi na bado nilikuwa nimevalia vazi la kulala
  • 8:08 - 8:12
    Nilikuwa nafanya kazi kweny kompyuta yangu nikijaribu kumaliza kazi fulani ya uandishi,
  • 8:12 - 8:14
    na nilikuwa nimekasirika,
  • 8:14 - 8:17
    na Conor akatumia hasira zangu kama kisingizio
  • 8:17 - 8:20
    kunikaba koo
  • 8:20 - 8:24
    na kuikaza hadi sikuweza kupumua au kupiga kelele,
  • 8:24 - 8:26
    na alitumia mkazo huo
  • 8:26 - 8:30
    kugonga kichwa changu mara kadhaa kwenye ukuta.
  • 8:30 - 8:35
    Siku tano baadaye, ile michubuko kumi shingoni mwangu ilipotea
  • 8:35 - 8:38
    na nikavaa nguo ya mama yangu ya harusi,
  • 8:38 - 8:40
    na nikafunga ndoa naye.
  • 8:40 - 8:42
    Licha ya yaliyotokea,
  • 8:42 - 8:46
    nilikuwa na hakika tungeishi maisha ya raha milele,
  • 8:46 - 8:50
    kwa sababu nilimpenda, na alinipenda sana.
  • 8:50 - 8:53
    Na aliniomba msamaha.
  • 8:53 - 8:57
    Alikuwa amechoshwa sana na mipango ya harusi yetu
  • 8:57 - 8:59
    na kwa kuwa kitu kimoja na mimi.
  • 8:59 - 9:00
    Halikuwa jambo la kawaida
  • 9:00 - 9:04
    na asingeniumiza tena.
  • 9:04 - 9:07
    Ilitokea mara mbili katika fungate.
  • 9:07 - 9:10
    Mara ya kwanza, nilikuwa naendesha gari kutafuta ufukwe wa siri
  • 9:10 - 9:12
    na nikapotea,
  • 9:12 - 9:15
    na akanipiga ngumi nzito kwenye upande wa kichwa changu
  • 9:15 - 9:18
    hata ule upande mwengine wa kichwa changu ukagonga
  • 9:18 - 9:20
    dirisha lililo kando ya dereva mara kadhaa.
  • 9:20 - 9:23
    Alafu tena siku chache baadaye, tukielekea nyumbani baada ya likizo ya harusi,
  • 9:23 - 9:26
    alikasirishwa na trafiki,
  • 9:26 - 9:29
    na akarusha Big Mac baridi usoni mwangu.
  • 9:29 - 9:32
    Conor aliendelea kunipiga mara moja au mbili kwa wiki
  • 9:32 - 9:35
    kwa miaka miwili na nusu ya ndoa yetu.
  • 9:35 - 9:38
    Nilifanya makosa kufikiria nilikuwa wa kipekee
  • 9:38 - 9:41
    na peke yangu katika hali hii.
  • 9:41 - 9:43
    Mmoja kati ya wanawake watatu wakiAmerika
  • 9:43 - 9:47
    hupitia ugomvi wa nyumbani ama kufuatwa fuatwa wakati mmoja maishani mwake,
  • 9:47 - 9:51
    na CDC inaripoti kwamba watoto milioni kumi na tano
  • 9:51 - 9:54
    wananyanyaswa kila mwaka, milioni kumi na tano.
  • 9:54 - 9:59
    Hivyo basi, nilikuwa kwenye ushirika mzuri sana.
  • 9:59 - 10:01
    Kurudia swali langu:
  • 10:01 - 10:03
    Kwa nini nilibaki?
  • 10:03 - 10:06
    Jibu lenyewe ni rahisi.
  • 10:06 - 10:09
    Sikujua alikuwa akininyanyasa.
  • 10:09 - 10:13
    Hata ingawa alielekeza bunduki zilizo na risasi kichwani mwangu,
  • 10:13 - 10:15
    akanisukuma ngazini,
  • 10:15 - 10:16
    akatishia kuua mbwa wetu,
  • 10:16 - 10:20
    akatoa ufunguo wa gari nikiendesha barabarani,
  • 10:20 - 10:23
    akamwaga maganda ya kahawa kichwani mwangu
  • 10:23 - 10:25
    nikijitayarisha kwa mahojiano ya kazi,
  • 10:25 - 10:29
    SIkuwai hata mara moja kujihisi kuwa mke anayenyanyaswa.
  • 10:29 - 10:33
    Badala yake, nilikuwa mwanamke mwenye nguvu
  • 10:33 - 10:35
    alimpenda sana mwanaume aliyekuwa na shida,
  • 10:35 - 10:37
    na nilikuwa mtu wa pekee duniani
  • 10:37 - 10:41
    ambaye angeweza kumsaidia Conor kukabiliana na mashetani yake.
  • 10:41 - 10:45
    Swali lingine kila mtu huuliza ni,
  • 10:45 - 10:47
    kwa nini hatoki tu?
  • 10:47 - 10:51
    Kwa nini sikuondoka? Ningeweza kuondoka wakati wowote.
  • 10:51 - 10:56
    Kwangu mimi, hili ndilo swali chungu na la kuhuzunisha zaidi ambalo watu huniuliza,
  • 10:56 - 10:59
    kwa sababu sisi waathiriwa tunajua jambo nyinyi msilojua:
  • 10:59 - 11:03
    Ni jambo la hatari sana kumtoroka mnyanyasaji.
  • 11:03 - 11:06
    Kwa sababu daraja ya mwisho katika tuhuma za kinyumbani
  • 11:06 - 11:09
    ni kumuua.
  • 11:09 - 11:12
    Zaidi ya asilimia sabini ya vifo vinavyosababishwa na tuhuma za kinyumbani
  • 11:12 - 11:16
    hutokea baada ya mwathiriwa kukatiza uhusiano huo,
  • 11:16 - 11:18
    baada ya kutoka,
  • 11:18 - 11:21
    kwa sababu wakati huo mnyanyasaji hana chochote cha kupoteza.
  • 11:21 - 11:24
    Matokeo mengine ni pamoja na kufuatwa fuatwa,
  • 11:24 - 11:27
    hata baada ya mnyanyasaji kuoa tena;
  • 11:27 - 11:29
    unyimaji wa hela;
  • 11:29 - 11:32
    na uingiliaji wa mfumo wa mahakama za kifamilia
  • 11:32 - 11:34
    ili kumtia wasiwasi mwathirika na wanawe,
  • 11:34 - 11:39
    ambao mara kwa mara hushurutishwa na majaji wa mahakama za kifamilia
  • 11:39 - 11:41
    kuwa na wakati usiosimamiwa
  • 11:41 - 11:45
    pamoja na mtu yule aliyemtuhumu mama yao.
  • 11:45 - 11:49
    Na bado twauliza, kwa nini hamtoroki tu?
  • 11:49 - 11:51
    Niliweza kuondoka,
  • 11:51 - 11:54
    kwa sababu ya kipigo kibaya cha mwisho
  • 11:54 - 11:57
    kilichofumbua macho yangu.
  • 11:57 - 12:00
    Nilitambua kwamba mtu yule niliyempenda sana
  • 12:00 - 12:03
    angekuja kuniua kama ningeendelea kumuacha hivi hivi tu.
  • 12:03 - 12:06
    Hivyo nikavunja ukimya.
  • 12:06 - 12:08
    Nikawaeleza watu wote:
  • 12:08 - 12:12
    polisi, jirani zangu,
  • 12:12 - 12:16
    marafiki zangu na familia, wageni,
  • 12:16 - 12:23
    na niko hapa leo kwa sababu nyote mlinisaidia.
  • 12:23 - 12:25
    Tuna tabia ya kuwabagua waathirika
  • 12:25 - 12:29
    kama vichwa vibaya vya habari,
  • 12:29 - 12:32
    wanaojitakia maovu, watu walioharibika.
  • 12:32 - 12:35
    Swali hilo, "Kwa nini haondoki?"
  • 12:35 - 12:40
    kwa wengine ni kama kusema, "Ni makosa yake kuendela kukaa hapo,"
  • 12:40 - 12:44
    kana kwamba waathirika huchagua kusudi kupenda wanaume
  • 12:44 - 12:46
    walio na lengo la kutumaliza.
  • 12:46 - 12:49
    Lakini tangu niandike kitabu "Crazy Love,"
  • 12:49 - 12:52
    nimesikia mamia ya hadithi kutoka kwa wanaume na wanawake
  • 12:52 - 12:55
    ambao pia waliondoka,
  • 12:55 - 12:59
    waliojifunza somo muhimu la maisha kutokana na yale yaliyotokea,
  • 12:59 - 13:03
    na waliojenga maisha yao tena--maisha yenye furaha
  • 13:03 - 13:06
    kama wafanyakazi, wake na kina mama,
  • 13:06 - 13:10
    maisha yasiyo na unyanyasaji, kama yangu.
  • 13:10 - 13:15
    Kwa sababu inaonekana kwamba mimi nilikuwa mwathirika halisi wa unyanyasaji majumbani.
  • 13:15 - 13:18
    na msalimika wa unyanyasaji wa majumbani.
  • 13:18 - 13:22
    Niliolewa na mtu mwema na mpole,
  • 13:22 - 13:24
    na pamoja tuna watoto watatu.
  • 13:24 - 13:28
    Nina yule mbwa wangu mweusi, na nina lile gari ndogo.
  • 13:28 - 13:31
    Kile sitawahi kuwa nacho tena,
  • 13:31 - 13:34
    milele,
  • 13:34 - 13:36
    ni bunduki iliyojaa risasi iliyoelekezwa kichwani mwangu
  • 13:36 - 13:40
    na mtu anayesema eti ananipenda.
  • 13:40 - 13:43
    Wakati huu, labda unafikiria,
  • 13:43 - 13:44
    "Hili ni jambo la kushangaza,"
  • 13:44 - 13:48
    ama, "Kwa nini alikuwa mjinga hivi,"
  • 13:48 - 13:54
    lakini muda huu wote, nimekuwa haswa nikiongea juu yako.
  • 13:54 - 13:57
    Nakuhakikishia kuna watu kadhaa
  • 13:57 - 13:59
    wanaonisikiliza saa hii
  • 13:59 - 14:02
    ambao wananyanyaswa
  • 14:02 - 14:04
    au ambao walinyanyaswa wakiwa watoto
  • 14:04 - 14:08
    au walio wanyanyasaji wenyewe.
  • 14:08 - 14:10
    unyanyasaji unaweza kuwa unamwathiri binti yako,
  • 14:10 - 14:15
    dadako, rafiki yako wa karibu wakati huu.
  • 14:15 - 14:18
    Niliweza kumaliza hadithi yangu wazimu ya mapenzi
  • 14:18 - 14:21
    kwa kuvunja ukimya.
  • 14:21 - 14:23
    Bado naendelea kuvunja ukimya leo.
  • 14:23 - 14:27
    Ni njia yangu ya kusaidia waathirika wengine,
  • 14:27 - 14:30
    na ni ombi langu la mwisho kwenu.
  • 14:30 - 14:33
    Ongeeni kuhusu mliyosikia hapa.
  • 14:33 - 14:36
    Unyanyasaji hushamiri tu katika ukimya.
  • 14:36 - 14:40
    Una nguvu ya kumaliza unyanyasaji majumbani
  • 14:40 - 14:44
    kwa kuongea kuhusu unyanyasaji.
  • 14:44 - 14:47
    Sisi waathirika tunahitaji kila mtu.
  • 14:47 - 14:51
    Tunawahitaji nyote kuelewa
  • 14:51 - 14:55
    siri za unyanyasaji majumbani.
  • 14:55 - 14:58
    Mulikieni mwanga unyanyasaji kwa kuuongelea
  • 14:58 - 15:00
    mkiwa na watoto wenu, wafanyakazi wenzenu,
  • 15:00 - 15:02
    marafiki zenu na familia.
  • 15:02 - 15:05
    Ongeleeni waliosalimika kama watu wema na wanaopendeka
  • 15:05 - 15:08
    walio na maisha kamili kwenye siku za usoni
  • 15:08 - 15:11
    Eleweni ishara za mapema za tuhuma
  • 15:11 - 15:14
    na muingilie kati kistadi
  • 15:14 - 15:18
    malizeni na muonyeshe waathirika njia safi ya kuiepuka.
  • 15:18 - 15:22
    Pamoja tunaweza kufanya vitanda vyetu,
  • 15:22 - 15:26
    meza zetu za mlo na familia zetu
  • 15:26 - 15:29
    mahali pa amani zinavyopaswa kuwa
  • 15:29 - 15:31
    Asanteni.
  • 15:31 - 15:39
    (Mahali)
Title:
Kwa nini waathirika wa unyanyasaji majumbani hawaondoki
Speaker:
Leslie Morgan Steiner
Description:

Leslie Morgan Steiner alikuwa katika "penzi la wazimu" -- yaani, alimpenda sana mwanaume aliyemnyanyasa mara kwa mara na kumtishia maisha. Steiner anahadithia uhusiano wake, akisahihisha maoni potofu ya watu wengi kuhusiana na waathirika wa unyanyasaji wa majumbani , na kueleza vile wote tunavyoweza kumaliza kimya hicho. (Imerekodiwa katika TEDxRainier.)

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDTalks
Duration:
15:59

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions